Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MUNGU NDIYE ATENDAYE MIUJIZA.

Tunaweza kuona ya kwamba vitu vyote ambavyo Mungu ameviumba ni muujiza kwetu. Pia aliumba kwa namna ya pekee jua, mwezi, nyota na sayari nyingine mbalimbali ambazo  aliziweka juu ya anga, huku zikiwa zinaning’inia bila kushikiliwa na kitu chochote, wala hazidondoki. Pia bahari nayo imekaa mahali ilipoamriwa bila kuvuka mpaka alioiwekea Bwana. Kwa hiyo tunapoona uumbaji wa vitu vyote ambavyo Mungu aliviumba vinashangaza, navyo ni ishara  kwetu ya kutosha na kutambua ya kwamba Mungu yupo. Kwa sababu hiyo yatupasa kufahamu ya kwamba yeye ndiye mwenye uwezo wote, yeye hutenda mambo yote sawasawa na mapenzi yake. Kwa hiyo tunaweza kuona Sababu ya Mungu kufanya muujiza kwa mkono wa Musa mbele ya Farao na Wamisri. Mungu akamwambia Farao; “lakini, nilikusimamisha wewe kwa sababu hii hii, ili nikuonyeshe uweza wangu, tena kwamba jina langu litangazwe katika dunia yote.” Kutoka 9:16. Kutokana na andiko hili hapa juu linazungumzia Mungu alifanya miujiza ili kumwonyesha Farao uweza wake. Na Kusudi lingine ni ili jina la Mungu litangazwe duniani kote. Ndio maana hata sasa Jina la Mungu linatangazwa ulimwengu kutokana na matendo makuu aliyoyatenda kwa nyakati tofauti.


Pia yatupasa kutambua ya kwamba Mungu ndiye atendaye miujiza yote. Kwa sababu hiyo hakuna mtu mwenye uwezo wa kufanya muujiza. Ndio maana mtume petro aliwahutubia Waisraeli akawaambia; “Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;” Matendo ya Mitume 2:22. Hili andiko hapa juu linamaanisha ya kwamba Mungu alifanya miujiza, ajabu na ishara kwa mkono wa Yesu Kristo. Kwa hiyo Mungu alimtumia kufanya matendo ya miujiza.


Kwa sababu hiyo yawapasa waliookoka kuwa makini na kufahamu kuna kanuni na mwongozo wa neno la Mungu kuhusu kufanya muujiza. Katika kanisa kuna baadhi ya wakristo  ambao wamejaliwa kuwa na karama ya muujiza. Wanaweza kutumiwa na Mungu ikiwa watafuata kanuni na mwongozo wa neno la Mungu linavyosema. Kwa hiyo mtu anaweza kufanya muujiza kwa mapenzi ya Mungu na kuongozwa na Roho wa Mungu. Kwa sababu hiyo mtu hawezi kufanya muujiza kwa matakwa yake au kama yeye apendavyo. Lakini kama mtu atataka kufanya muujiza  kwa matakwa yake haiwezi kutokea. Ila kwa mtu aliye mnyenyekevu na kutaka mapenzi ya Mungu yatimizwe, huyo ndiye hutenda miujiza kwa imani na kuongozwa na Roho Mtakatifu.


Mambo yakuzingatia ili mtu aweze kutumiwa na Mungu katika maisha yake ni haya yafuatayo;
1.Kudumu katika utakatifu. Hii ndiyo njia ambayo inampendekeza Mungu. Ndio maana Mungu amesema, “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.” Zaburi 16:3.


2. Kumwomba Mungu siku zote.
3. Kumsifu na kumwabudu Mungu.
4. Kufunga mara kwa mara.


5. Kuyatoa maisha yako kwa ajili ya Mungu na kumhofu yeye. Kufanya hivyo ni Jambo la msingi katika kumtumikia Mungu. Ndivyo Bwana wetu Yesu kristo alifanya, yeye ni kielelezo katika maisha yetu. Imeandikwa “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;” Waebrania 5:7. Andiko hili limeonyesha wazi ya kuwa Yesu alimtolea Mungu mwili wake na kumhofu.
6. Kunyenyekea.


Kutokana na fundisho hili ninashauri ya kwamba mtu ambaye anatumiwa na Mungu kwa  karama ya miujiza awe makini asije akampa mtu tumaini ya kwamba Mungu atafanyia muujiza  fulani, wakati Mungu hajamthibitishia hivyo. Kuna mtumishi mmoja alikuwa anahubiri katika kanisa fulani. Katika kanisa hilo kulikuwa na mama mmoja ambaye hajafanikiwa kuwa na mtoto. Yule mtumishi akamwambia yule mama majira kama haya mwaka ujao utakuwa na mtoto, lakini haikuwa kama alivyomwahidi. Kwa sababu hiyo yule mama alipewa tumaini ambalo si kweli.


Kwa hiyo si sahihi kuwatangazia watu wenye shida mbalimbali waje kanisani au kwenye mkutano wa injili na Bwana atawaponya na kuwaweka huru. Ni muhimu kutambua ya kwamba kuna kusudi kuu la Mungu ambalo ni kuhubiri habari njema (injili).  Kwa hiyo hilo ndilo kusudi kuu la Mungu kwa watu wake. Kwa sababu hiyo mtumishi wa Mungu akiwa anahubiri habari njema ya ufalme wa Mungu kwa usahihi na huku akiwa amedumu katika neno la Mungu. Mtu wa namna hiyo neema ya Mungu inakuwa juu yake kwa ajili ya kulithibitisha neno la Mungu kwa ishara na maajabu. Tunaweza kuona kupitia wale mitume, imeandikwa;
“Nao wale wakatoka, wakahubiri kotekote, Bwana akitenda kazi pamoja nao, na kulithibitisha lile neno kwa ishara zilizofuatana nalo.]” Marko 16:20.


