Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUUKOMBOA WAKATI.

Ninajua Mungu aliumba ulimwengu na vyote vilivyomo na vinatokana na yeye. Na pia aliweka majira na wakati, tunaweza kufahamu na kuona kuna majira ya mchana na usiku. Yote hayo aliyafanya kwa kusudi lake kamili. Tukiangalia kusudi la Mungu kumuumba mwanadamu ni ili amtumikie na kumwabudu.

Kwa sababu hiyo yampasa mkristo aliyeokoka au mtumishi wa Mungu kuukomboa wakati na kuutumia muda  kila siku kwa ajili ya kuutafuta uso wa Mungu. Ni muhimu kufahamu ya kwamba muda ukishapita kama hujautumia vizuri hautarudi tena.Ukishaupoteza muda unakuwa umepata hasara. Ijapokuwa mtu anaweza kuwa na shughuli nyingi za kila siku katika maisha yake ni muhimu atenge muda kwa ajili kufanya ibada mbele za Mungu. Angalao atenge muda wa lisaa limoja asubuhi na jioni lisaa limoja. Yesu alipokuwa na wale wanafunzi wake Katika maombi kwenye  bustani ya Gethsemane alifikiri wangeomba hata lisaa limoja. “Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa? Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”. Mathayo 26:40.

Jambo lingine la kuangalia ni muhimu kuepuka mambo ambayo sii ya lazima.  Jihadhari na kuwa na kiasi usitumie muda wako mwingi  zaidi  kwenye  Facebook,  TV,  Whatsapp, Twitter,  na  biashara.  Mambo  hayo huchukua nafasi na kukupotozea muda wa kumtafuta Mungu. Kama utautumia muda vizuri utakuwa na muda mwingi zaidi wa kuutafuta uso wa Mungu. Mkristo aliye na bidii ya kuutafuta uso wa Mungu na kumpendeza anakuwa na amani itokayo  kwa Mungu. Pia anakuwa karibu sana na Mungu. Naye Roho Mtakatifu atampasha habari kutoka kwa Mungu. “...huyo Roho wa kweli... hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari”. Yohana 16:13-14. Kusoma zaidi bofya hapa; Mungu anavyosema.

Tuaweza kujifunza kutoka kwa Yesu ya kwamba alikuwa na ratiba ambayo ilikuwa ya kudumu kwa ajili ya kuutafuta uso wa Mungu. “Basi, kila mchana alikuwa akifundisha hekaluni, na usiku huenda kulala katika mlima uitwao wa Mizeituni. Akatoka akaenda mpaka mlima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake; wanafunzi wake nao wakafuatana naye”. Luka 21:37; 22:39. Haya maandiko yanaonesha wazi ya kwamba ilikuwa ni desturi kwake kwenda mlimani kuomba kila siku. Kwa sababu hiyo ndio maana alikuwa na uwezo na mamlaka ya Mungu juu yake.  Hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kumshinda yule maovu na majaribu yake na kuwa salama kama hafanyi maombi kila siku. Ndio maana mstari wa hapo juu Yesu alisema ‘ombeni msije mkaingia majaribuni.’  

Alitahadharisha kwa kusema maneno hayo kwa sababu shetani siku zote anawatafuta wale ambao wamesimama imara katika Mungu ili kuwajaribu wamkosee Mungu. Ndio maana alimjaribu Yesu na Mitume nao wakamshinda kwa maombi na neno la Mungu. Kulifamu neno la Mungu ni muhimu ili tuweze kugundua uongo wa Shetani na kumpinga. “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze”. 1 Petro 5:8.  “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.
Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”. Yakobo 4:7-8.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...