Karibu katika somo hili na kulifuatilia kwa makini nawe utajengwa na kuzidi kuimarika katika neno la Mungu. Nianze kwa kusema kuwa neno la Mungu ni njia, na ni nuru katika maisha yetu. Neno la Mungu limefananishwa na njia kwa sababu mtu akiishi sawasawa na neno linavyosema anajua anakokwenda na kwamba anafuata njia sahihi na wala hatapotea kamwe. "Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru" (Yn 8:32). Sehemu nyingine neno limefananishwa na nuru. Ikiwa mtu anaishi sawasawa na neno la Mungu linavyosema, mtu huyo anatembea katika nuru kungali mchana wala hatapotea njia. Kwa sababu hiyo neno la Mungu ndilo linatufundisha na kufahamu mambo yote ambayo Mungu alitukirimia katika Kristo Yesu. Mojawapo ya mambo hayo ni;
1. Alituweka huru kutoka laana zote za ukoo, familia na mababu wa zamani. Na si hivyo tu alituweka huru mbali na mikosi na balaa. Ni kwa sababu hiyo Yesu Kristo alifanyika laana itokanayo na torati kwa ajili yetu. Ndiyo maana andiko linasema, "Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanyika laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa , Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti." (Gal 3:13). Kwa sababu hiyo hakuna laana kwa mtu ambaye ameokoka kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu na kutusamehe dhambi. "...Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi. Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli." (Yn 8:34, 36). Maandiko haya mawili hapa juu yanafundisha kuhusu kazi moja ya kuwekwa huru na kutengwa mbali na laana na dhambi. Na si hivyo tu, ila kwa upendo wa Mungu ulio mkuu kwetu alitutoa katika utawala wa nguvu za giza na kutuingiza katika ufalme wa Yesu. Kwa hiyo sasa, kwa watu wote waliomkubali na kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao wanaishi katika ufalme wa Mungu pamoja na Yesu Kristo ambaye ni Mwana wake. "Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake" (Kol 1:13).
2. Kwa mtu ambaye amekwishaokoka mapepo hayana nafasi katika maisha yake. Kwa sababu amezaliwa kwa mara ya pili kwa roho na maji na pia amemwamini Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake na kufanyika mwana wa Mungu. Vile vile akiishi sawasawa na neno lisemavyo, hakika hakuna pepo atakayemkaribia wala kuingia ndani yake. Yeye yuko huru mbali na pepo kwa sababu amekwisha kuokolewa kutoka mamlaka ya giza. Mtu ambaye ameokoka anakuwa ni kiumbe kipya kwa sababu ameyaaacha mambo ya zamani yasiyofaa (yaani dhambi). Huyo amezaliwa kwa roho na kufanyika upya roho yake, na kuwa na namna ya Mungu ya Utakatifu. "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama! yamekuwa mapya" (2Kor 5:17)
Mtu ambaye anaweza kupagawa na pepo ni yule anayeishi maisha ya dhambi. Atendaye dhambi anakuwa ametengana na Mungu na ndipo pepo wabaya humwingia na kuishi ndani yake. Ndiyo maana Yesu alionya na kusema madhara yatakayosabishwa na pepo baada ya kuondolewa ndani ya mtu. Lakini ikiwa mtu hakuishi maisha ya utakatifu pepo watamwingia tena na kufanya makao ndani yake. "Pepo amtokapo mtu...Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya" (Mat 12:43-45.)
1. Alituweka huru kutoka laana zote za ukoo, familia na mababu wa zamani. Na si hivyo tu alituweka huru mbali na mikosi na balaa. Ni kwa sababu hiyo Yesu Kristo alifanyika laana itokanayo na torati kwa ajili yetu. Ndiyo maana andiko linasema, "Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanyika laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa , Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti." (Gal 3:13). Kwa sababu hiyo hakuna laana kwa mtu ambaye ameokoka kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu na kutusamehe dhambi. "...Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi. Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli." (Yn 8:34, 36). Maandiko haya mawili hapa juu yanafundisha kuhusu kazi moja ya kuwekwa huru na kutengwa mbali na laana na dhambi. Na si hivyo tu, ila kwa upendo wa Mungu ulio mkuu kwetu alitutoa katika utawala wa nguvu za giza na kutuingiza katika ufalme wa Yesu. Kwa hiyo sasa, kwa watu wote waliomkubali na kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao wanaishi katika ufalme wa Mungu pamoja na Yesu Kristo ambaye ni Mwana wake. "Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake" (Kol 1:13).
2. Kwa mtu ambaye amekwishaokoka mapepo hayana nafasi katika maisha yake. Kwa sababu amezaliwa kwa mara ya pili kwa roho na maji na pia amemwamini Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake na kufanyika mwana wa Mungu. Vile vile akiishi sawasawa na neno lisemavyo, hakika hakuna pepo atakayemkaribia wala kuingia ndani yake. Yeye yuko huru mbali na pepo kwa sababu amekwisha kuokolewa kutoka mamlaka ya giza. Mtu ambaye ameokoka anakuwa ni kiumbe kipya kwa sababu ameyaaacha mambo ya zamani yasiyofaa (yaani dhambi). Huyo amezaliwa kwa roho na kufanyika upya roho yake, na kuwa na namna ya Mungu ya Utakatifu. "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama! yamekuwa mapya" (2Kor 5:17)
Mtu ambaye anaweza kupagawa na pepo ni yule anayeishi maisha ya dhambi. Atendaye dhambi anakuwa ametengana na Mungu na ndipo pepo wabaya humwingia na kuishi ndani yake. Ndiyo maana Yesu alionya na kusema madhara yatakayosabishwa na pepo baada ya kuondolewa ndani ya mtu. Lakini ikiwa mtu hakuishi maisha ya utakatifu pepo watamwingia tena na kufanya makao ndani yake. "Pepo amtokapo mtu...Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya" (Mat 12:43-45.)
Amina sana Mtumishi wa Mungu akubariki katika kuifanya kazi yake,naomba somo la matumizi ya damu ya yesu na ulinzi juu ya
JibuFutawatakatifu.
Asante Sana kwa injili sahihi.Mungu aitwaye Jehovah akubariki katika Jina la Yesu Kristo Amen and amen.
JibuFuta