Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia 2012

MAADILI YA NENO LA MUNGU.

Mungu alituumba kwa kusudi la kuishi katika maadili ya neno lake, ndio maana imeandikwa,   “Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo”   Waefeso 2:10.  Mavazi ya mwanamke Neno lake Mungu linatufundisha maadili ya mavazi ya kuvaa kwa mwanamke.     Vivyo hivyo wanawake wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri…"  1Timotheo 2:9.   Ikiwa mwanamke amevaa gauni fupi, linalobana au lililopasuli na kuonyesha sehemu zake za mwili ambazo hazipaswi kuonekana wazi  anajiabisha na kujivunjia heshima mbele za Mungu na jamii. Kujichubua uso ni kuondoa rangi ya asili aliyoumbwa nayo. Kunyoa nyusi na kupaka    rangi badala ya nyusi na kuvaa nywele badia, haya si maadili ya neno la Mungu.       Mwanamke afanyaye  mambo kama haya hapa juu anampinga  na kumkosoa muumbaji wake ambaye ni Mungu.  Ni sawa na kumwambia alikosea alivyomu...

KUEPUKA DHAMBI

Kutokusamehe wengine Kitendo cha kutosamehe  wanaokukosea ni dhambi kama dhambi zingine . Kusamehe ni agizo la Mungu na ni wajibu wako . “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe makosa yenu”     Mathayo 6:14,15.   Unapokosewa usingoje kuombwa msamaha unapaswa kumsamehe aliyekukosea kwa wakati huo huo.   Unapomsamehe aliyekukosea unakuwa na amani na utulivu ndani ya moyo wako na ndio maana imeandikwa,   “ Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo;-------”   Mithali 4:23. Unapolinda moyo wako unakuwa salama. Ili kuendelea kuwa salama yakupasa uepuke ugomvi, mabishano na maneno yasiyofaa,    hayo hayana maana huleta uharibifu katika moyo wako.     Maneno yasiyo maana Kwa maadili ya Mungu ametuumba kwa ajili ya mema katika kutenda na kusema. Anataka tumpendeze yeye katika mambo yote, na ndipo tutaurithi ufalme wa Mun...

MAOMBI - 2.

Mwendelezo wa somo la maombi   lililotangulia. Karibu endelea kujifunza. 5.   Kuomba kwa bidii bila kukata tamaa. Maombi ya namna hii ni dua, unamwomba Mungu tena na tena hadi anakupa unachokihitaji. Ukisoma habari za Watumishi wa Mungu walifanya maombi ya dua na kupokea waliyoyahitaji. Na si hivyo tu, Bwana wetu Yesu Kristo alifanya dua na kutufundisha kuomba kwa bidii na kupokea.   “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi,akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu”   Waebrania 5:7. “Akawaambia mfano, imewapasa kumwomba Mungu siku zote, wala wasikate tamaa, Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu. Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, nipatie haki na adui wangu. Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu na kujali watu, lakini, kwa kuwa mjane huyu a...

MAOMBI - 1.

Neno   MAOMBI   linamaanisha kupeleka  hitaji/mahitaji  mbele za Mungu kwa ajili ya kupatiwa msaada.  Unapomwomba Mungu kitu chochote ni muhimu ujue anakusikia. Ni sawa na mtoto anapomwomba baba yake kalamu au daftari anamsikia na kumpa.Unapomuomba Mungu unaongea na Baba yako wa mbinguni naye anakusikia kama baba wa dunia hii anavyomsikiliza mtoto wake.   “ Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe? Au akiomba samaki, atampa nyoka? Basi ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! si zaidi sana Baba yenu aliye  mbinguni atawapa mema   (mahitaji)   wao wamwombao”?     Mathayo 7:9-11. Jinsi ya kuomba 1.   Kuomba kwa imani. Ili uombe kwa imani ni lazima uwe na imani, na imani inapatikana katika neno la Mungu.   “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja neno la Kristo”   Warumi 10:17.   Unapomwomba Mungu ni lazima uamini kile kitu ambacho umemwomba am...

UBATIZO.

Maana ya neno ubatizo. Neno ubatizo linatokana na neno la Kiyunani baptizo. Maana ya neno baptizo ni kuzamisha.                   Kubatizwa ni agizo la Mungu.   Mungu alimtuma Yohana aje duniani kuhubiria watu watubu dhambi zao na kuwabatiza. “Tubuni, kwa maana  ufalme wa Mungu umekaribia” Mathayo 3:2. “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordan; Naye akawabatiza katika mto Yordani, huku wakiziungama dhambi zao” Mathayo 3:5,6. Asiyeye kubali kabatizwa atahukumiwa.     Kubatizwa ni mojawapo ya sheria za Mungu ambazo mwanadamu anapaswa kuzitii. Asiye kubali kubatizwa hataingia katika ufalme wa Mungu. “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa” Marko 16:16. Kubatizwa katika maji mengi.    Hii ni sheria ya Mungu  yakuzingatia kama vile Yesu Kristo alivyo batizwa katika maji mengi. “Naye Yesu alipokwisha ba...

VIFO VYA MITUME WA YESU.

Mathayo - Alikufa kwa kuuwawa kwa upanga mbali kidogo na mji wa Ethopia. Marko    -   Alikufa kule Alexandria baada ya kukokotwa kikatili kwenye barabara ya mji. Luka   -   Alitundikwa juu ya mti wa mizeituni katika nchi ya Kigiriki ya kimaendeleo. Yohana   -   Alitiwa kwenye pipa la mafuta yanayochemka lakini hakufa kwa njia ya miujiza na baadaye akapelekwa kwenye    Kisiwa cha Patimo ili afe hata hivyo hakufa huko. Alikufa huko Efeso miaka 100 BK. Petro   –   Alisulubiwa kule Rumi kichwa chini miguu juu mwaka 67 BK. Yakobo Zebedayo   –   Alikatwa kichwa kule Yerusalemu mwaka 44 BK,   Mdo 12:1-2. Yakobo wa Alifayo   –   Alitupwa kutoka kwenywe kinara na kisha kupigwa na rungu lenye  misumari mpaka kufa, mwaka 62 BK. Batholomayo   –   Alichunwa ngozi akiwa hai mpaka akafa. Andrea   –   Alifungwa kwenye msalaba huku akiendelea kuwahubiria w...