Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAADILI YA NENO LA MUNGU.

Mungu alituumba kwa kusudi la kuishi katika maadili ya neno lake, ndio maana imeandikwa, “Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo” Waefeso 2:10. 

Mavazi ya mwanamke
Neno lake Mungu linatufundisha maadili ya mavazi ya kuvaa kwa mwanamke.   Vivyo hivyo wanawake wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri…" 1Timotheo 2:9. Ikiwa mwanamke amevaa gauni fupi, linalobana au lililopasuli na kuonyesha sehemu zake za mwili ambazo hazipaswi kuonekana wazi  anajiabisha na kujivunjia heshima mbele za Mungu na jamii. Kujichubua uso ni kuondoa rangi ya asili aliyoumbwa nayo. Kunyoa nyusi na kupaka  rangi badala ya nyusi na kuvaa nywele badia, haya si maadili ya neno la Mungu.    

Mwanamke afanyaye  mambo kama haya hapa juu anampinga  na kumkosoa muumbaji wake ambaye ni Mungu.  Ni sawa na kumwambia alikosea alivyomuumba. Si vema kumkosoa Muumbaji wake kwa matendo hayo. Yeye ni mkuu, hakosei ni mwenye haki wakati wote.“Ole wake ashindanaye na Muumba wake! Kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je! Udongo umwambie yeye afinyangaye; Unafanya nini? Au kazi yako, Hana mikono? Mimi nimeumba dunia, nimemhuluku mwanadamu juu yake; Mimi, naam, mikono yangu mimi, imezitandaza mbingu, na jeshi lake lote nimeliamuru” ISaya 45:9,12. Hatuwezi kumfundisha wala kuhoji uumbaji wake kwa sababu imeandikwa, “Mungu akaona kila kitu alichokifanya na tazama ni chema sana…” Mwanzo 1:31.

Kuvaa mavazi ya namna hiyo ni kuharibu watoto ambao ni taifa la wakati ujao. Watoto hujifunza kwetu kwa yale wanayoyaona tunafanya yawe ni mabaya au ni mema. Kwa hiyo wazazi wanapaswa kuvaa mavazi ya heshima na kusitiri mwili ili kuficha maeneo yote ya mwili yasiyopaswa kuonekana. Kwa mfano huwezi kusema Mungu anaangali mambo ya rohoni na kwamba haangalii mambo ya mavazi. Si vyema kusema hivyo kwa kuwa Yesu aliwafundisha waandishi na Mafarisayo, wanapaswa kusafisha kikombe ndani na nje ili kiwe safi.

Katika maneno hayo Yesu alimaanisha ya kwamba haiwezekani kuwa safi kwa nje na ndani ni kuchafu, bali nje na ndani kunapaswa kuwa safi. “Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mwasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi. Ewe Farisayo kipofu, safisha kwanza ndani ya kikobe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi” Mathayo 23:25,26.    
  
Mavazi ya mwanamume
Pia mwanamume anapaswa kuvaa mavazi ya heshima na kusitiri mwili , haya ndio maadili ya neno la Mungu. Hapaswi kuiga namna ya dunia hii na kuvaa mavazi kwa namna isivyo sahihi, kama kufungia suruali katikati ya makalio (mlegezo) na kuacha kifua wazi, mambo haya  hayapendezi mbele za Mungu. “Basi ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza  Mungu; ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mngeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kupendeza, na ukamilivu” Warumi 12:1,2.       

Kuimba mbele za Mungu.
Tunapokuwa tunafanya ibada mbele za Mungu  iwe ni kusifu, kuabudu, kuimba na kucheza inatupasa kujua tuko mbele ya Mungu mkuu anayestahili kuhofiwa na kuheshiwa na wanadamu wote. “Nchi yote na imwogope Bwana,Wote wakaao duniani na wamche” (kumhofu) Zaburi 33:8.  Mungu hafanyiwi dhihaka ya kuchezewa sawa na mtoto anavyoweza kuchezea mwana sesere kama apendavyo. Vile vile hatuwezi kumfurahisha Mungu wetu kwa kuimba na kucheza kwa namna ya dunia hii.  

Hayo hayampendezi Mungu na kwa neno lake anasema hivi, “Niondoleeni kelele za nyimbo zenu; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu. Lakini hukumu na itelemke kama maji, na haki kama maji makuu” Amosi 5:23,24.   Ni vema wewe uliyekwisha kumjua Mungu yakupasa kufanya ibada ya kumpendeza mbele zake. Ametupa maadili ya neno lake  kuhusu jinsi ya kufanya ibada ya kupendeza kwa kuimba na kucheza kwa namna nzuri. Imeandikwa, “Mwabuduni Bwana kwa uzuri na utakatifu, Tetemekeni mbele zake, nchi yote” Zaburi 96:9.   

Kwa mfano, kufanya mikutano ya injili kwa kuimba na kucheza kwa mapigo na sauti ya miziki ya namna ya dunia ili watu wasioamini wavutiwe na kuokoka. Kwa kufanya hivyo si sahihi ni kulitukanisha jina la Bwana kana kwamba hana nguvu na uwezo wa kuokoa watu wake, hili nalo ni dhambi,  kama hutatubu na kuacha kufanya hivyo utahukumiwa. “Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi” Yakobo 4:17. Mungu ndiye anayeokoa watu kwa neno lake si mwanadamu kwa kuwavuta kwa kuimba na kucheza miziki ya kidunia. Yesu alisema;  
Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho. Yohana 6:44

Kuimba na kucheza
Kuimba na kucheza inakubalika mbele za Mungu kwa kutumia vyombo. “Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinada na kinubi; Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana. Kila mwenye punzi na amsifu Bwana. Haleluya” Zaburi 150:3-6.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...