Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUISHI MAISHA YA UKAMILIFU.

Yesu alifundisha ya kwamba yatupasa  tuwe wakamilifu kama Baba yetu wa Mbinguni alivyo mkamilifu. Huku akiwa ameonyesha wazi upendo wa Mungu kwa wanadamu, jinsi Mungu anavyowatendea wema wenye haki na wasio haki. Kwa sababu hiyo yatupasa kutenda kama Mungu kwa kuonyesha
upendo wetu kwa watu wote.  

Je? Tunawezaje kuonyesha upendo wa Mungu kwa jinsi gani?  Jibu la swali hili ni kama ifuatavyo:
1. Kuwapenda watu wote.
2. Kuwatendea mema watu wote.
3, kuwaombea baraka watu wote. 
Kamwe! Hatuwezi kumpendeza Mungu kama tunawatakia adui zetu wapatwe na mabaya. Pia hatupaswi kuwaombea maadui zetu ili wapatwe na mabaya. , Hayo siyo mapenzi ya Mungu kwetu. Mapenzi ya Mungu katika maandiko yanasema; "Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo? Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo? Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.” Mathayo 5:43-48.“Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.” Warumi 12:14.

Kwa hiyo kutokana na somo hili mkristo ambaye ameokoka ili  aweze kuwa mkamilifu yampasa kuyatenda yale yote ambayo Mungu ameagiza katika sheria yake. Kwa sababu hiyo anakuwa ni mtakatifu kama Mungu alivyo mtakatifu.

Tunaweza kuona ya kwamba hakuna viwango vya ukamilifu na Utakatifu. Kiwango ni kimoja tu ambacho ni kuwa mkamilifu na mtakatifu kama Mungu alivyo. Inamaana yatupasa kuwa na utakatifu wa Mungu. Au kwa maelezo mengine kuwa sawa na Mungu katika utakatifu. Ndio maana amesema hivi; 
“Nanyi mtakuwa watakatifu kwangu mimi; kwa kuwa mimi BWANA ni mtakatifu nami nimewatenga ninyi na mataifa, ili kwamba mwe wangu.” Walawi 20:26. “kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.” 1 Petro 1:16. Kwa hiyo andiko hili hapa juu linaonyesha wazi ya kwamba mtu atakuwa ametengwa na kuwa mali ya Mungu iwapo atakuwa ni mtakatifu kama Mungu alivyo mtakatifu. Kwa sababu hiyo ikiwa kuna mtu anadhani hakuna mwanadamu anayeweza kuwa mkamilifu na mtakatifu huyo hayajui maandiko kwa ukamilifu. Ingekuwa ni jambo ambalo haliwezekani kwa mwanadamu kutimiza Mungu asingetoa agizo watu wake wawe watakatifu. Na pia asingesema “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.” Zaburi 16:3. Pia andiko lingine linathibitisha na kuonyesha ya kwamba mwanadamu anaweza kuishi maisha ya utakatifu. Ikiwa ameweka nia moyoni  kuzishika amri. Ndio maana imeandikwa;
Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito. 1 Yohana 5:3

Jambo lingine ambalo si sahihi ikiwa mtu anafikiri ya kwamba mkristo anapookoka anakuwa ni mchanga na bado anatenda dhambi siyo kweli. Kwa sababu  mtu anapozaliwa kwa mara ya pili anakuwa ameamua kuachana na dhambi na kuungama na kuwa kiumbe kipya. Pia anakuwa ni mkamilifu na mtakatifu kama Baba yetu wa mbinguni alivyo. Mkristo anapookoka anakuwa ni mchanga kwa sababu bado hayajui sana maneno ya Mungu. Ila anakuwa ameyafahamu maneno ya Mungu kwa sehemu ndio maana akaokoka. Ukiangalia kwa makini katika neno la Mungu limeweka wazi jambo hili; ndio maana imeandikwa, “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.” 2 Wakorintho 5:17.  “Ila sasa ninakwenda Yerusalemu, nikiwahudumu watakatifu;”
Warumi 15:25. Mtumishi wa Mungu mtume Paulo alithibitisha ya kwamba kanisa la Yerusalemu ni watakatifu. Pia alithibitisha na makanisa mengine  yaliyokuwa sehemu mbalimbali vilevile walikuwa ni watakatifu. Alikuwa na maana ya kwamba wakristo waliookoka siku za karibu na wale wa waliookoka tangu siku nyingi wote ni watakatifu. 

Hapa nitaelezea kuhusu wakristo wachanga na wale walioukulia wokovu.
“Kwa maana, iwapasapo kuwa  waalimu, (maana wakati mwingi umepita), mnahitaji kufundishwa na mtu mafundisho ya kwanza ya maneno ya Mungu; nanyi mmekuwa mnahitaji maziwa wala si chakula kigumu. Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.” Waebrania 5:12-14.  Kutokana na maandiko hayo yanaonyesha makundi mawili ya wakristo waliookoka ambao ni kama watoto wachanga na watu wazima.

Mtoto mchanga ni mkristo ambaye ameokoka lakini bado hajakuzwa kwa ukamilifu kwa mafundisho ya awali au ya kwanza ya neno la Mungu.

Na mtu mzima ni mkristo  aliyeokoka na kufundishwa mafundisho ya kwanza na  kuukulia wokovu. Kwa sababu hiyo kwa kadiri anavyoendelea kufundishwa neno la Mungu anakuwa amepewa chakula cha watu wazima.

Ili mtu aliyeokoka aweze kudumu katika ukamilifu na utakatifu ni lazima azingatie haya yafuatayo;
1 Yampasa kutawala moyo wake asiwaze mabaya wala kutamani mambo yasiyofaa.
2. Yampasa kutawala kinyme chake asije akasema maneno yasiyofaa. Andiko linasema, “... Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu. Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum.” Yakobo 3:2,6. Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema. 1 Wakorintho 15:33.

Kipimo cha utakatifu.
Kama mkristo atapima utakatifu wake kwa  miujiza anayoifanya au kwa kunena kwa lugha mpya hiyo siyo njia sahihi.

Mkristo anaweza kuuthibitisha utakatifu wake kwa njia zifuatazo;
1. Ikiwa  anaishi  sawasawa na neno la Mungu linavyosema. 
2. Ikiwa ameziungama dhambi
  zote na kusamehewa.
3. Anaishi maisha yasiyo na
   dhambi yoyote.
Kwa sababu hiyo akiwa mtu  amethibitisha utakatifu alio nao kupitia njia hizi hapa juu ndipo anakuwa na uhakika ya kwamba yeye ni mtakatifu. Naye Roho  mtakatifu humshuhudia nafsni mwake. 

Sasa unaweza kubofya hapa chini na kuendelea na soma linalosema;  KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...