Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 12, 2017

MUNGU ANAVYOSEMA NA WATUMISHI WAKE.

Tutaangalia katika somo hili jinsi Mungu anavyosema na watumishi wake. Kuna  njia ambayo Mungu alitumia kusema na wana wa Israel kupitia  watumishi wake  wakati wa Agano la Kale  na Agano Jipya ilikuwa ni kwa njia ya manabii. Mungu alipotaka kusema na wana wa Israel alimtuma nabii na kumwaagiza maneno ambayo atawaambia watu wake. Ndio maana imeandikwa,  "Maana  unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu".   2 Petro 1:21. Kutokana na andiko hili linaonyesha wazi nabii yampasayo kuzingatia. Jambo la kwanza kwa mkristo au mtumishi aliyeokoka ni lazima atoe unabii kwa mapenzi ya Mungu (yaani kwa matakwa Mungu). Jambo la pili ili mkristo au mtumishi aliyeokoka aweze kutoa unabii ni lazima awe ameongozwa na Roho mtakatifu.   Njia hii ni mojawapo tu lakini zipo njia nyingine ambazo Mungu hutumia kusema na watu wake  ambazo ni kama ifuatavyo; 1. Kwa njia ya...