Mzazi au mlezi yampasa kufahamu ya kwamba yeye mfano wa kuigwa katika familia. Kwa kawaida watoto hujifunza mambo wanayoyaona au kusikia kwa wazazi, walezi, Waalimu na watu wengine. Kwa hiyo watoto kuwa na maadili mema au mabaya ni kutokana na malezi ya pande zote. Kwa kawaida watoto walivyo bado hawajaweza kupambanua yaliyo mema na mabaya. Lakini wakielimishwa wanaweza kutambua yaliyo mema na mabaya.
Kuna mambo ya muhimu ambayo mtoto anapaswa kufundishwa ni haya yafuatayo:
1.Kumfundisha mtoto kusema neno asante. Neno asante ni muhimu kwa kila mtu apewapo kitu au kutendewa jambo lolote jema. Kwa hiyo yampasa kusema neno asante. Kwa kufanya hivyo ni jambo jema na pia ni maadili kwa watu wa rika zote.
Kama mtu mzima hatoi shukrani kwa yale mema ambayo ametendewa huenda yamkini hakulelewa tangu akiwa mtoto ya kwamba yampasa akipewa chakula au amemnunulia nguo aseme asante, au anapopewa kitu chochote na wazazi wake. Usipomlea mtoto katika maadali mema atakapokuwa mtu mzima hataona umuhimu wa kushukuru. Ndio maana kuna baadhi ya watu hawawezi kusema neno la shukrani. Ndio maana kuna mithali inasema umleavyo mtoto ndivyo akuavyo. Kutokana na msemo huo unadhihirisha wazi mambo mawili.
Jambo la kwanza na msingi ni mzazi au mlezi kumlea mtoto katika maadili mema. Kwa sababu hiyo atakua katika maadili. Kwa hiyo katika maisha yake atakuwa anaishi katika maadili mema, ndio maana neno linasema “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.” Mithali 22:6 Lakini ikiwa hatalelewa katika maadili yanayofaa atakuwa hana maadili mema katika maisha yake. Kwa hiyo ni muhimu kwa wazazi au walezi kuwa makini na kuwasaida ili baadae nao waweze kuwa wazazi wenye maadili mema.
2. Kumfundisha mtoto maneno ya Mungu na jinsi ya kumwabudu kwa kufanya maombi, kutoa Sadaka kumsifu na kumshukuru.
3. Kumfundisha kuwa mkarimu. Ni wakati umempa biskuti au karanga na kumwambia amgawie mtu mwingine. Ikiwa hatafanya hivyo endelea kumzoesha kwa kuchukua ulichompa kama ni karanga na kumgawia mtu mwingine halafu mbakizie zake . Kwa kufanya hivyo unakuwa umemfundisha kuwa mkarimu. Kwa sababu hiyo siku nyingine akipewa karanga anaweza kumngawia mtoto mwenzake au mtu mwingine. Hiyo ndiyo njia sahihi ya kuondoa ubinafsi na uchoyo ndani ya nafsi ya mtoto.
Jambo lingine mzazi au mlezi
anapokuwa anapika ni muhimu kuwa makini asimpe mtoto chakula kabla ya kuwekwa mezani. Nasema hivyo kwa sababu mtoto anapoona chakula anachokipenda sana anaweza kulia na kuomba apewe. Kama utakuwa unampa kidogo huko jikoni kabla ya chakula kuwekwa mezani utakuwa unamjenga mtoto kuwa na tabia ya ubinafsi na uchoyo. Kwa hiyo yakupasa kumwambia asubiri mpaka chakula kiwekwa mezani naye atapewa.
1.Kumfundisha mtoto kusema neno asante. Neno asante ni muhimu kwa kila mtu apewapo kitu au kutendewa jambo lolote jema. Kwa hiyo yampasa kusema neno asante. Kwa kufanya hivyo ni jambo jema na pia ni maadili kwa watu wa rika zote.
Kama mtu mzima hatoi shukrani kwa yale mema ambayo ametendewa huenda yamkini hakulelewa tangu akiwa mtoto ya kwamba yampasa akipewa chakula au amemnunulia nguo aseme asante, au anapopewa kitu chochote na wazazi wake. Usipomlea mtoto katika maadali mema atakapokuwa mtu mzima hataona umuhimu wa kushukuru. Ndio maana kuna baadhi ya watu hawawezi kusema neno la shukrani. Ndio maana kuna mithali inasema umleavyo mtoto ndivyo akuavyo. Kutokana na msemo huo unadhihirisha wazi mambo mawili.
Jambo la kwanza na msingi ni mzazi au mlezi kumlea mtoto katika maadili mema. Kwa sababu hiyo atakua katika maadili. Kwa hiyo katika maisha yake atakuwa anaishi katika maadili mema, ndio maana neno linasema “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.” Mithali 22:6 Lakini ikiwa hatalelewa katika maadili yanayofaa atakuwa hana maadili mema katika maisha yake. Kwa hiyo ni muhimu kwa wazazi au walezi kuwa makini na kuwasaida ili baadae nao waweze kuwa wazazi wenye maadili mema.
2. Kumfundisha mtoto maneno ya Mungu na jinsi ya kumwabudu kwa kufanya maombi, kutoa Sadaka kumsifu na kumshukuru.
3. Kumfundisha kuwa mkarimu. Ni wakati umempa biskuti au karanga na kumwambia amgawie mtu mwingine. Ikiwa hatafanya hivyo endelea kumzoesha kwa kuchukua ulichompa kama ni karanga na kumgawia mtu mwingine halafu mbakizie zake . Kwa kufanya hivyo unakuwa umemfundisha kuwa mkarimu. Kwa sababu hiyo siku nyingine akipewa karanga anaweza kumngawia mtoto mwenzake au mtu mwingine. Hiyo ndiyo njia sahihi ya kuondoa ubinafsi na uchoyo ndani ya nafsi ya mtoto.
