Mkristo wa kweli ni mtu yule ambaye ameokoka na kukionja kipawa cha nguvu za Mungu. Na pia ametoa mwili wake kuwa sadaka kwa Mungu. Kwa sababu hiyo kwa kufanya hivyo ni ibada kwa Mungu. Ndio maana imandikwa kwenye "Warumi 12:1 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana."
Nikutie moyo wewe ambaye umeokoka ni muhimu kuwa na sifa ambazo nimezieleza hapa juu. Hayo ndiyo maisha ambayo Mungu amekusudia tuyaishi, na ndipo tunakuwa watakatifu kama Mungu alivyosema; "Kwa kuwa mimi ni BWANA... Mungu wenu; basi mtakuwa watakatifu, kwa kuwa mimi ni Mtakatifu." Mambo ya Walawi 11:45."
Lakini pia anakuwa na shauku au kiu kwa ajili ya kumwabudu Mungu. Kwa sababu hiyo, wakristo wa namna hiyo wanapokuwa katika kumwabudu Mungu watauona uzuri wa Mungu na uwepo wa nguvu zake.Wanatamani wakati wote kudumu katika utakatifu. Pia hujilinda na kuepuka kufanya dhambi. Huyapenda mambo ya Mungu kuliko ya dunia.Vilevile huwa ni watu mwenye bidii katika kumtafuta Mungu kwa kuomba, kufunga na kumsifu Mungu.
Jambo lingine hawapendezwi na mambo yasiyo ya haki. Watu kama hao ndio watakaourithi ufalme wa Mungu.
Ni kwa sababu wameshinda majaribu ya yule maovu na ndani yao hamna hila. Hao ndio watu ambao Yesu alisema; "...watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa wamestahili.Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake. Ufunuo wa Yohana 3:4-5."
Ni kwa sababu wameshinda majaribu ya yule maovu na ndani yao hamna hila. Hao ndio watu ambao Yesu alisema; "...watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa wamestahili.Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake. Ufunuo wa Yohana 3:4-5."
Nikutie moyo wewe ambaye umeokoka ni muhimu kuwa na sifa ambazo nimezieleza hapa juu. Hayo ndiyo maisha ambayo Mungu amekusudia tuyaishi, na ndipo tunakuwa watakatifu kama Mungu alivyosema; "Kwa kuwa mimi ni BWANA... Mungu wenu; basi mtakuwa watakatifu, kwa kuwa mimi ni Mtakatifu." Mambo ya Walawi 11:45."
Maoni
Chapisha Maoni