Ili mtu ajue matumizi sahihi ya damu ya Yesu ni muhimu aangalie neno la Mungu linavyosema. pia kwa kila jambo ambalo mtu analitenda ni muhimu kwanza kulithibitisha kwa kutumia neno la Mungu na kuona kama linaendana sawasawa na maandiko. Kwa hiyo jambo lolote linalopingana na neno la Mungu sii halali kulifanya. Ikiwa mtu atatenda jambo lolote lililo kinyume na neno la Mungu atakuwa amefanya dhambi. Kwa sababu hiyo yampasa kila mmoja aliyeokoka kujua matumizi sahihi ya damu ya Yesu sawasawa na neno la Mungu.
Matumizi ya damu Yesu ni haya yafuatayo:
1. Kuosha dhambi za ulimwengu. Ndio maana andiko linasema,"Bali tukieneda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake yatusafisha dhambi zetu. 1Yohana 1:7." "Hao ndio watokao katika dhiki iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo (Yesu) . Ufunuo 7:14."
2. Kanisa limenunuliwa kwa damu ya Yesu.Ndio maana imeandikwa, " Nanyi mfahamu ya kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au kwa dhahabu...bali kwa damu ya thamani, kama ya Mwana-Kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo. 1Petro 1:18-19." "...Kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa. Ufunuo wa Yohana 5:9."
3. Kuondoa dhambi ya ulimwengu.
Ndio maana Yesu alikuja kama Mwana-Kondoo kwa ajili ya dhambi za ulimwengu na damu yake ilimwagika pale msalabani. Kwa sababu hiyo Yesu akasema, "Kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi. Mathayo 26:28." Andiko linginge linaonyesha wakati Yohana mbatizaji alipomwona Yesu alimthibitisha akasema, "...Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu". Yohana 1:29."
"Naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote" 1Yohana 2:2." "Na kwa yeye kuvipatanisha vitu vyote kwa nafsi yake, akiisha kufanya amani kwa damu ya msalaba wake; kwa yeye, ikiwa ni vitu vilivyo juu ya nchi, au vilivyo mbinguni. Wakolosai 1:20."
Katika maandiko hayo yanaonyesha Yesu ndiye anayempatanisha mtu mwenye dhambi na Mungu. Ni pale mtu anapomgeukia Mungu kwa kuweka nia moyoni mwake kuachana na dhambi, kumwamini Yesu na kutubu.
Yesu alikufa mara moja.
Imeandikwa, "Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; ...Warumi 6:10." Kwa sababu Yesu alikufa mara moja, pia damu yake ilimwagika mata moja, wala haikumwagika kila siku. Bali kwa damu ya Yesu watu wanapata ondoleo la dhambi zao. Kwa sababu hiyo kuitumia damu ya Yesu kwa namna nyingine sii sahihi. Katika neno la Mungu hakuna mahali popote ambapo Mungu anatoa ruhusa kuitumia kwa namna nyingine. Kwa sababu hiyo kuitumia katika kuombea mtu kwa kusema damu ya Yesu imfunike na kumlinda. Ifunike biashara yake, ifunike watoto wake. Kuomba au kusema ninanyunyiza damu ya Yesu katika nyumba hii, ninanyunyiza damu ya Yesu katika biashara hii. Kuomba kwa namna hiyo ni kinyume na neno la Mungu. Na si hivyo tu, ikiwa mtu anaitumia damu ya Yesu kama ulinzi kwa kusema kwa damu ya Yesu najifunika, au damu ya Yesu ilinde nyumba hii au gari hili, haya sii matumizi ya damu ya Yesu.
Damu ya Yesu ni kwa ajili ya kumtakasa mtu na kumweka wakfu kwa Mungu. Kulingana na neno la Mungu wakati wa agano la kale imeandikwa karibu vitu vyote vilitakaswa kwa damu sawa sawa na sheria ya Mungu. "Maana kila amri lipokwisha kunenwa na Musa kwa hao watu wote, kama ilivyomuru sheria, aliitwaa damu ya ndama na ya mbuzi, pamoja na maji na sufu nyekundu na hisopo, akakinyunyizia kitabu chenyewe, na watu wote, akisema, Hii ni damu ya agano mliloamriwa na Mungu. Na ile hema nayo na vyombo vyote vya ibada alivinyunyizia damu vivyo hivyo. Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo, Waebrania 9:19-22." Kwa sababu hiyo tunasafishwa na kuondolewa dhambi.
Baada ya kuelezea kazi au matumizi ya damu ya Yesu.
Kuhusu ulinzi wetu neno la Mungu linasema "Nanyi mnalindwa na nguvu za Mungu kwa njia ya imani...1Petro 2:5."
Pia imeandikwa,"Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa. Zaburi 34:7."
Kwa hiyo kutokana na maandiko haya yanaonyesha wazi tunalindwa na NGUVU ZA MUNGU na MALAIKA.
Ndugu zangu katika Bwana ninawasihi kwa jina la Yesu Kristo yatupasa kufahamu kuomba sawasawa na neno la Mungu. Na kufamya yote sawasawa na neno lake.
Mungu Baba yetu katika Jina la Yesu atujalie nuru ya ufahamu katika mioyo yetu ili tufahamu jinsi itupasavyo kuomba na kufanya yote katika mapenzi yake. Amen.
Amina mtumishi wa mungu.Endelea kujifunza zaidi kuhusu damu ya Yesu kimatumizi.
JibuFutaBarikiwa Sana
JibuFutaAmina sana mtumishi hapa nmezidi kuongeza maarifa zaidi
JibuFutaNimejifunza na kuelewa umuhimu wa Damu ya Yesu
JibuFuta