Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. " 
"Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33.

Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,  "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu" Walawi   19:2.

Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora, Hao ndio nilipendezwa nao” Zaburi 16:3. "Bwana wetu Yesu Kristo anakazia jambo hilo akisema, “ Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama baba yenu wa mbinguni alivyo mtakatifu” Mathayo 5:48 

Mambo ya kuzingatia.
1 Kujifunza neno. “Tena mtaifahamu kweli (Neno) nayo hiyo kweli itawaweka huru. Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli” Yohana 8:32 . Hiyo kweli inakuweka mbali na dhambi, hutasikia huru ndani yako. “Wapenzi mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu” 1Yohana 3:21.       

2.  Kuamini neno linavyosema.
“Basi ikiwa ikalika ahadi ya kuingia katika raha yake  (mbingini), na tuogope, mmoja wenu asije akaonekana ameikosa. Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia. Maana sisi tulioamini tunaingia katika raha yake, kama vile alivyosema”. Ebrania 4:1-3.  

3 .
Kutenda neno kama linavyosema. “Yesu akajibu, akawaambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. Mtu asiyenipenda, hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalosikia silo langu, ila ni la Baba aliyenipeleka" Yohana 14:23-24. Hapa chini kuna andiko lifuatalo ambalo si kwamba linamhusu kijana tu, bali linamhusu kila mtu aliyeokoka yampasa kuwa safi na kulitii neno la Mungu. Andiko linasema “Jinsi gani kijana aisafish njia yake Kwa kutii akilifuata neno lako .       
4. Kuweka neno la Mungu moyoni.  Kuweka neno la Mungu moyoni litakuongoza na wewe utaepuka maovu. “Moyoni mwangu nimeweka neno lako, nisije nikakutenda dhambi”. Zaburi 119:11. Kwa kuwa neno linamwongoza mtu linamsababisha alitii na kuishi maisha safi ndio mana Yesu aliwaambia wanafunzi wake “Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia”. Yohana 15:3 
  
5.  Kuomba kila siku.  Tunapoomba Mungu anatupa uwezo wa kushinda majaribu yote. Ndio maana imeandikwa, "Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu"  Wafilipi 4:23. Kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni, roho i radhi lakini mwili ni dhaifu” Mathayo 26:41 .   

Endelea na somo linalohusu, Maisha kamili ya mkristo aliyeokoka. Bofya hapa na utasoma Sehemu ya kwanza na ya pili. 

Maoni

  1. Ninabarikiwa na Neno hili,nataman kujua principle yakuomba kila sku ndio kukesha???maana imeunganshwa point na andiko hilo

    JibuFuta
  2. Nmebarikiwa sana na neno hili, Mungu na anisaidie niishi maisha ya utakatifu.
    Be blessed

    JibuFuta
  3. Nimejifunza niliyokua siyatambui MUNGU akubariki

    JibuFuta
  4. Nimebarikiwa sana endelea kututumia masomo namnahii Mungu akubariki

    JibuFuta
  5. Ameeen 🙏🙏🙏 mtumishi MUNGU AZIDI KUKUBARIKI

    JibuFuta
  6. Somo Zuri Sana Mtumishi Ubarikiwe

    JibuFuta
  7. Ubarikiwe sana kwa Shule hii
    Nmejifunza

    JibuFuta
  8. AMEN!! MUNGU akubariki kwa baraka zote

    JibuFuta
  9. Bila jina23:16

    Ubarikiwe sana mtumishi
    Usichoke kusema kweli

    JibuFuta
  10. Bila jina14:06

    Nmebarikiwa sana na neno hili mungu akubariki na akuweke uzidi kunifunza zaidi Be blessed

    JibuFuta
  11. Bila jina00:35

    Ameen

    JibuFuta
  12. Novatus12:19

    Ubarikiwe mtu wa Mungu, kwa somo zuri.
    Ni kweli kabisa Yesu atakapokuja mara ya pili, atakuja kuwachukua watakatifu waliozifua nguo zao ktk damu ya mwanakondoo.

    JibuFuta
  13. Bila jina15:24

    Ubarikiwe sana mtumishi wa Mungu Kwa somo hili kweli nimejua Jinsi ya kuishi MAISHA ya utakatifu Be blessed man of God 🙏🙏🙌🙌

    JibuFuta
  14. Bila jina23:58

    Nimebarikiwa na ujumbe be blessed

    JibuFuta
  15. Bila jina14:31

    Hakika tutaishi katika IMANI ya kweli kama baba asemavyo be blessed

    JibuFuta
  16. Bila jina17:11

    Mungu akubariki Sana nimejifunza jinsi yakuishi maisha ya utakatifu

    JibuFuta
  17. Bila jina20:30

    Hakika nimasomo yenye faraja kubwa mno bwana awabariki sana

    JibuFuta
  18. Bila jina18:01

    Mungu akubariki sana mtumishi wa Mungu hakika nimepata kitu kupitia hili soma

    JibuFuta
  19. Bila jina22:12

    Mi nimebarikiwa na hilo somo haswaa!!

