Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MUNGU ANAVYOSEMA NA WATUMISHI WAKE.

Tutaangalia katika somo hili jinsi Mungu anavyosema na watumishi wake. Kuna njia ambayo Mungu alitumia kusema na wana wa Israel kupitia  watumishi wake  wakati wa Agano la Kale  na Agano Jipya ilikuwa ni kwa njia ya manabii. Mungu alipotaka kusema na wana wa Israel alimtuma nabii na kumwaagiza maneno ambayo atawaambia watu wake. Ndio maana imeandikwa,  "Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu". 2 Petro 1:21. Kutokana na andiko hili linaonyesha wazi nabii yampasayo kuzingatia. Jambo la kwanza kwa mkristo au mtumishi aliyeokoka ni lazima atoe unabii kwa mapenzi ya Mungu (yaani kwa matakwa Mungu). Jambo la pili ili mkristo au mtumishi aliyeokoka aweze kutoa unabii ni lazima awe ameongozwa na Roho mtakatifu. Njia hii ni mojawapo tu lakini zipo njia nyingine ambazo Mungu hutumia kusema na watu wake  ambazo ni kama ifuatavyo;

1. Kwa njia ya maono na ndoto.
Mtume Paulo alipewa maelekezo na Mungu kupitia maono sehemu ambayo atakwenda kuhubiri. “Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, kumsihi, na kumwambia, vuka, uje Makedonia utusaidie”. Matendo 16:9. 

2. Kwa njia ya malaika.
Malaika wa Mungu alimtokea Zakaria  ambaye ni Kuhani alipokuwa katika zamu yake ya akivukiza uvumba  hekaluni. Mungu alimpa taarifa ya kwamba maombi  aliyomwomba Mungu ameyasikia, na kuhusu mtoto atakayezaliwa.
 "Akatokewa na malaika wa Bwana, amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia.
Zakaria alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia. Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana". Luka 1:11-13. 

3. Kwa njia ya Yesu Kristo.
 “Mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika mwana aliyemwekwa kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.” Waebrania 1:2.

4. Kwa njia ya Roho Mtakatifu.
Mungu alisema na Mitume kupitia Roho Mtakatifu. "Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia.Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa", Matendo 16:6-7.  "Na Petro alikuwa akiyafikiri yale maono. Roho akamwambia, Wako watu watatu wanakutafuta. Basi ondoka ushuke ufuatane nao, usione tashwishi, kwa maana ni mimi niliyewatuma". Matendo 10:19,20.

Sababu za kutosikia sauti ya Mungu.
Kuna mambo ambayo ni sababu ya mtu kushindwa kuisikia sauti ya Mungu. Mambo hayo ni haya yafuatayo;

1.Kutozaliwa mara ya pili na kuokoka. Ikiwa mtu hajaokoka hana uhusiano na Mungu. Kwa sababu hiyo hawezi kuisikia sauti ya Mungu.

2. Kutosamehe waliokukosea na kuweka kinyongo, chuki na uadui.

3. Kuisha katika dhambi.
Maisha ya dhambi ni pale mtu anaposema uongo, usengenyaji, wivu, chuki, kinyongo, uadui, mawazo mabaya, dharau, kujivuna, kujisifu, kujiona bora kuliko wengine, ubaguzi,  kutamani mke au mume wa mtu mwingine, na mambo mengine yote yasiyompendeza Mungu.

Mungu huongea kwa kusudi maalumu.
Siyo kila wakati Mungu anasema na watu wake, bali hufanya hivyo kwa kusudi lake na kwa uhitaji wa mtu kwa yale ambayo anamwomba au  kumwuliza Mungu jambo fulani ambalo anahitaji jibu kutoka kwake.

Sababu ya pili. Mungu husema kwa ajili ya kuwaonya watu wake ikiwa wameishi maisha ya dhambi ili waweze  kumgeukia yeye kwa njia ya  kutubu na kuziacha dhambi zao na  kuwapa maelekezo namna ya  kuishi sawasawa na neno lake  asije akawahukumu.

Sababu ya tatu. Mungu husema na watu wake kwa ajili ya kufariji na kutia moyo kutokana na dhiki na shida wanazopitia katika maisha yao.

Sababu ya nne.  Mungu anaweza kusema kwa ajili ya kusudi lake maalumu. Kusudi hilo linaweza kuwa kwa ajili ya mtu binafsi, Kanisa, Taifa au ulimwengu.

