Utakatifu - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi
kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu
kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo
linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani
yake kwa ajili ya kufanya uamuzi. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha
alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi kwa hiari maisha ya
kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. “
"Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au
ufanyeni mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda
yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33.
Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote
aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa, "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa
watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu" Walawi 19:2.
Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema; “Watakatifu waliopo duniani ndio walio
bora, Hao ndio niliopendezwa nao” Zaburi 16:3.
"Bwana wetu Yesu
Kristo anakazia jambo hilo akisema, “ Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama
baba yenu wa mbinguni alivyo mtakatifu” Mathayo 5:48.
Mambo ya kuzingatia.
1. Kujifunza neno. “ Tena mtaifahamu kweli (Neno) nayo hiyo kweli itawaweka huru. Basi Mwana
akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli” Yohana 8:32. Hiyo kweli
inakuweka huru mbali na dhambi, hutasikia hukumu ndani yako. “Wapenzi mioyo
yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu” 1Yohana 3:21.
2. Kuamini neno linavyosema.“Basi ikiwa ikaliko ahadi ya kuingia katika raha yake (mbingini), na tuogope, mmoja wenu asije akaonekana ameikosa. Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia. Maana sisi tulioamini tunaingia katika raha yake, kama vile alivyosema”. Ebrania 4:1-3.
3. Kutenda neno kama linavyosema. “Yesu akajibu, akawaambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. Mtu asiyenipenda, hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalosikia silo langu, ila ni la Baba aliyenipeleka" Yohana 14:23-24. Hapa chini kuna andiko lifuatalo ambalo si kwamba linamhusu kijana tu, bali linamhusu kila mtu aliyeokoka yampasa kuwa safi na kulitii neno la Mungu. Andiko linasema “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii akilifuata neno lako”. Zaburi 119:9.
4. Kuliweka neno la Mungu moyoni. Kuliweka neno la Mungu moyoni litakuongoza na wewe utaepuka maovu. “Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, nisije nikakutenda dhambi”. Zaburi 119:11. Kwa kuwa neno linamwongoza mtu linamsababisha alitii na kuishi maisha safi ndio mana Yesu aliwaambia wanafunzi wake “Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia”. Yohana 15:3.
5. Kuomba kila siku. Tunapoomba Mungu anatupa uwezo wa kushinda majaribu yote. Ndio maana imeandikwa,"Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu” Wafilipi 4:23. Kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni, roho i radhi lakini mwili ni dhaifu”. Mathayo 26:41.
Ninabarikiwa na Neno hili,nataman kujua principle yakuomba kila sku ndio kukesha???maana imeunganshwa point na andiko hilo
JibuFutaNmebarikiwa sana na neno hili, Mungu na anisaidie niishi maisha ya utakatifu.
JibuFutaBe blessed
Nimejifunza niliyokua siyatambui MUNGU akubariki
JibuFutaNimebarikiwa sana endelea kututumia masomo namnahii Mungu akubariki
JibuFutaAmeeen 🙏🙏🙏 mtumishi MUNGU AZIDI KUKUBARIKI
JibuFutaSomo Zuri Sana Mtumishi Ubarikiwe
JibuFutaUbarikiwe sana kwa Shule hii
JibuFutaNmejifunza
AMEN!! MUNGU akubariki kwa baraka zote
JibuFutaUbarikiwe sana mtumishi
JibuFutaUsichoke kusema kweli
Nmebarikiwa sana na neno hili mungu akubariki na akuweke uzidi kunifunza zaidi Be blessed
JibuFutaAmeen
JibuFutaUbarikiwe mtu wa Mungu, kwa somo zuri.
JibuFutaNi kweli kabisa Yesu atakapokuja mara ya pili, atakuja kuwachukua watakatifu waliozifua nguo zao ktk damu ya mwanakondoo.
Ubarikiwe sana mtumishi wa Mungu Kwa somo hili kweli nimejua Jinsi ya kuishi MAISHA ya utakatifu Be blessed man of God 🙏🙏🙌🙌
JibuFutaNimebarikiwa na ujumbe be blessed
JibuFutaHakika tutaishi katika IMANI ya kweli kama baba asemavyo be blessed
JibuFutaMungu akubariki Sana nimejifunza jinsi yakuishi maisha ya utakatifu
JibuFutaHakika nimasomo yenye faraja kubwa mno bwana awabariki sana
JibuFutaNimebarikiwa sana
JibuFutaMungu akubariki sana mtumishi wa Mungu hakika nimepata kitu kupitia hili soma
JibuFuta