Je ni nani anaweza kubatizwa na kushiriki meza ya Bwana?
Kabla ya kujibu swali hili tunaweza kuona kwanza kuna makundi mawili ambao ni watu wakubwa na watoto.Hawa wote wanahita wakati sahihi wa kubatizwa na kushiriki meza ya Bwana.
Kanuni ya kuzingatia ya neno la Mungu ni moja kwa watu wakubwa na watoto, ambayo ni kumwamini Yesu na kutubu dhambi zao. Lakini kwa upande wa watoto wadogo bado hawajafikia ukomavu, kujitegemea na kuamini. Kwa hiyo ni jukumu la wazazi, walezi na kanisa kuendelea kuwafundisha neno la Mungu. Na hatimaye wakati utafika na kuweza kupambanua neno na kumtegemea Mungu katika maisha yao.
Kwa sababu hiyo siyo sahihi kuwabatiza na kuwashirikisha meza ya Bwana watoto. Yesu alifundisha katika kitabu cha“Marko 16:16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.”
Kama alivyosema Yesu hapa juu anayeami ndiye atabatizwa. Kwa sababu hiyo watoto bado hajafikia umri ambao wanaweza kuamini na kujitegemea katika neno la Mungu.
Pia kwa upande wa watu wakubwa baadi yao hawastahilli kushiriki meza ya Bwana kwa sababu ni wenye dhambi. Kwa hiyo ni muhimu kutambua meza ya Bwana ni takatifu. Kwa hiyo katika hao wenye dhambi walioshiriki baadhi yao waliugua na kufa.
Ndiyo maana imeandikwa katika kitabu cha “1 Wakorintho 11:27-31
27 Basi kila aulaye mkate huo, au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa amejipatia hatia ya mwili na damu ya Bwana.
28 Lakini mtu ajihoji mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe.
29 Maana alaye na kunywa, hula na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kutokuupambanua ule mwili.
30 Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio hawawezi na dhaifu, na watu kadha wa kadha wamelala.
31 Lakini kama tungejipambanua nafsi zetu, tusingehukumiwa.”
Ni muhimu kufahamu maana ya neno "kupambanua" linamaanisha kutofautisha vizuri kati ya mambo mawili au zaidi kwa kutumia akili, maarifa, au uchambuzi wa kina.
Pia ni kuchambua kwa undani ili kuelewa tofauti au maana halisi ya jambo.
Maoni
Chapisha Maoni