Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TUNDA LA UAMINIFU.

  • Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu  wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu. “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu. Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.” Kum 7:9, 12. “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu  halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma. Isa 55:11"

  • Tabia ya mtu mwaminifu.
  • 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawasawa na maagizo, sheria na taratibu . Ikiwa ni mtu aliyeajiriwa katika kazi za nyumbani au ya serikali anafanya kazi ipasavyo, si mwizi, mpokea rushwa, mdhulumaji na wala si mwenye hila. Unaweza kuona ilivyoandikwa kuhusu mtumishi aliyeajiriwa kazi za nyumbani ambaye alipaswa kufanya kwa uaminifu. “Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake? Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.” Mt 24:45-46.

  • 2. Hatendi dhambi.Yusufu mtumishi wa Potifa kwa kuwa alikuwa mwaminifu aliposhawishiwa na mke wa Potifa ili kufanya naye dhambi ya uzinzi alikataa. “....mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia, lala nami. Lakini alikataa akamwambia....Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?” Mwa 39:7-9.

  • 3.  Hachukui kitu cha mtu mwingine, iwe ni fedha, mali, au kitu kingine chochote ambacho   si halali yake. Akitoa fedha kwa ajili ya malipo yoyote na akarudishiwa pesa ya ziada  hurudisha  kiasi kilichozidi.  Ikiwa  amemwona mtu  ambaye amedondosha fedha  au amepoteza kitu chochote humrudishia. Kwa kufanya hivyo analitii na kulitenda neno la Mung linavyosema, “Umwonapo ng’ombe wa nduguyo au kondoo wake akipotea....sharti umrudishe kwa nduguyo. Na kwamba yule nduguyo hayuko karibu nawe, na ukiwa humjui, umchukue kwenu nyumbani kwako, uwe naye hata aje nduguyo kumtafuta, nawe mrudishie....tena fanya vivyo kwa kila kitu kilichopotea cha nduguyo,....” Kum 22:1-3.

  • Umuhimu wa kuwa mwaminifu.
  • Mkristo ambaye ameokoka akiwa ni mwaminifu,  Mungu anamwamini na kumweka katika kazi ya utumishi.  Tunaweza kujifunza kwa baadhi ya watu ambao Mungu aliwaona ni waaminifu na kuwachagua na kuwafanya kuwa watumishi wa kazi yake, mfano  wa Yesu, Musa na  Paulo  “....Yesu aliyekuwa mwaminifu kwake yeye aliyemweka, kama Musa naye alivyokuwa, katika nyumba yote ya Mungu. Na Musa kweli alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama  mtumishi....” Ebr 3:1,5. Mtume Paulo alikuwa ni mwaminifu ndio maana  ameandika akisema, “Namshukuru Kristo Bwana wetu, aliyenitia nguvu kwa sababu aliniona kuwa mwaminifu, akaniweka katika utumishi wake.” 1Tim 1:12.

  • Yampasayo mtu ili aweze kudumu katika uaminifu.
  • Bwana wetu Yesu Kristo alipokuwa hapa duniani kwa sababu alikuwa ni mwaminifu kila alipojaribiwa na alizitambua hila za shetani wala hakufanya kosa lolote. Ndio maana ulipokaribia wakati wa kukamatwa aliwaambia wanafunzi wake akisema, “....yuaja mkuu wa ulimwengu huu hana kitu kwangu.” Yn 14:30.

  • Kwa mkristo ambaye ameokoka, amejazwa Roho mtakatifu na kudumu katika uaminifu, Roho mtakatifu humfunulia hila zote za Shetani anapojaribiwa. Waliosimama imara katika neno la Mungu Shetani huja na kuwajaribu katika shida na dhiki. Usikubali mawazo ya shetani, bali mpinge na kumkemea, kwa kumwambia, nenda zako Shetani. “Ndipo Yesu alipomwambia, Nenda zako, Shetani,....Kisha Ibilisi akamwacha....” Mt 4:10-11. “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia,  Mkaribieni Mungu naye atawakaribia ninyi....” Yak 4:7-8. Kutokana na andiko hili mtu anaweza kuwa karibu na Mungu  na kumkemea Shetani naye huondoka, ikiwa analitii neno na kuishi linavyosema.

  • Wale wote waliozaliwa mara ya pili imewapasa kuushinda ulimwengu na dhiki kwa sababu aliye ndani yao ni mkuu kuliko shetani, naye Yesu alimshinda na kushuhudia akisema, “Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.” Yn 16:33. Kwa upande mwingine, tunapolifahamu neno la Mungu tunazitambua hila za shetani na kumshinda. “Nao wakamshinda kwa damu ya mwana-kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao, ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.” Ufu 12:11. “....Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima....Yeye ashindaye hatapatikana na madhara ya mauti ya pili (Jehanum).” Ufu 2:11-11.

  • Kinachotokea kwa  mtu anayedumu katika uaminifu.
  • 1. Mungu humbariki na uzao wake. “Mtu mwaminifu atakuwa na Baraka tele” Mit 28:20.
  •  “Mwenye haki aendaye katika unyofu (uaminifu) wake, Watoto wake wabarikiwa baada yake.” Mit 20:7.

  • 2. Mungu anakuwa karibu naye wakati anapomwita au kumwomba. “Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.” Zab 145:18.

  • 3. Anampendeza Mungu. “Walio wakamilifu katika njia zao humpendeza.” Mit 11:20.

Maoni

  1. Mungu awabariki lakini pia naomba somo la utii

    JibuFuta
  2. Mbarikiwe sana nimejifunza na kuna mahali nimevuka

    JibuFuta
  3. Bila jina20:58

    Nikweli Familia,Jamii,Selikali,KANISA nahata Mungu mwenyewe anamtafta mtu mwaminifu amuwakilishe Duniani

    JibuFuta
  4. Bila jina10:37

    Nahisi kubarikiwa amina

    JibuFuta
  5. Bila jina14:02

    Ameni ameni hakika nimejifunza mambo mengi

    JibuFuta
  6. Bila jina13:01

    Hakika nabarikiwa sana

    JibuFuta
    Majibu
    1. Bila jina04:17

      Naitaiji maombi zaidi asante nimemshinda shetani

      Futa
  7. Bila jina21:29

    Hakika mmekuwa chanzo Cha utakatifu kwangu

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa Roh

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu    - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi  kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea  Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi  maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa ajili ya kufanya uamuzi. Ndio maana Yesu  alipokuwa akifundisha  alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi kwa hiari maisha ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. “ "Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanyeni mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya,  kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana"   Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana  Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"     Walawi  19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio