Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUMCHA BWANA MUNGU WAKO.

Neno kumcha Bwana lina maana ya kumwogopa au kumhofu Mungu. Tuangalie ni nani anaweza kuwa na hofu ya Mungu? Jibu la swali hili ni kwamba mtu anayeweza kumhofu Mungu ni yule ambaye ameamua kumpenda Mungu. Uthibitisho wa mtu anayempenda  Mungu ni yule ambaye hufanya haya yafuatayo; .

1.Anaishi neno la Mungu linavyosema.

2. Ana bidii kufanya ibada kwa Mungu.  Pia kwa njia ya maombi, kumsifu na kumwabudu Mungu.

3.Anachukia dhambi na kuziepuka.

4.Furaha yake ni kumwabudu Mungu. Asipofanya ibada anahisi amepungukiwa ile nafasi ya kukaa mbele za Bwana. Mtu wa namna hiyo anakuwa amemwishia Bwana.
Ndio maana imeandikwa, Zaburi 34:9 "Mcheni Bwana, enyi watakatifu wake, ....” Watakatifu ni wale watu ambao wamejitolea  maisha yao kwa Mungu na kumpenda kuliko mambo yoyote ya dunia hii.

Tunaweza kujifunze kwa Yesu Kristo ambaye ndiye kielelezo alikuwa anamcha Mungu. Ndio maana imeandikwa katika Isaya 11:2-3 "Na roho ya Bwana atakaa juu yake, .... roho ya maarifa na kumcha Bwana; .... na furaha yake itakuwa katika kumcha Bwana;...”

Imeandikwa katika Mithali 16:6 ".... kwa kumcha Bwana watu hujiepusha na maovu.” Kutokana na andiko hilo linamaanisha watu walio na hofu ya Mungu hawatendi dhambi kwa sababu wanamwogopa Mungu. Ndiyo maana neno la Mungu linafundisha katika Zaburi 4:4 "mwe na hofu wala msitende dhambi, ...." Andiko hilo linasisitiza kwa watu wote, kuwa na hofu ya Mungu na kukataza kutenda dhambi. Wanadamu wote wanapaswa kumhofu Mungu na kila mtu kuuchunguza moyo wake kwa yale anayoyatenda. Je, unayoyatenda yanampendeza Mungu ?

Ikiwa mtu ataishi katika dhambi anakuwa hana hofu ya Mungu. Kwa sababu hiyo Mungu atamwacha kwa sababu hakai na mwenye dhambi. Yeye ni mtakatifu hukaa na watakatifu. Isaya 57:15
Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.

Maoni

  1. asante kwa mafundisho

    JibuFuta
  2. Bila jina19:53

    Mungu akuzidishie roho Hekima, ili tuzidi kujifunzq kwako

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...