Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUEPUKA DHAMBI

Kutokusamehe wengine
Kitendo cha kutosamehe  wanaokukosea ni dhambi kama dhambi zingine . Kusamehe ni agizo la Mungu na ni wajibu wako. “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi. Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe makosa yenu”  Mathayo 6:14,15. Unapokosewa usingoje kuombwa msamaha unapaswa kumsamehe aliyekukosea kwa wakati huo huo.  

Unapomsamehe aliyekukosea unakuwa na amani na utulivu ndani ya moyo wako na ndio maana imeandikwa, “ Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo;-------” Mithali 4:23.Unapolinda moyo wako unakuwa salama. Ili kuendelea kuwa salama yakupasa uepuke ugomvi, mabishano na maneno yasiyofaa,   
hayo hayana maana huleta uharibifu katika moyo wako.  

Maneno yasiyo maana
Kwa maadili ya Mungu ametuumba kwa ajili ya mema katika kutenda na kusema.
Anataka tumpendeze yeye katika mambo yote, na ndipo tutaurithi ufalme wa Mungu.  
Maneno yasiyo maana ni kama, kutaniana, kudhihaki, matusi, ugomvi, mabishano na yanayofanana  na hayo. “Msidanganyike mazungumzo mabaya huharibu tabia njema” 1Wakorintho 15:33. “Basi, nawaambia, kila neno lisilo maana,watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu. Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa” Mathayo 12:36,37.

Kujisifu
Mungu ametuonya na kutufundisha tusijisifu kwa  mambo yoyote kwa kuwa hapendezwi na hayo. “Bwana asema hivi, mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake,wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake; bali ajisifuye ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi,na kunijua, ya kuwa mimi ni Bwana, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema Bwana” Yeremia 9:23,24.

 “Haya basi, ninyi msemao, leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; walakini hujui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha kutoweka. Badala ya kusema Bwana akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi. Lakini sasa mwajivuna katika majivuno yenu, kujisifu kote kwa namna hii ni kubaya” Yakobo 4:13-16. “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mweziwe kuwa bora kuliko nafsi yake” Wafilipi 2:3.

 Kiburi
Wenye kiburi watahukumiwa, ni vizuri kujichunguza katika maisha yako usije ukahukumiwa. “Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu. Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho ya kutakabari hutangulia maanguko” Mithali 16:5,18.

Hasira
Sii vyema kukasirika kwa kuwa utatenda isivyo haki, ili kujilinda na kuwa salama wakati wowote, unapokosewa samehe, nawe utakuwa na amani na utulivu. Katika maisha yako kamwe usiruhusu kukasirika kwa sababu kutakusababishia uchungu na kufadhaika moyoni mwako. Unapokosewa ni vema kutawala moyo wako usiwe na haraka ya kusema, imeandikwa hivi, “Azuiaye maneno yake ni mwenye maarifa; Na mwenye roho ya utulivu ana busara” Mithali 17:27. “Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji” Mithali 16:32. 

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...