Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

KUWEKWA HURU KUTOKA DHAMBI YA UZINZI NA UASHARATI.

Jambo la kwanza ninamshukuru Mungu kwa neema yake aliyonipa kufundisha neno lake. Ndungu mpendwa ninajua ya kwamba Mungu alikupenda sana, hata akamtoa Mwana wake wa pekee Yesu Kristo kwa ajili yako ili akukomboe kutoka katika dhambi zote ikiwemo dhambi ya uzinzi na uasherati. Sasa ninakusihi kwa neema ya Mungu fuatana nami kwa makini kuhusu  somo hili nawe utauna utukufu wa Mungu katika maisha yako. Tunaweza kuangalia kwa makini dhambi ya uzinzi na uasharati ambayo mtu akiitenda inaharibu ufahamu wake na hatimaye kuangamia. Mtu anapoteza uhusiano wake na Mungu, mawasiliano kati yake na Mungu yanakatika. Mungu  ni Makatifu hana ushirika na wenye dhambi. “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.” Mithali 6:26.   “Lakini maovu yenu yamewafarikisha (yamewatenganisha) ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki  kusikia.”   Isahau 59:2. Atendaye dhambi ya zinaa au  uasherati ...
Machapisho ya hivi karibuni

USISAHAU KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Yakupasa kuwa makini sana usisahau kuishi maisha ya ukamilifu. Unaweza kusahau mambo mengine, lakini jambo hili la ukamilifu yakupasa kuzingatia wakati wote. Tafakari kila wakati je wewe ni mkamilifu?. Ni muhimu kuishi kwa ukamilifu kwa sababu hujui saa wala wakati ambao utaondoka hapa duniani. Siku ile ya mwisho inakuja ghafla na kanisa litanyakuliwa. Hiyo ni siku ambayo hakuna anayeijua. Wale w alio tayari katika ukamilifu hao ndio watakaonyakuliwa. Wale ambao si wakamilifu wataachwa na hatimaye watahukumu na kutupwa katika ziwa la moto.  Kuliko utengwe na uso wa Mungu milele ni bora kuishi katika ukamilifu.   kwa sababu  hiyo yakupasa kudumu na kuyafanya mambo yote kwa ukamilifu mbele za Mungu na wanadamu. Kwa hiyo ufanywe umempendeza  Mungu na kupata kibali kwake.  Ni muhimu kudumu katika ukamilifu wakati wote, ukiwa umelala, unatembea, unakula, unapoongea na watu, unaposafiri, unapokuwa katika shughuli zako mbalimbali. Ndugu, tambua ya kwamba Mungu ana...

HATUA ZA KUUKULIA WOKOVU NA NEEMA YA MUNGU

Mwaminini Mungu; Neno hili hapa juu  ambalo ni kichwa cha soma hili Yesu ndiye alisema wakati akiwa na wanafunzi wake. " Marko 11:21-22 Petro akakumbuka habari yake, akamwambia, Rabi, tazama, mtini ulioulaani umenyauka. Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu." Jinsi ya kuamini. Kumwamini Mungu ni pale mkristo anapomtumaini na kumtegemea  katika moyo wake. Kwa hiyo neno lake Mungu linaonyesha wazi ni mtu mwenye haki ndiye atakayeishi kwa kumwamini yeye . Imeandikwa "Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye. Waebrania 10:38" Kutokana na hili somo hapa juu linaonyesha wazi ya kwamba kusudi la Mungu ni mwanadamu aishi kwa kumtumaini na kumtegemea yeye. Ndio maana pia amesema katika " Yeremia 17:5-7 B WANA asema hivi,  Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu. Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake  Na moyoni mwake amemwacha BWANA. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jang...

MKRISTO WA KWELI.

Mkristo wa kweli ni mtu yule ambaye ameokoka na kukionja kipawa cha nguvu za Mungu. Na pia ametoa mwili wake kuwa sadaka kwa Mungu. Kwa sababu hiyo kwa kufanya hivyo ni ibada kwa Mungu.  Ndio maana imandikwa kwenye  "Warumi 12:1   Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana."  Lakini pia  anakuwa na shauku au kiu kwa ajili ya kumwabudu Mungu. Kwa sababu hiyo, wakristo wa namna hiyo wanapokuwa katika kumwabudu Mungu watauona uzuri wa Mungu na uwepo wa nguvu zake.Wanatamani wakati wote kudumu katika utakatifu. Pia hujilinda na kuepuka kufanya dhambi. Huyapenda mambo ya Mungu kuliko ya dunia.Vilevile huwa ni watu mwenye bidii katika kumtafuta Mungu kwa kuomba, kufunga na kumsifu Mungu. Jambo lingine hawapendezwi na mambo yasiyo ya haki. Watu kama hao ndio watakaourithi ufalme wa Mungu. Ni kwa sababu wameshinda majaribu ya yule maovu na ndani yao hamna hila...

