Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAOMBI - 1.

Neno MAOMBI linamaanisha kupeleka  hitaji/mahitaji  mbele za Mungu kwa ajili ya kupatiwa msaada.  Unapomwomba Mungu kitu chochote ni muhimu ujue anakusikia. Ni sawa na mtoto anapomwomba baba yake kalamu au daftari anamsikia na kumpa.Unapomuomba Mungu unaongea na Baba yako wa mbinguni naye anakusikia kama baba wa dunia hii anavyomsikiliza mtoto wake. Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe? Au akiomba samaki, atampa nyoka? Basi ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! si zaidi sana Baba yenu aliye  mbinguni atawapa mema (mahitaji) wao wamwombao”?  Mathayo 7:9-11.

Jinsi ya kuomba
1. Kuomba kwa imani.
Ili uombe kwa imani ni lazima uwe na imani, na imani inapatikana katika neno la Mungu. “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja neno la Kristo” Warumi 10:17.  Unapomwomba Mungu ni lazima uamini kile kitu ambacho umemwomba amekupa, bila ya kuwa na shaka yoyote nawe utapokea. “Amin, nawaambia, ye yote atakayeuambia mlima huu, ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Kwa sababu hiyo nawaambia, yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapoke, nayo yatakuwa yenu” Marko 11:23, 24.

“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana (wazi) ya mambo yasiyoonekana.  Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao”  Waebrania 11:1,6. “Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba” 1Yohana 4:15.

 2. Kuomba katika utakatifu
Ili uombe katika utakatifu yakupasa kuishi maisha ya utakatifu, haya ni maisha ya haki.  “Bwana yu mbali na wasio haki; Bali huisikia sala ya mweye haki” Mithali 15:29. “Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi; bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake, humsikia huyo” Yohana 9:31. “Wapenzi mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu; na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake,na kuyatenda yapendezayo machoni pake” 1Yohana 3:21,22.

3. Kuomba katika Roho Mtakatifu 
Mtu ili aombe katika Roho Mtakatifu ni muhimu awe amejazwa Roho Mtakatifu kama wale Mitume wa Yesu. “Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka” Matendo 1:4. Bali, ninyi wapenzi, mkijijenga juu ya imani… takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu” Yuda 1:20.

 “Kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho”...Waefeso 6:18. Yesu Kristo alishukuru katika Roho Mtakatifu, “Saa ile ile alishangilia kwa Roho Mtakatifu, akasema,Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo  ilivyokupendeza” Luka 10:21.    


4. Kuomba katika mapenzi ya Mungu
Ni kuomba sawa sawa na neno au maagizo ya Mungu na wala si vinginevyo. Kwa mfano huwezi kumuomba Mungu akusaidie na kukufanikisha kufanya uovu wowote kama ujambazi, namna hii ni kuomba vibaya, Mungu hasikii maombi kama haya. Ni muhimu uyafahamu maandiko  yote ya neno la Mungu usije ukaomba vibaya.  “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawa sawa na mapenzi yake, atusikia” 1Yohana 5:14. “Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tama zenu” Yakobo 4:3.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...