Ruka hadi kwenye maudhui makuu

FAHAMU KUHUSU MADHABAHU

Kuhusu somo hili tuweza kuona,nini maana ya madhabahu na ilivyotumika. 

Madhabahu ni mahali palipotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kumtolea Mungu sadaka mbali mbali za kuteketezwa kama sadaka za dhambi na amani. Jambo hilo lilifanyika wakati wa agano la kale. Mungu ndiye aliyetoa maelekezo ya kuijenga madhabahu kwa kutumia mawe.

Wakati huo Musa lipewa hayo maelekezo, “Kumbukumbu la Torati 27:5-75 Na huko umjengee madhabahu Bwana, Mungu wako, madhabahu ya mawe, usitumie chombo cha chuma juu yake.

6 Jenga hiyo madhabahu ya Bwana, Mungu wako, kwa mawe yasiyochongwa; ukamtolee Bwana, Mungu wako, sadaka za kuteketezwa juu yake;

7 ufanye na sadaka za amani, ukale huko; nawe furahi mbele za Bwana, Mungu wako."

Kwa hiyo sadaka ziliwekwa juu ya madhabahu na kutekelezwa mbele za Bwana.

Kwa wakati huu wa agano jipya hatujengi tena madhabahu ya mawe na kuteketeza sadaka juu yake.

Ni kwa sababu Yesu Kristo alikuja kama sadaka ya ulimwengu na kufa msalabani. Kwa sababu hiyo kwa damu yake iliyomwagika pale msabani kwa ajili yakutusafisha dhambi zetu. Jambo hili alithibitisha Yohana mbatizaji kama ilivyoandikwa  katika kitabu cha "Yohana 1:29  Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!" Pia imeandikwa katika "1 Yohana 1:7 bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote."

Neno madhabahu linatumika kwa namna isiyo sahihi katika nyumba ya ibada. Kwenye nyumba ya kuabudia ile sehemu ya mbele kuitwa ni madhabahu siyo sahihi. Wakati huu wa agano jipya hakuna madhabahu na wala hatujengi madhabahu. Kwa sababu hiyo madhabahu ilijengwa na kutumika wakati wa agano la kale. Ndio maana hatutoi sadaka za kutekeleza. 

Jambo lingine ni kuhusu damu ya Yesu ambayo ilimwagika mara moja tu pale msalaba kwa ajili ya msamaha wa dhambi. Kwa sababu hiyo ni muhimu kuwa makini na kuzingatia neno la Mungu linavyosema kuhusu matumizi ya damu ya Yesu. Pia ni muhimu kuepuka kuitumia damu ya Yesu au neno madhabahu kwa namna isiyo sahihi bila uthibitisho wa neno la Mungu. 

Siyo sahihi kuitumia damu ya Yesu wakati wa kukemea pepo na kusema kwa damu ya Yesu pepo toka au kumwombea mtu damu ya Yesu imfunike na kumlinda. Yesu aliagiza akasema mtatoa pepo kwa jina langu. Wala hakusema mtatoa pepo kwa damu yangu. 

Ni muhimu kujifunza neno la Mungu kwa bidii na kulifahamu. Kwa hiyo kupita neno la Mungu ndio uthibitisho katika maisha yako, na kwa kila jambo unalolifanya. Kwa sababu hiyo zingatia kwa kila jambo unalolifanya ni sawa na neno la Mungu.

Ni muhimu kufahamu kazi ya damu ya Yesu ni kuosha dhambi. Ndio maana imeandikwa katika, "Ufunuo wa Yohana 1:5 ... kwa Yesu Kristo, shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake,"

Endelea kusoma zaidi,

MATUMIZI YA DAMU YA YESU

Maoni

  1. Bila jina08:59

    Kwasasa hivi hakuna madhabahu

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...