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

MUNGU NDIYE ATENDAYE MIUJIZA.

Tunaweza kuona ya kwamba vitu vyote ambavyo Mungu ameviumba ni muujiza kwetu. Pia aliumba kwa namna ya pekee jua, mwezi, nyota na sayari nyingine mbalimbali ambazo  aliziweka juu ya anga, huku zikiwa zinaning’inia bila kushikiliwa na kitu chochote, wala hazidondoki. Pia bahari nayo imekaa mahali ilipoamriwa bila kuvuka mpaka alioiwekea Bwana. Kwa hiyo tunapoona uumbaji wa vitu vyote ambavyo Mungu aliviumba vinashangaza, navyo ni ishara  kwetu ya kutosha na kutambua ya kwamba Mungu yupo. Kwa sababu hiyo yatupasa kufahamu ya kwamba yeye ndiye mwenye uwezo wote, yeye hutenda mambo yote sawasawa na mapenzi yake. Kwa hiyo tunaweza kuona Sababu ya Mungu kufanya muujiza kwa mkono wa Musa mbele ya Farao na Wamisri. Mungu akamwambia Farao; “lakini, nilikusimamisha wewe kwa sababu hii hii, ili nikuonyeshe uweza wangu, tena kwamba jina langu litangazwe katika dunia yote.” Kutoka 9:16. Kutokana na andiko hili hapa juu linazungumzia Mungu alifanya miujiza ili kumwonyesha Farao uweza wake....

KULEA WATOTO KATIKA MAADILI MEMA 1.

M zazi au mlezi yampasa kufahamu ya kwamba yeye mfano wa kuigwa katika familia. Kwa kawaida watoto hujifunza mambo wanayoyaona au kusikia kwa wazazi, walezi, Waalimu na watu wengine. Kwa hiyo watoto kuwa na maadili mema au mabaya ni kutokana na malezi ya pande zote. Kwa kawaida watoto walivyo bado hawajaweza kupambanua yaliyo mema na mabaya. Lakini wakielimishwa wanaweza kutambua  yaliyo mema na mabaya. Kuna mambo ya muhimu ambayo mtoto anapaswa kufundishwa ni haya yafuatayo: 1.Kumfundisha mtoto kusema neno asante. Neno asante ni muhimu kwa kila mtu apewapo kitu au kutendewa jambo lolote jema. Kwa hiyo yampasa kusema neno  asante. Kwa kufanya hivyo ni jambo jema na pia ni maadili kwa watu wa rika zote. Kama mtu mzima hatoi shukrani kwa yale mema ambayo ametendewa huenda yamkini hakulelewa tangu akiwa mtoto ya kwamba yampasa akipewa chakula au amemnunulia nguo aseme asante, au anapopewa kitu chochote na wazazi wake. Usipomlea mtoto katika maadali mema atakapokuwa mtu mzima h...

USHUHUDA WA MAONO YA MBINNGUNI NA JEHANUM. NA NYISAKI CHAULA.

Huu ni ushuhuda wa maono juu ya mbinguni na Jehanamu uliotolewa na mwanamke Nyisaki Chaula.  Nyisaki Chaula ni mtumishi wa Mungu, mkazi wa mkoa wa Mbeya nchni Tanzania Yesu Kristo aliye hai alimchukua na kumwonyesha maono hayo, na ilikuwa mwezi desemba mwaka 1991. Yesu Kristo alimpa maono hayo, akamwagiza aandike na kushuhudia maono hayo kwa kanisa lake na watu wote, ili kila mwanadamu apate kufahamu uhalisi wa mbinguni na Jehanamu, makao yanayowasubiri wanadamu wote baada ya maisha ya hapa duniani. Hii si habari ya kutungwa, ni jambo la kweli ambalo lilitokea. Usome ujumbe huu kwa moyo uliofunguka, huku ukimwomba Mungu akuwezeshe kuuelewa na pia kuwaeleza wengine. Ujumbe huu umenukuliwa kama ulivyoandikwa na mwanamke Nyisaki Chaula mwenyewe, ambaye alionyeshwa maono haya! USHUHUDA WA MAONO YA JEHANAMU. NA NYISAKI CHAULA. UYOLE – MBEYA, TANZANIA . UTANGULIZI Nduguyangu kuna shuhuda nyingi sana zinazoletwa duniani, kuhusu mbinguni na jehanamu, lakini ni watu wachach...