Tunaposoma katika biblia tunaweza kuona ahadi mbalimbalii ambazo Mungu ameahidi kwa ajili watoto wake. Ni wale ambao wameokolewa na Yesu na kuishi sawasawa na neno la Mungu.Kwa sababu wamedumu katika neno lake anawatimizia ahadi zake.
Lakini ili yatimie yale aliyoahidi katika neno lake kuna mambo ya kuzingatia.Ni haya yafuatayo;
1. Kusoma neno lake na kufahamu ahadi zake.
2. Kuamini yale aliyoahidi katika neno lake.Tunawe kuona jinsi Ibrahimu alivyomwamini Mungu, katika kitabu cha “Warumi 4:20-22.Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu;
huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.
Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki.”
3. Kuomba kwa imani sawasawa na yale aliyoahidi. Daudi ni kielelezo cha kuigwa aliomba akasema, “Dua yangu na ifike mbele zako,Uniponye sawasawa na ahadi yako.ZABURI 119:170.” Aliomba hivyo kwa sababu alikuwa anajua ahadi za Mungu.
4. Kuomba mapenzi yake yatimie sawasawa na ahadi zake. Lakini mtu anakuwa ameomba vibaya pale anaposema lazima atafanya. Kusema hivyo siyo sahihi kwa sababu yeye hufanya yote kwa mapenzi yake. Ndio maana Yesu alifundisha jinsi ya kuomba akasema,“Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,
Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni. Mathayo 6:9-10.”
5.Kumtegemea na kumtumaini Mungu kwa yale yote aliyoahidi. Daudi alimtumaini Mungu katika neno akasema “Nami nitamjibu neno anilaumuye, Kwa maana nalitumainia neno lako. Zaburi 119:42.” Kwenye kitabu cha Yeremia Mungu amesema,
“Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.Yeremia 17:7.”
Kutokana na andiko hili linamaanisha ya kwamba atakuwa amepokea baraka za Bwana. Ina maana anayapokea yale aliyokuwa anayahitaji kwa kumtegemea na kumtumaini Mungu.
Kumbuka ni muhimu kusoma neno la Mungu na kuzingatia uliyojifunza katika somo hili. Ikiwa utafanya hivyo utafahamu ahadi za Mungu.
Hapa nitazitaja baadhi ya ahadi
kama ifuatavyo;
1.Ahadi ya uponyaji.
“Mithali 3:7-8
Usiwe mwenye hekima machoni pako; Mche Bwana,ukajiepushe na uovu. Itakuwa afya mwilini pako, Na mafuta mifupani mwako.”
“Kutoka 23:25 Nanyi mtamtumikia Bwana, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako.”
2.Ahadi ya ulinzi na kuokolewa.
“Zaburi 34:7
Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.”
“Zaburi 50:15
Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.”
Maoni
Chapisha Maoni