Utakatifu - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "
"Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33.
Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa, "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu" Walawi 19:2.
Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema; “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora, Hao ndio nilipendezwa nao” Zaburi 16:3. "Bwana wetu Yesu Kristo anakazia jambo hilo akisema, “ Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama baba yenu wa mbinguni alivyo mtakatifu” Mathayo 5:48 .
Mambo ya kuzingatia.
1 . Kujifunza neno. “Tena mtaifahamu kweli (Neno) nayo hiyo kweli itawaweka huru. Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli” Yohana 8:32 . Hiyo kweli inakuweka mbali na dhambi, hutasikia huru ndani yako. “Wapenzi mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu” 1Yohana 3:21.
2. Kuamini neno linavyosema. “Basi ikiwa ikalika ahadi ya kuingia katika raha yake (mbingini), na tuogope, mmoja wenu asije akaonekana ameikosa. Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao. Lakini neno lile lililosikiwa halikuwafaa hao, kwa sababu halikuchanganyika na imani ndani yao waliosikia. Maana sisi tulioamini tunaingia katika raha yake, kama vile alivyosema”. Ebrania 4:1-3.
3 . Kutenda neno kama linavyosema. “Yesu akajibu, akawaambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake. Mtu asiyenipenda, hayashiki maneno yangu; nalo neno mnalosikia silo langu, ila ni la Baba aliyenipeleka" Yohana 14:23-24. Hapa chini kuna andiko lifuatalo ambalo si kwamba linamhusu kijana tu, bali linamhusu kila mtu aliyeokoka yampasa kuwa safi na kulitii neno la Mungu. Andiko linasema “Jinsi gani kijana aisafish njia yake Kwa kutii akilifuata neno lako ” .
4. Kuweka neno la Mungu moyoni. Kuweka neno la Mungu moyoni litakuongoza na wewe utaepuka maovu. “Moyoni mwangu nimeweka neno lako, nisije nikakutenda dhambi”. Zaburi 119:11. Kwa kuwa neno linamwongoza mtu linamsababisha alitii na kuishi maisha safi ndio mana Yesu aliwaambia wanafunzi wake “Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia”. Yohana 15:3
5. Kuomba kila siku. Tunapoomba Mungu anatupa uwezo wa kushinda majaribu yote. Ndio maana imeandikwa, "Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu" Wafilipi 4:23. Kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni, roho i radhi lakini mwili ni dhaifu” Mathayo 26:41 .
Endelea na somo linalohusu, Maisha kamili ya mkristo aliyeokoka. Bofya hapa na utasoma Sehemu ya kwanza na ya pili.
Ninabarikiwa na Neno hili,nataman kujua principle yakuomba kila sku ndio kukesha???maana imeunganshwa point na andiko hilo
JibuFutaNmebarikiwa sana na neno hili, Mungu na anisaidie niishi maisha ya utakatifu.
JibuFutaBe blessed
Nimejifunza niliyokua siyatambui MUNGU akubariki
JibuFutaNimebarikiwa sana endelea kututumia masomo namnahii Mungu akubariki
JibuFutaAmeeen 🙏🙏🙏 mtumishi MUNGU AZIDI KUKUBARIKI
JibuFutaSomo Zuri Sana Mtumishi Ubarikiwe
JibuFutaUbarikiwe sana kwa Shule hii
JibuFutaNmejifunza
AMEN!! MUNGU akubariki kwa baraka zote
JibuFutaUbarikiwe sana mtumishi
JibuFutaUsichoke kusema kweli
Nmebarikiwa sana na neno hili mungu akubariki na akuweke uzidi kunifunza zaidi Be blessed
JibuFutaAmeen
JibuFutaUbarikiwe mtu wa Mungu, kwa somo zuri.
JibuFutaNi kweli kabisa Yesu atakapokuja mara ya pili, atakuja kuwachukua watakatifu waliozifua nguo zao ktk damu ya mwanakondoo.
Ubarikiwe sana mtumishi wa Mungu Kwa somo hili kweli nimejua Jinsi ya kuishi MAISHA ya utakatifu Be blessed man of God 🙏🙏🙌🙌
JibuFutaNimebarikiwa na ujumbe be blessed
JibuFutaHakika tutaishi katika IMANI ya kweli kama baba asemavyo be blessed
JibuFutaMungu akubariki Sana nimejifunza jinsi yakuishi maisha ya utakatifu
JibuFutaHakika nimasomo yenye faraja kubwa mno bwana awabariki sana
JibuFutaNimebarikiwa sana
JibuFutaMungu akubariki sana mtumishi wa Mungu hakika nimepata kitu kupitia hili soma
JibuFutaMi nimebarikiwa na hilo somo haswaa!!
JibuFutaMungu awaweke pahali patakatifu kwa mafundisho mnayoyafundisha
JibuFutaNashkuru sana kwa hii funzo nitafunza wengine
JibuFutaNimejifunza kuwa unatakiwa kukaa karibu na neno la mungu Yan bibilia Kila saa ili uweze kujifunza zaidi na kuelewa Mungu anataka Nini kwangu,pia kuelewa na neno jinsi ukiomba unatakiwa kuamini
JibuFutaBLESSED
JibuFutaAtukuzwe MUNGU kwaajili yako
JibuFutaAmeen barikiwa sana mtumishi
JibuFutaUbarikiwe mtumishi
JibuFutaAsante Sana kwa habari hii njema
JibuFutaSomo zuri sana, naweza kulipata kwa njia ya WhatsApp
JibuFuta