    JibuFuta
  20. Bila jina22:15

    Mungu awaweke pahali patakatifu kwa mafundisho mnayoyafundisha

    JibuFuta
  21. Bila jina22:30

    Nashkuru sana kwa hii funzo nitafunza wengine

    JibuFuta
  22. Bila jina15:38

    Nimejifunza kuwa unatakiwa kukaa karibu na neno la mungu Yan bibilia Kila saa ili uweze kujifunza zaidi na kuelewa Mungu anataka Nini kwangu,pia kuelewa na neno jinsi ukiomba unatakiwa kuamini

    JibuFuta
  23. Bila jina13:42

    BLESSED

    JibuFuta
  24. Bila jina16:24

    Atukuzwe MUNGU kwaajili yako

    JibuFuta
  25. Bila jina12:55

    Ameen barikiwa sana mtumishi

    JibuFuta
  26. Bila jina12:28

    Ubarikiwe mtumishi

    JibuFuta
  27. Bila jina16:40

    Asante Sana kwa habari hii njema

    JibuFuta
  28. Bila jina00:18

    Somo zuri sana, naweza kulipata kwa njia ya WhatsApp

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...

UPONYAJI WA MAGONJWA.

Chanzo cha magonjwa. Kuna magonjwa yanayotokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya yule mtu ambaye aliyekuwa mngonjwa akamwabia,   “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi”   Yn 5:14.   Ikiwa mtu aliyeokoka akirudia kuishi maisha ya dhambi pepo mchafu anapoona nafasi anachukua pepo wengine na kuingia kwake. Yesu alisema,  “Mara huenda akachukua pamoja naye    pepo    wengine walio waovu    kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”   Mt 12:45.    Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili. Kwa upande mwingine mtu anaweza akawa ni mgonjwa au amekosa lishe.  Uponyaji wa Mungu.                     Mambo ya kuzingatia na kuponywa ni ha...

KUWEKWA HURU KUTOKA DHAMBI YA UZINZI NA UASHARATI.

Jambo la kwanza ninamshukuru Mungu kwa neema yake aliyonipa kufundisha neno lake. Ndungu mpendwa ninajua ya kwamba Mungu alikupenda sana, hata akamtoa Mwana wake wa pekee Yesu Kristo kwa ajili yako ili akukomboe kutoka katika dhambi zote ikiwemo dhambi ya uzinzi na uasherati. Sasa ninakusihi kwa neema ya Mungu fuatana nami kwa makini kuhusu  somo hili nawe utauna utukufu wa Mungu katika maisha yako. Tunaweza kuangalia kwa makini dhambi ya uzinzi na uasharati ambayo mtu akiitenda inaharibu ufahamu wake na hatimaye kuangamia. Mtu anapoteza uhusiano wake na Mungu, mawasiliano kati yake na Mungu yanakatika. Mungu  ni Makatifu hana ushirika na wenye dhambi. “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.” Mithali 6:26.   “Lakini maovu yenu yamewafarikisha (yamewatenganisha) ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki  kusikia.”   Isahau 59:2. Atendaye dhambi ya zinaa au  uasherati ...

KUDUMU KATIKA UPENDO WA MUNGU.

Neno la Mungu katika Biblia linatufudisha kuhusu upendo wa Mungu  kwetu. Yeye Mungu ndiye  mwanzo wa upendo kwa sababu alitupenda kwanza. “...alitupenda sisi kwanza”.   1 Yohana 4:19. Jinsi mtu anavyoweza kuwa na upendo wa Mungu. Ni pale mtu anapokuwa amezingatia kudumu katika upendo wa Mungu kama ifuatavyo; 1.Kuishi sawasawa na maagizo yote ya neno la Mungu na kumpenda. “Na sasa, Israeli, BWANA, Mungu wako, anataka nini kwako, ila umche BWANA, Mungu wako, na kwenda katika njia zake zote, na kumpenda, na kumtumikia BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote;”   Kumbukumbu la Torati 10:12.   “Lakini mjibidiishe sana kuzifanya amri na sheria, ambazo Musa, mtumishi wa BWANA, aliwaamuru, kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kwenenda katika njia zake zote, na kuzishika amri zake, na kushikamana na yeye, na kumtumikia kwa moyo wenu wote na nafsi yenu yote”.   Yoshua 22:5. 2. Jambo lingine la kuzingatia ni kwamba yampasa mtu kuyashika maagiz...

MADHARA YA DHAMBI.

Huu ni wakati mwingine ambao Bwana amenijalia kuwepo kwa kusudi lake jema. Nitaelezea katika somo hili kuhusu dhambi ilivyo na madhara kwa mtu aitendaye. Kwanza tuangalie dhambi  ilivyoanza kwa Adamu na Hawa ni wakati walipokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambayo Mungu aliwakataza wasile. Kwa sababu hiyo dhambi ilisababisha madhara mengi kwa uzao wake na vizazi vyote duniani. Kwa hiyo shida zote zilizopo duniani zimetokana na dhambi. Kutokana na wazazi wetu wa kwanza Adamu na Hawa kwa kuwa walitenda dhambi na vizazi vingine vyote vimehesabiwa ni wenye dhambi. Mtu  anazaliwa akiwa na asili ya dhambi kutoka kwa wazazi wa kwanza Adamu na Hawa. Warumi 3:23 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;” Kutokana na sababu hiyo ndio maana kila mwanadamu anakufa sawasawa na Mungu  alivyosema katika kitabu cha Mwanzo 2:16-17 “BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa u...