Kitu cha kwanza mkristo aliyeokoka anapaswa kukijua ni kwamba hapa duniani kuna majaribu ya namna nyingi. Kwa sababu hiyo yule mwovu hutujaribu katika hayo. Lengo lake ni kututoa katika kusudi la Mungu ili tutende dhambi. Mtu ambaye anamcha Mungu kwa bidii ni rahisi sana kushinda majaribu yote. Tunaweza kuona katika maandiko ya kwamba Yesu Kristo ambaye ni Bwana wetu na Ayubu walijaribiwa na Shetani. Walimshinda kwa sababu walikuwa wakimcha Mungu.
Kwa hiyo ili mkristo aweze kumshinda Shetani yapo mambo muhimu ya kujifunza katika neno la Mungu. Mambo hayo ni kama ifuatavyo;
Kwa hiyo ili mkristo aweze kumshinda Shetani yapo mambo muhimu ya kujifunza katika neno la Mungu. Mambo hayo ni kama ifuatavyo;
1. Kulifahamu neno la Mungu. Ikiwa Mtu analifahamu neno la Mungu ni jambo la muhimu sana. Tunajifunza kwa Yesu alivyojaribiwa na ibilisi na kushinda ni kwa sababu alikuwa analifahamu neno la Mungu linavyosema. Kwa sababu hiyo aliweza kuzitambua hila za Shetani na kumpinga. "Ibilisi akamwambia, .... liambie jiwe hili liwe mkate. Yesu akamjibu, Imeandikwa mtu ya kwamba hataishi kwa mkate tu." Luka 4:3-4. Pia Shatani alimjaribu Ayubu akapoteza watoto, watumishi na mali zake zote. Kwa sababu alikuwa anamfahamu Mungu kwa ukamilifu hakutenda dhambi. Ndio maana imeandikwa "Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi, wala hakumwazia Mungu kwa upumbavu." Ayubu 1:22. Kuna umuhimu wa mwamini aliyeokoka ili kuyafahamu maandiko ya neno la Mungu yampasa kujifunza kwa bidii na kuyahifadhi moyoni. Ndipo anaweza kuzitambua hila za Shetani na kumpinga. Kuna umuhimu wa mwamini aliyeokoka ili kuyafahamu maandiko ya neno la Mungu yampasa kujifunza kwa bidii na kuyahifadhi moyoni. Ndipo anaweza kuzitambua hila za Shetani na kumpinga.
“Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.” Wakolosai 3:16.
2. Kudumu katika maombi. "Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; ...." Mathayo 26:41. Ikiwa mtu anamwomba Mungu kila siku ni rahisi kuzitambua hila za Shetani na kumshinda.
“Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.” Wakolosai 3:16.
2. Kudumu katika maombi. "Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; ...." Mathayo 26:41. Ikiwa mtu anamwomba Mungu kila siku ni rahisi kuzitambua hila za Shetani na kumshinda.
3. Kujilinda na kuepuka dhambi.
Ni muhimu kila mkristo aliyeokoka kuwa makini na kuyatambua mazingira yenye ushawishi wa mambo maovu na kuyaepuka. Kwa kufanya hivyo hataingia majaribuni. "....aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi." 1Yohana 5:18.
"Palikuwa na mtu....alikuwa aliitwa Ayubu....ni mmoja aliyemcha Mungu na kuepukana na maovu." Ayubu 1:1.
"Palikuwa na mtu....alikuwa aliitwa Ayubu....ni mmoja aliyemcha Mungu na kuepukana na maovu." Ayubu 1:1.
Mungu akubariki kwa somo zuri
JibuFuta