Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

KUBATIZWA NA KUSHIRIKI MEZA YA BWANA

 Je ni nani anaweza kubatizwa na kushiriki meza ya Bwana? Kabla ya kujibu swali hili tunaweza kuona kwanza kuna makundi mawili ambao ni watu wakubwa na watoto.Hawa wote wanahita wakati sahihi wa kubatizwa na kushiriki meza ya Bwana. Kanuni ya kuzingatia ya neno la Mungu ni moja kwa watu wakubwa na watoto, ambayo ni kumwamini Yesu na kutubu dhambi zao. Lakini kwa upande wa watoto wadogo bado hawajafikia ukomavu, kujitegemea na kuamini. Kwa hiyo ni jukumu la wazazi, walezi na kanisa kuendelea kuwafundisha neno la Mungu. Na hatimaye wakati utafika na kuweza kupambanua neno na kumtegemea Mungu katika maisha yao. Kwa sababu hiyo siyo sahihi kuwabatiza na kuwashirikisha meza ya Bwana watoto. Yesu alifundisha katika kitabu cha“Marko 16:16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.” Kama alivyosema Yesu hapa juu anayeami ndiye atabatizwa. Kwa sababu hiyo watoto bado hajafikia umri ambao wanaweza kuamini na kujitegemea katika neno la Mungu.   Pia kwa upande wa watu ...
Machapisho ya hivi karibuni

AHADI ZA MUNGU KWA AJILI YAKO

Tunaposoma katika biblia tunaweza kuona ahadi mbalimbalii ambazo Mungu ameahidi kwa ajili watoto wake. Ni wale ambao wameokolewa na Yesu na kuishi sawasawa na neno la Mungu.Kwa sababu wamedumu katika neno lake anawatimizia ahadi zake. Lakini ili yatimie yale aliyoahidi katika neno lake kuna mambo ya kuzingatia.Ni haya yafuatayo; 1. Kusoma neno lake na kufahamu ahadi zake. 2. Kuamini yale aliyoahidi katika neno lake.Tunawe kuona jinsi Ibrahimu alivyomwamini Mungu, katika kitabu cha “Warumi 4:20-22.Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu;  huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi. Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki.” 3. Kuomba kwa imani sawasawa na yale aliyoahidi. Daudi ni kielelezo cha kuigwa aliomba akasema, “Dua yangu na ifike mbele zako,Uniponye sawasawa na ahadi yako.ZABURI 119:170.” Aliomba hivyo kwa sababu alikuwa anajua ahadi za Mungu. 4. Kuomba mapenzi yake yatimie sawasawa na ahadi za...

FAHAMU KUHUSU MADHABAHU

Kuhusu somo hili tuweza kuona,nini maana ya madhabahu na ilivyotumika.  Madhabahu ni mahali palipotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kumtolea Mungu sadaka mbali mbali za kuteketezwa kama sadaka za dhambi na amani. Jambo hilo lilifanyika wakati wa agano la kale. Mungu ndiye aliyetoa maelekezo ya kuijenga madhabahu kwa kutumia mawe. Wakati huo Musa lipewa hayo maelekezo, “Kumbukumbu la Torati 27:5-75 Na huko umjengee madhabahu Bwana, Mungu wako, madhabahu ya mawe, usitumie chombo cha chuma juu yake. 6 Jenga hiyo madhabahu ya Bwana, Mungu wako, kwa mawe yasiyochongwa; ukamtolee Bwana, Mungu wako, sadaka za kuteketezwa juu yake; 7 ufanye na sadaka za amani, ukale huko; nawe furahi mbele za Bwana, Mungu wako." Kwa hiyo sadaka ziliwekwa juu ya madhabahu na kutekelezwa mbele za Bwana. Kwa wakati huu wa agano jipya hatujengi tena madhabahu ya mawe na kuteketeza sadaka juu yake. Ni kwa sababu Yesu Kristo alikuja kama sadaka ya ulimwengu na kufa msalabani. Kwa sababu hiyo kwa damu yake iliyo...

TEGEMEO NA TUMAINI LIKO KWA MUNGU.