Kuepuka mazoea.
Kwa mtu aliye na karama ya miujiza. Ni muhimu kufahamu ya kwamba si kila mara Mungu atamtumia kutenda miujiza. Yeye Mungu hutenda kwa wakati na kwa kusudi maalum. Kwa mfano kama miujiza imetendeka katika mji fulani, lakini si lazima itendeke mji mwingine kwa sababu inategemea mapenzi ya Mungu.


Pia inategemea imani na utii kwa wale wanaohubiriwa habari njema. Hapa ngoja nikupe  mfano ili uweze kuelewa. Kulikuwa na watu kumi ambao waliokuwa na ukoma walimwendea Yesu huku wakiamini  angeweza kuwaponya. Lakini aliwapa agizo wakajionyeshe kwa Kuhani. Walipokuwa njiani wanaelekea kwa Kuhani walipona. Waweze kuona kwa sababu ya imani yao na kutii agizo walilopewa ndio maana walipona. “Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali, wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu! Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.”
Luka 17:12-14. Vilevile kulikuwa na mtu aliyepooza naye akapewa agizo. “Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako. Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastaajabu wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, Namna hii hatujapata kuiona kamwe.”  Marko 2:11-12. Kwa hiyo pasipo imani na utii hakuna muujiza kutoka kwa Mungu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...

UPONYAJI WA MAGONJWA.

Chanzo cha magonjwa. Kuna magonjwa yanayotokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya yule mtu ambaye aliyekuwa mngonjwa akamwabia,   “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi”   Yn 5:14.   Ikiwa mtu aliyeokoka akirudia kuishi maisha ya dhambi pepo mchafu anapoona nafasi anachukua pepo wengine na kuingia kwake. Yesu alisema,  “Mara huenda akachukua pamoja naye    pepo    wengine walio waovu    kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”   Mt 12:45.    Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili. Kwa upande mwingine mtu anaweza akawa ni mgonjwa au amekosa lishe.  Uponyaji wa Mungu.                     Mambo ya kuzingatia na kuponywa ni ha...

KUWEKWA HURU KUTOKA DHAMBI YA UZINZI NA UASHARATI.

Jambo la kwanza ninamshukuru Mungu kwa neema yake aliyonipa kufundisha neno lake. Ndungu mpendwa ninajua ya kwamba Mungu alikupenda sana, hata akamtoa Mwana wake wa pekee Yesu Kristo kwa ajili yako ili akukomboe kutoka katika dhambi zote ikiwemo dhambi ya uzinzi na uasherati. Sasa ninakusihi kwa neema ya Mungu fuatana nami kwa makini kuhusu  somo hili nawe utauna utukufu wa Mungu katika maisha yako. Tunaweza kuangalia kwa makini dhambi ya uzinzi na uasharati ambayo mtu akiitenda inaharibu ufahamu wake na hatimaye kuangamia. Mtu anapoteza uhusiano wake na Mungu, mawasiliano kati yake na Mungu yanakatika. Mungu  ni Makatifu hana ushirika na wenye dhambi. “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.” Mithali 6:26.   “Lakini maovu yenu yamewafarikisha (yamewatenganisha) ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki  kusikia.”   Isahau 59:2. Atendaye dhambi ya zinaa au  uasherati ...

KUDUMU KATIKA UPENDO WA MUNGU.

Neno la Mungu katika Biblia linatufudisha kuhusu upendo wa Mungu  kwetu. Yeye Mungu ndiye  mwanzo wa upendo kwa sababu alitupenda kwanza. “...alitupenda sisi kwanza”.   1 Yohana 4:19. Jinsi mtu anavyoweza kuwa na upendo wa Mungu. Ni pale mtu anapokuwa amezingatia kudumu katika upendo wa Mungu kama ifuatavyo; 1.Kuishi sawasawa na maagizo yote ya neno la Mungu na kumpenda. “Na sasa, Israeli, BWANA, Mungu wako, anataka nini kwako, ila umche BWANA, Mungu wako, na kwenda katika njia zake zote, na kumpenda, na kumtumikia BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote;”   Kumbukumbu la Torati 10:12.   “Lakini mjibidiishe sana kuzifanya amri na sheria, ambazo Musa, mtumishi wa BWANA, aliwaamuru, kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kwenenda katika njia zake zote, na kuzishika amri zake, na kushikamana na yeye, na kumtumikia kwa moyo wenu wote na nafsi yenu yote”.   Yoshua 22:5. 2. Jambo lingine la kuzingatia ni kwamba yampasa mtu kuyashika maagiz...

MADHARA YA DHAMBI.

Huu ni wakati mwingine ambao Bwana amenijalia kuwepo kwa kusudi lake jema. Nitaelezea katika somo hili kuhusu dhambi ilivyo na madhara kwa mtu aitendaye. Kwanza tuangalie dhambi  ilivyoanza kwa Adamu na Hawa ni wakati walipokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambayo Mungu aliwakataza wasile. Kwa sababu hiyo dhambi ilisababisha madhara mengi kwa uzao wake na vizazi vyote duniani. Kwa hiyo shida zote zilizopo duniani zimetokana na dhambi. Kutokana na wazazi wetu wa kwanza Adamu na Hawa kwa kuwa walitenda dhambi na vizazi vingine vyote vimehesabiwa ni wenye dhambi. Mtu  anazaliwa akiwa na asili ya dhambi kutoka kwa wazazi wa kwanza Adamu na Hawa. Warumi 3:23 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;” Kutokana na sababu hiyo ndio maana kila mwanadamu anakufa sawasawa na Mungu  alivyosema katika kitabu cha Mwanzo 2:16-17 “BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa u...