Ninafundisha mambo ambayo ni sababu kwa mkristo aliyeokoka kupoteza imani yake. Tutaangalia matokeo yatokanayo kwa mkristo ambaye amepoteza imani. Ni kama ifuatavyo;
1. Anakuwa amepoteza ujasiri wa Mungu ndani yake. Kwa sababu hiyo anakuwa na hofu na mashaka. Hali ya kutoamini inachukua nafasi moyoni mwake. Tunaweza kuona na kujifunza kwa Yesu Kristo alivyowafundisha wale mitume wake. “Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu. Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Marko 11:22-23.”
2. Jambo lingine mkristo anapokuwa amepoteza imani anakuwa hana matumaini kwa Mungu.
Mambo ambayo ni sababu ya mtu kupoteza imani yake; Ni haya yafuatayo.
1.Kuishi katika dhambi.
2. Kuwa na mashaka.
”Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.
Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.
Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote. Yakobo 1:6-8.”
”Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku.
Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.
Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote. Yakobo 1:6-8.”
Ni muhimu kutambua kusudi la Mungu kwetu, alipotuumba aliweka kanuni mojawapo ambayo ni kuishi kwa imani kwa kumtumaini Mungu. Pia kuishi maisha ya haki. