Je ni nani anaweza kubatizwa na kushiriki meza ya Bwana? Kabla ya kujibu swali hili tunaweza kuona kwanza kuna makundi mawili ambao ni watu wakubwa na watoto.Hawa wote wanahita wakati sahihi wa kubatizwa na kushiriki meza ya Bwana. Kanuni ya kuzingatia ya neno la Mungu ni moja kwa watu wakubwa na watoto, ambayo ni kumwamini Yesu na kutubu dhambi zao. Lakini kwa upande wa watoto wadogo bado hawajafikia ukomavu, kujitegemea na kuamini. Kwa hiyo ni jukumu la wazazi, walezi na kanisa kuendelea kuwafundisha neno la Mungu. Na hatimaye wakati utafika na kuweza kupambanua neno na kumtegemea Mungu katika maisha yao. Kwa sababu hiyo siyo sahihi kuwabatiza na kuwashirikisha meza ya Bwana watoto. Yesu alifundisha katika kitabu cha“Marko 16:16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.” Kama alivyosema Yesu hapa juu anayeami ndiye atabatizwa. Kwa sababu hiyo watoto bado hajafikia umri ambao wanaweza kuamini na kujitegemea katika neno la Mungu. Pia kwa upande wa watu ...
Tunaposoma katika biblia tunaweza kuona ahadi mbalimbalii ambazo Mungu ameahidi kwa ajili watoto wake. Ni wale ambao wameokolewa na Yesu na kuishi sawasawa na neno la Mungu.Kwa sababu wamedumu katika neno lake anawatimizia ahadi zake. Lakini ili yatimie yale aliyoahidi katika neno lake kuna mambo ya kuzingatia.Ni haya yafuatayo; 1. Kusoma neno lake na kufahamu ahadi zake. 2. Kuamini yale aliyoahidi katika neno lake.Tunawe kuona jinsi Ibrahimu alivyomwamini Mungu, katika kitabu cha “Warumi 4:20-22.Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu; huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi. Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki.” 3. Kuomba kwa imani sawasawa na yale aliyoahidi. Daudi ni kielelezo cha kuigwa aliomba akasema, “Dua yangu na ifike mbele zako,Uniponye sawasawa na ahadi yako.ZABURI 119:170.” Aliomba hivyo kwa sababu alikuwa anajua ahadi za Mungu. 4. Kuomba mapenzi yake yatimie sawasawa na ahadi za...