Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAOMBI - 2.

Mwendelezo wa somo la maombi lililotangulia. Karibu endelea kujifunza.

5. Kuomba kwa bidii bila kukata tamaa.
Maombi ya namna hii ni dua, unamwomba Mungu tena na tena hadi anakupa unachokihitaji. Ukisoma habari za Watumishi wa Mungu walifanya maombi ya dua na kupokea waliyoyahitaji. Na si hivyo tu, Bwana wetu Yesu Kristo alifanya dua na kutufundisha kuomba kwa bidii na kupokea. “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi,akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu” Waebrania 5:7.

“Akawaambia mfano, imewapasa kumwomba Mungu siku zote, wala wasikate tamaa, Akasema, Palikuwa na kadhi katika mji fulani, hamchi Mungu, wala hajali watu. Na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane, aliyekuwa akimwendea-endea, akisema, nipatie haki na adui wangu. Naye kwa muda alikataa; halafu akasema moyoni mwake, Ijapokuwa simchi Mungu na kujali watu, lakini, kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitampatia haki yake, asije akanichosha kwa kunijia daima. Bwana akasema, sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu. Na Mungu je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao? Nawaambia atawapatia haki upesi…" Luka 18:1-8.

"… Naye Eliya akapanda juu mpaka kilima cha Karmeli; akasujudu kifudifudi, akainama uso mpaka magotini. Akamwambia mtumishi wake, kwea sasa, utazame upande wa baharini. Akakwea, akatazama, na kusema, Hakuna kitu. Naye akasema, enenda tena mara saba. Ikawa mara ya saba akasema, Tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. Akanena, Enenda, umwambie Ahabu, Tandika ushuke mvua isikuzuie. Ikawa muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikanya mvua nyingi…" 1Wafalme 18:42- 45.  Haya maaandiko yanaonyesha jnsi Eliya alivyomwomba Mungu mara sita mvua haikunyesha, lakini hakukata tamaa  aliomba tena kwa mara ya saba na mvua ikanyesha. Hakika Mungu anajibu maombi ukiomba kwa bidii.

6. Jinsi ya kuomba 
 1) Kuomba kwa jina la Yesu.
“Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya” Yohana 14:13, 14.

2)
 Kwa mfano maombi ya ulinzi. Ee Mungu Baba kwa jina la Yesu, ninakuomba unilinde salama, na kuniepusha na hatari zote. Ninakushukru kwa kuwa umenisikia ni katika jina la Yesu. Amen.

7.Kuomba na kushukuru.
ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu” 1Wathesalonike 5:17,18. “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba pamoja na kushuru, haja zote na zijulikane na Mungu” Wafilipi 4:6.  

8. Kabla ya kumwomba Mungu hujibu.
Ahadi hii inawezekana kwa wale waliomwamini Mungu na kupokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wao.“Naitakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu;  na wakiwa katika kunena nitasikia” Isaya 64:24. “...maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi  hamjamwomba” Mathayot 6:8. “Umtumaini Bwana ukatende mema,...Nawe utajifurahisha kwa Bwana, Naye atakupa haja ya moyo wako”. Wakati mwingine hata kabla ya kuomba unapewa haja ya moyo wako, lakini kwa kutimiza agizo la kumtumaini (kumtegemea) na kutenda mema.

Kujibiwa kabla ya kuomba ni  kwa neema yake Mungu katika Kristo Yesu. Haimaanishi tusiombe, yatupasa kuomba ni wajibu wetu kwa kuwa yeye hujibu maombi kwa kulitukuza jina lake katika  Yesu Kristo. “Mkiomba neno lo lote kwa jina langu hilo nitalifanya ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana” Yohana 14:13. Mungu hufanya zaidi ya yale tuyaombayo na kuyawaza.“Basi atukuzwe awezaye kufanya mambo ya ajabu mno kuliko yote tuyaombayo au tuyawazayo, kwa kadri ya nguvu itendayo kazi ndani yetu” Waefeso 3:20.

Sababu za kuomba.  
)     Kuomba tusiingie majaribuni Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi lakini mwili ni dhaifu” Mathayo 26:41.
)      Kuomba kwa  ajili mahitaji yetu mbele za Mungu. 

Wakati wa kuomba
Kila wakati. “Kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu kuwaombea watakatifu wote” Waefeso 6:18. “Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani” Wakolosai 4:2.

Mahali pa kufanyia maombi
1. Hekaluni (Kanisani). “Basi Petro na Yohana walikuwa wakikwea pamoja kwenda hekaluni saa ya kusali, saa tisa” Matendo 3:1.

2. Chumbani. “Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha funga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi” Mathayo 6:6.  
3.Mahali panapofaa.
Yesu alikwenda katika mlima Mizeituni na wanafunzi wake kuomba. “Akatoka akaenda mlima Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; wanafunzi wake wakafuatana naye. Alipofika mahali pale aliwaambia ombeni… Mwenyewe akajitenga nao…akapiga magoti akaomba” Luka 22:39- 41. Paulo na sila walikuwa wanatafuta mahali pa faragha wakasema hivi “… tukaenda kando ya mto, Ambapo tukadhani yakuwa pana mahali pa kusali…" Matendo 16:13.

Sababu maombi kutojibiwa
1. Kuishi maisha ya dhambi.
“Twajua ya kuwa Mungu hawasikii wenye dhambi…” Yohana 9:31.
“Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka hata asiweze kuokoa; wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; lakini maovu yenu yamewafarakanisha ninyi na Mungu wenu,na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia” Isaya 59:1,2.

2. Komba pasipo na imani

Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; naye akisita-sita, Roho yangu haina furaha naye “Bwana akasema, kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mgeuambia mkuyu huu, Ng’oka, nao ukapandwe baharini, nao ungewatii” Luka 17:6. “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao” Waebrania 10:38, 11:6.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...