Jinsi ya Kumtegemea Mungu ni pale unapoweka tumaini kwake. Kwa sababu hiyo unakuwa umemtumaini.  Ili uweze kuwa na Mungu katika maisha yako yakupasa kumtegemea na kumtumaini. Kwa hiyo jambo la muhimu  yakupasa kumtegemea na kumtumaini katika mambo yote.  Unaweza kumtegemea na kumtumaini sawasawa na ahadi za neno lake. Hatua inayofuata amini ahadi ya neno lake na kuomba. Lakini posipo kumtegemea na kumtumaini yeye unakuwa umepoteza uhusiano wako na yeye. Na kama utaweka tegemeo na tumaini lako katika mali zako, au kitu kingine chochote, unakuwa umemwacha Bwana. Imeandikwa katika"Yeremia 17:5-8 BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.  Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.  Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA, Ambaye BWANA ni tumaini lake.  Maana atakuwa kama mti ul...

KUKUMBUKWA NA MUNGU

Kuna watumishi wa Mungu katika biblia ambao walikumbukwa na Mungu. Ni kwa sababu walikuwa na sifa njema mbele zake. Mojawapo ya sifa hizo, walikuwa wameyatoa maisha yao kwake ili kumpendeza. Kwa sababu hiyo Waliisha sawasawa na neno lake.  Walikuwa wakitii kwa kila neno ambalo Mungu aliwaagiza, ndio maana wamekumbukwa kwa  ajili ya mema yao katika vizazi vingi. Kwa sababu hiyo watu kama hao Mungu alipendezwa nao. Wamekuwa kielelezo kwa watu wengine. Watu kama hao wakiondoka hapa duniani watakumbukwa.  Hapa nitawataja baadhi ya watu katika biblia ambao wamekumbukwa  ni Ibraimu, Musa na Daudi. Ni vema kufahamu ya kwamba mtu mwenye sifa njema, amepanda wema katika maisha yake na vizazi vyake.  Kwa soma hili tunajifunza ya kwamba yatupasa tuangalie jinsi tunavyo enenda mbele za Mungu. Ili tukiondoka hapa duniani tuache sifa njema mbele za Mungu na wanadamu. Kwa sababu ya sifa njema uzao wako unabarikiwa. Kuna watu wengine hawakutii maagizo yake wamekumbukwa kwa ajil...

USISAHAU KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Yakupasa kuwa makini sana usisahau kuishi maisha ya ukamilifu. Unaweza kusahau mambo mengine, lakini jambo hili la ukamilifu yakupasa kuzingatia wakati wote. Tafakari kila wakati je wewe ni mkamilifu?. Ni muhimu kuishi kwa ukamilifu kwa sababu hujui saa wala wakati ambao utaondoka hapa duniani. Siku ile ya mwisho inakuja ghafla na kanisa litanyakuliwa. Hiyo ni siku ambayo hakuna anayeijua. Wale w alio tayari katika ukamilifu hao ndio watakaonyakuliwa. Wale ambao si wakamilifu wataachwa na hatimaye watahukumu na kutupwa katika ziwa la moto.  Kuliko utengwe na uso wa Mungu milele ni bora kuishi katika ukamilifu.   kwa sababu  hiyo yakupasa kudumu na kuyafanya mambo yote kwa ukamilifu mbele za Mungu na wanadamu. Kwa hiyo ufanywe umempendeza  Mungu na kupata kibali kwake.  Ni muhimu kudumu katika ukamilifu wakati wote, ukiwa umelala, unatembea, unakula, unapoongea na watu, unaposafiri, unapokuwa katika shughuli zako mbalimbali. Ndugu, tambua ya kwamba Mungu ana...

HATUA ZA KUUKULIA WOKOVU NA NEEMA YA MUNGU

Mwaminini Mungu; Neno hili hapa juu  ambalo ni kichwa cha soma hili Yesu ndiye alisema wakati akiwa na wanafunzi wake. " Marko 11:21-22 Petro akakumbuka habari yake, akamwambia, Rabi, tazama, mtini ulioulaani umenyauka. Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu." Jinsi ya kuamini. Kumwamini Mungu ni pale mkristo anapomtumaini na kumtegemea  katika moyo wake. Kwa hiyo neno lake Mungu linaonyesha wazi ni mtu mwenye haki ndiye atakayeishi kwa kumwamini yeye . Imeandikwa "Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye. Waebrania 10:38" Kutokana na hili somo hapa juu linaonyesha wazi ya kwamba kusudi la Mungu ni mwanadamu aishi kwa kumtumaini na kumtegemea yeye. Ndio maana pia amesema katika " Yeremia 17:5-7 B WANA asema hivi,  Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu. Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake  Na moyoni mwake amemwacha BWANA. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jang...