Jinsi ya Kumtegemea Mungu ni pale unapoweka tumaini kwake. Kwa sababu hiyo unakuwa umemtumaini.
Ili uweze kuwa na Mungu katika maisha yako yakupasa kumtegemea na kumtumaini. Kwa hiyo jambo la muhimu yakupasa kumtegemea na kumtumaini katika mambo yote.
Unaweza kumtegemea na kumtumaini sawasawa na ahadi za neno lake. Hatua inayofuata amini ahadi ya neno lake na kuomba.
Lakini posipo kumtegemea na kumtumaini yeye unakuwa umepoteza uhusiano wako na yeye. Na kama utaweka tegemeo na tumaini lako katika mali zako, au kitu kingine chochote, unakuwa umemwacha Bwana. Imeandikwa katika"Yeremia 17:5-8 BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA.
Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.
Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea BWANA, Ambaye BWANA ni tumaini lake.
Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji,
Uenezao mizizi yake karibu na mto;
Hautaona hofu wakati wa hari ujapo,
Bali jani lake litakuwa bichi;
Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua,
Wala hautaacha kuzaa matunda."
Kumbuka kumtegemea na kumtumaini Mungu, kwa sababu yeye ndiye atayekusaidi wakati wa shida. Kwa sababu hiyo usiweke tegemeo na tumaini katika mali uliyo nayo au kitu chochote ulicho nacho.
Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa; "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka, Mathayo 11:12 ." " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu." Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...
Maoni
Chapisha Maoni