Maana ya neno ubatizo.
Neno ubatizo linatokana na neno la Kiyunani baptizo. Maana ya neno baptizo ni kuzamisha.
Kubatizwa ni agizo la Mungu.
Mungu alimtuma Yohana aje duniani kuhubiria watu watubu dhambi zao na kuwabatiza. “Tubuni, kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia” Mathayo 3:2. “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordan; Naye akawabatiza katika mto Yordani, huku wakiziungama dhambi zao” Mathayo 3:5,6.
Asiyeye kubali kabatizwa atahukumiwa.
Kubatizwa ni mojawapo ya sheria za Mungu ambazo mwanadamu anapaswa kuzitii. Asiye kubali kubatizwa hataingia katika ufalme wa Mungu. “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa” Marko 16:16.
Kubatizwa katika maji mengi.
Hii ni sheria ya Mungu yakuzingatia kama vile Yesu Kristo alivyo batizwa katika maji mengi. “Naye Yesu alipokwisha batizwa mara akapanda kutoka majini” .…Mathayo 3:16. Yesu alisisitiza ni lazima Mtu azaliwe kwa maji. Ukweli ili Mtu azaliwe kwa maji ni lazima azamishwe ndani ya maji, anapopanda kutoka majini anakuwa amezaliwa kwa maji. “Yesu akajibu amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji….. hawezi kuingia ufalme wa Mungu” Yohana 3:5. “Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu huko kulikuwa na maji tele; na watu wakamwendea, wakabatizwa” Yohana 3:23.
Sababu ya kubatizwa:
1. Ni kutimiza haki au sheria ya Mungu, ndio maana Yesu alimwendea Yohana ili abatizwe. “Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe. Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, mimi nahitaji kubatizwa na wewe,nawe waja kwangu? Yesu akajibu akamwambia, kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo (sisi) kuitimiza haki yote. Basi akamkubali” Mathayo 3:13 -15.
2. Ni ishara ya kuzikwa pamoja na Kristo katika mauti yake. “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?. Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake”…..Warumi 6:3,4.
Neno ubatizo linatokana na neno la Kiyunani baptizo. Maana ya neno baptizo ni kuzamisha.
Kubatizwa ni agizo la Mungu.
Mungu alimtuma Yohana aje duniani kuhubiria watu watubu dhambi zao na kuwabatiza. “Tubuni, kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia” Mathayo 3:2. “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordan; Naye akawabatiza katika mto Yordani, huku wakiziungama dhambi zao” Mathayo 3:5,6.
Asiyeye kubali kabatizwa atahukumiwa.
Kubatizwa ni mojawapo ya sheria za Mungu ambazo mwanadamu anapaswa kuzitii. Asiye kubali kubatizwa hataingia katika ufalme wa Mungu. “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa” Marko 16:16.
Kubatizwa katika maji mengi.
Hii ni sheria ya Mungu yakuzingatia kama vile Yesu Kristo alivyo batizwa katika maji mengi. “Naye Yesu alipokwisha batizwa mara akapanda kutoka majini” .…Mathayo 3:16. Yesu alisisitiza ni lazima Mtu azaliwe kwa maji. Ukweli ili Mtu azaliwe kwa maji ni lazima azamishwe ndani ya maji, anapopanda kutoka majini anakuwa amezaliwa kwa maji. “Yesu akajibu amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji….. hawezi kuingia ufalme wa Mungu” Yohana 3:5. “Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni, karibu na Salimu, kwa sababu huko kulikuwa na maji tele; na watu wakamwendea, wakabatizwa” Yohana 3:23.
Sababu ya kubatizwa:
1. Ni kutimiza haki au sheria ya Mungu, ndio maana Yesu alimwendea Yohana ili abatizwe. “Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe. Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, mimi nahitaji kubatizwa na wewe,nawe waja kwangu? Yesu akajibu akamwambia, kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo (sisi) kuitimiza haki yote. Basi akamkubali” Mathayo 3:13 -15.
2. Ni ishara ya kuzikwa pamoja na Kristo katika mauti yake. “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?. Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake”…..Warumi 6:3,4.
Ubatizo wa toba.