Tahadhari kuhusu kusikia sauti, kuota ndoto, kuona maono na unabii.
Jambo muhimu kwa kanisa na watumishi wa Mungu ni kuwa makini wasiamini kila sauti watakayoisikia kwa sababu si kila sauti inatokana na Mungu.  Wakati mwingine huwa ni sauti ya shetani na malaika zake ambao waliomwasi Mungu na kupoteza nafasi zao  Mbinguni. Ndio maana tukisoma maandiko tunaweza kuona  shetani alivyosema na Hawa na kumdanganya ale matunda aliyokatazwa na Mungu asile.  ”Nyoka akamwambia mwanamke. Hakika, hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya... Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula...Alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.“ Mwanzo 3:4-6.

Kuhusu ndoto ni muhimu kuwa makini kwa sababu kuna ndoto zinazotokana na fikra au mawazo  ambayo yanatokana na mambo uliyoyaona, kuyasikia au kuyahisi. “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno” Mhubiri 5:3Vilevile mtu anaweza kuota ndoto ambazo hutokana na Shetani kwa sababu anaisha maisha ya dhambi. Huweza kuota ndoto ambazo ni mbaya, za kutisha na mateso. 

Pia kuhusu maono. Sii maono yote yanatokana na Mungu, bali  mengine yaweza kutoka kwa shetani. Tukisoma katika biblia kuna andiko linalohusu mwanamke mchawi aliyemwona nabii Samweli  ambaye alikuwa amekufa siku nyingi zilizopita kwa njia ya shetani. Ilikuwa ni baada ya Sauli kumwendea ili ambashirie “Yule mwanamke akamwambia Sauli, Ninaona mungu anatoka katika nchi naye akamuuliza ni mfano wa nini? Akamjibu, Ni mzee anazuka; naye amefunikwa vazi. Basi Sauli akatambua ya kwamba ndiye Samweli mwenyewe…”  1Samweli 28:13.  

Sehemu nyingine  tunaweza kuona shetani alipomjia Yesu ili kumjaribu na kwa muda mfupi alimwonyesha  utajiri wote wa dunia hii. “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia. Ndipo Yesu akamwambia, Nenda zako, Shetani, kwa maana imeandikwa, msujudie Bwana Mungu wako umwabudu yeye peke yake. Kisha Ibilisi akamwacha; na tazama, wakaja malaika wakamtumikia." (Mathayo 4:8-11).

Kuhusu unabii. Unabii wowote unaotolewa  unapaswa kupimwa  ndipo kuuthibitisha kama umetokana na Mungu. Kuhusu sehemu hii nitaelezea unabii uliotolewa na manabii ambao waliingiwa na pepo wabaya kwa ajili ya kutabiri uongo na hatimaye Ahabu alidangaywa ili auwawe vitani. Wale pepo walimwambia Mungu, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo vinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka, ukafanye hivyo. 2Nyakati 18:22.

Kupima unabii, ndoto na maono  kwa usahihi ni kwa njia zifuatazo;
  1. Neno la Mungu.
  2. Roho Mtakatifu.

Ni muhimu kwa kila mkristo na mtumishi wa Mungu aliyeokoka ayafahamu mambo haya yafuatayo; 

1. Awe anayafahamu maneno ya Mungu kwa ukamilifu


2. Awe  anadumu katika utakatifu kwa kuishi sawasawa na maneno ya Mungu yanayosema. 


3. Awe amejazwa Roho mtakatifu


Mambo hayo matatu ni muhimu sana kwa kanisa. Ikiwa mtu amekamilika katika mambo hayo anaweza   kupambanua na kuthibitisha ya kuwa unabii, ndoto na maono yametokana na Mungu au shetani.


Ili kufahamu zaidi bofya hapa: Jinsi ya kuwatambua manabii wa kweli.

Maoni

  1. Mungu akubariki sana
    Nimebarikiwa sana

    JibuFuta
  2. Bila jina01:10

    Mfano mzuri ambao Yesu mwenyewe alishuka akiongea na mtu ni pale alipo mkemea sauli ambaye ni paulo

    JibuFuta
  3. Bila jina04:51

    Barikiwa

    JibuFuta
  4. Bila jina15:19

    UBARIKIWE MNOO

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...