Jambo lingine mzazi au mlezi
anapokuwa anapika ni muhimu kuwa makini asimpe mtoto chakula kabla ya kuwekwa mezani. Nasema hivyo kwa sababu mtoto anapoona chakula anachokipenda sana anaweza kulia na kuomba apewe. Kama utakuwa unampa kidogo huko jikoni kabla ya chakula kuwekwa mezani utakuwa unamjenga mtoto kuwa na tabia ya ubinafsi na uchoyo. Kwa hiyo yakupasa kumwambia asubiri mpaka chakula kiwekwa mezani naye atapewa.
Ikiwa mtoto anadokoa chakula jikoni au kitu kingine chochotea si vema kusema huyu
ni mtoto anapokua ataacha. Akiachwa bila kuonywa tabia ya udokozi itakuwa ndani yake hata atapokuwa mtu mzima. Kwa hiyo ni muhimu kumwonya mapema angali mtoto. Kwa kuwa umleavyo mtoto ndivyo akuavyo.
Kuna baadhi ya wapishi wenye uchu wa nyama au chakula wanachokipenda wakati wanapopika wanakula kwa kiasi fulani huko jikoni. Mtu wa namna hiyo ni mlafi hawezi kurithi ufalme wa Mungu. “...ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” Wagalatia 5:21.
4. Kumfundisha mtoto kula kwa kiasi. Ikiwa kuna chakula anachokipenda sana mpe kwa kiasi cha kushiba. Baada ya kula akiomba kuongezewa chakula mwongezee kidogo sana, au mwambie ulichokula kinatosha. Watoto wadogo huwa wanaelewa wakielekezwa.
4. Kumfundisha mtoto kula kwa kiasi. Ikiwa kuna chakula anachokipenda sana mpe kwa kiasi cha kushiba. Baada ya kula akiomba kuongezewa chakula mwongezee kidogo sana, au mwambie ulichokula kinatosha. Watoto wadogo huwa wanaelewa wakielekezwa.
5. Kumfundisha mtoto Kuwa na nidhamu. Awe anaamkia watu ambao ni wakubwa kwake kwa umri. Awaheshemu wageni wanaokuja nyumba kwako bila kuwasumbua.
Kwa hiyo ili tuweze kuwa na taifa lenye maadili mema ni lazima mtoto ajengwa katika maadili mema kuanzia nyumbani. Kwa hiyo siyo sahihi kuwaacha watoto kuangalia picha katika televisheni na intaneti ambazo siyo salama kwa watoto, zinaharibu maadili ya watoto. Pia kuna baadhi ya machapisho ambayo yana picha na maneno yasiyo salama kwa watoto. Kwa hiyo yakupasa kumlinda na kumwelimisha mtoto wako kwa kumweleza ni yapi yanafaa na yasiyofaa.
Jambo lingine la muhimu yakupasa kutambua kuhusu mtoto wako rafiki zake ni nani! Ili kuchunguza na kubaini tabia za hao rafiki zake. Je? Ni nzuri au ni mbaya. Njia ya kutumia ni kupitia mtoto mwenyewe kwa kuwa na ukaribu naye kwa maongezi. Kwa mfano unaweza ukamuuliza rafiki zake ni nani! hata kama unawafahamu. Kwa hiyo anaweza kukuambia habari za watoto wengine na hata za rafiki zake. Kwa sababu hiyo unaweza kufahamu maadili ya marafiki zake na watoto wengine. Kama atakuwa amekueleza tabia za watoto ambazo ni kinyume na maadili mema mshauri kwa kumwambia hayo wanayoyafanya siyo maadili mema. Pia mkataze asije akayaiga hayo. Vilevile mwepumshe mtoto wako na marafiki wabaya. Kwa kufanya hivyo utakuwa umemjenga katika maadili mema.
Kwa hiyo ili tuweze kuwa na taifa lenye maadili mema ni lazima mtoto ajengwa katika maadili mema kuanzia nyumbani. Kwa hiyo siyo sahihi kuwaacha watoto kuangalia picha katika televisheni na intaneti ambazo siyo salama kwa watoto, zinaharibu maadili ya watoto. Pia kuna baadhi ya machapisho ambayo yana picha na maneno yasiyo salama kwa watoto. Kwa hiyo yakupasa kumlinda na kumwelimisha mtoto wako kwa kumweleza ni yapi yanafaa na yasiyofaa.
Jambo lingine la muhimu yakupasa kutambua kuhusu mtoto wako rafiki zake ni nani! Ili kuchunguza na kubaini tabia za hao rafiki zake. Je? Ni nzuri au ni mbaya. Njia ya kutumia ni kupitia mtoto mwenyewe kwa kuwa na ukaribu naye kwa maongezi. Kwa mfano unaweza ukamuuliza rafiki zake ni nani! hata kama unawafahamu. Kwa hiyo anaweza kukuambia habari za watoto wengine na hata za rafiki zake. Kwa sababu hiyo unaweza kufahamu maadili ya marafiki zake na watoto wengine. Kama atakuwa amekueleza tabia za watoto ambazo ni kinyume na maadili mema mshauri kwa kumwambia hayo wanayoyafanya siyo maadili mema. Pia mkataze asije akayaiga hayo. Vilevile mwepumshe mtoto wako na marafiki wabaya. Kwa kufanya hivyo utakuwa umemjenga katika maadili mema.
Amen 🙏
JibuFutaNimependa ubarikiwe
JibuFutaSawa mtumishi ubarikiwe
JibuFuta