Wakati Yohana akibatiza watu walipomwendea waliziungama dhambi zao na kubatizwa, ndio maana ukaitwa ubatizo wa toba kwa sabhabu mambo haya mawili yalifanyika kwa wakati mmoja ijapokuwa kila moja linajitegemea na lina maana yake. Kubatizwa hakuondoi dhambi bali ni kuitimiza haki au sheria ya Mungu. Toba ni neno linalomaanisha kuungama dhambi mbele za Mungu. Dhambi huondolewa na Mungu mtu anapoungama. “Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” 1Yohana 1:9
Ni nani anayebatizwa?
Ni Mtu mzima kwa sababu anaweza kufahamu neno la Mungu na kuliamini ndio maana imeandikwa “aaminiye” pia anaweza kuwa na “dhamiri safi” neno dhamiri limaanisha nia “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa” Marko 16:16. “Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo” 1Petro 3:21.
Watoto wadogo hawabatizwi.
Kwa sababu bado ni wadogo hawawezi kuamini, hawajafikia kuwa watu wazima. Katika sheria ya Mungu kwenye Biblia hakuna mahali popote imeandikwa watoto walibatizwa, bali walibarikiwa. “Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea. Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao. Amini, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama watoto wadogo hataingia kabisa. Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia” Marko 10:13-16.
Usipunguze wala kuongeza kuhusu ubatizo.
Kwa sababu Mungu ameagiza kubatizwa kwa maji mengi yatupasa kufanya hivyo na sii vinginevyo. Yatupasa kumtii Mungu kwa sheria zake zote bila kuzipindisha au kwenda kinyume nazo. Kwa mfano wewe una mtoto wako umempa agizo aoge lakini yeye kwa utashi wake akaamua kunawa miguu je, ametimiza agizo lako? endelea kufikiri je, utafurahi kwa kitendo chake kwa kufanya kinyume na agizo lako?
Anayeongeza au kupunguza maagizo au maneno ya Mungu hataingia kwenye uzima wa milele mbinguni. “Na mtu akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki”. Ufunuo 22:19. “Msiliongeze neno niwaamurulo wala msilipunguza, mpate kuzishika amri za Bwana, Mungu wenu, niwaamuruzo” Kumbukumbu 4:2.
Wakati Yohana akibatiza watu walipomwendea waliziungama dhambi zao na kubatizwa, ndio maana ukaitwa ubatizo wa toba kwa sabhabu mambo haya mawili yalifanyika kwa wakati mmoja ijapokuwa kila moja linajitegemea na lina maana yake. Kubatizwa hakuondoi dhambi bali ni kuitimiza haki au sheria ya Mungu. Toba ni neno linalomaanisha kuungama dhambi mbele za Mungu. Dhambi huondolewa na Mungu mtu anapoungama. “Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” 1Yohana 1:9
Ni nani anayebatizwa?
Ni Mtu mzima kwa sababu anaweza kufahamu neno la Mungu na kuliamini ndio maana imeandikwa “aaminiye” pia anaweza kuwa na “dhamiri safi” neno dhamiri limaanisha nia “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa” Marko 16:16. “Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo” 1Petro 3:21.
Watoto wadogo hawabatizwi.
Kwa sababu bado ni wadogo hawawezi kuamini, hawajafikia kuwa watu wazima. Katika sheria ya Mungu kwenye Biblia hakuna mahali popote imeandikwa watoto walibatizwa, bali walibarikiwa. “Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea. Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao. Amini, nawaambieni, Ye yote asiyeukubali ufalme wa Mungu kama watoto wadogo hataingia kabisa. Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabarikia” Marko 10:13-16.
Usipunguze wala kuongeza kuhusu ubatizo.
Kwa sababu Mungu ameagiza kubatizwa kwa maji mengi yatupasa kufanya hivyo na sii vinginevyo. Yatupasa kumtii Mungu kwa sheria zake zote bila kuzipindisha au kwenda kinyume nazo. Kwa mfano wewe una mtoto wako umempa agizo aoge lakini yeye kwa utashi wake akaamua kunawa miguu je, ametimiza agizo lako? endelea kufikiri je, utafurahi kwa kitendo chake kwa kufanya kinyume na agizo lako?
Anayeongeza au kupunguza maagizo au maneno ya Mungu hataingia kwenye uzima wa milele mbinguni. “Na mtu akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki”. Ufunuo 22:19. “Msiliongeze neno niwaamurulo wala msilipunguza, mpate kuzishika amri za Bwana, Mungu wenu, niwaamuruzo” Kumbukumbu 4:2.
Maoni
Chapisha Maoni