Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YAMPASAYO MWALIMU AU MHUBIRI.

Ninayo furaha kwa ajili ya wakati huu ambao Mungu amenijalia kufundisha neno lake. Ni wakati muhimu wa kujifunza  neno la Mungu ambalo ni habari njema inayotujenga katika imani. Kwa hiyo tunajegwa na kuwa imara katika kumtumikia Mungu.

Kwa sababu hiyo ili watumishi wa Mungu wajengwe na kuwa imara katika neno la Mungu wanapaswa kujifunza kwa bidii. Jambo lingine wanapaswa kujifunza kwa watumishi wengine wanapokuwa wanafundisha au kuhubiri neno la Mungu.

Ikiwa mtumishi wa Mungu anajihesabia haki ya kwamba anajua mambo yote ya Mungu Si sahihi, bali anajidanganya nafasi yake mwenyewe. Lakini tunaweza kuyafahamu maneno ya Mungu katika ukamilifu wote. Ila hatuwezi kuyafahamu mambo yote ya Mungu kwa sababu si yote ametufunulia.  Ndio maana Imeandikwa;
“Mambo siri ni ya BWANA, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria hii.” Kumbukumbu Torati 29:29. “Kwa maana tunafahamu kwa sehemu;...”  1 Wakorintho 13:9.

Tunaweza kuona habari njema ya wokovu ilikuwa imefichwa, lakini kwa pendo lake Mungu aliwafunulia manabii na mitume. Kwa sababu hiyo wakaweza kuihubiri siri ya Mungu kwa mataifa yote. Ndio maana mtume Paulo alisema; “Sasa na atukuzwe yeye awezaye kuwafanya imara, sawasawa na injili yangu na kwa kuhubiriwa kwake Yesu Kristo, sawasawa na ufunuo wa ile siri iliyositirika tangu zamani za milele,” Warumi 16:25. “pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili;”
Waefeso 6:19.

Kwa sababu hiyo kuna mambo ambayo yamefichwa  katika neno la Mungu. Ikiwa mwalimu au mhubiri anayo bidii ya kujifunza yeye mwenyewe na kwa watumishi wengine atakuwa amejifunza jambo jipya. Kwa hiyo kwa kadri  anavyojifunza anazidi kuyafahamu mambo ya Mungu.

Jambo la muhimu kuzingatia tambua ya kwamba Mungu hufunua mambo yaliyofichwa katika neno lake kwa wale wote wampendao.  “Siri ya BWANA iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake.” Zaburi 25:14. “Maana mtu mkaidi ni chukizo kwa BWANA, Bali siri yake ni pamoja na wanyofu.” Mithali 3:32.  

Mwalimu au mhubiri wa kweli anapaswa kuwa mfano kwa  wengine kama ifuatavyo;
1.Ni muhimu  aishi neno la Mungu linavyosema.

2. Awezaye kufundisha na kuhubiri kwa usahihi neno la Mungu.

3. Awezaye kuomba sawasawa na neno la Mungu.


4. Mazungumzo yake ni lazima yaendane na neno la Mungu.

5. Anayefaa mavazi vyenye staha (heshima).

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...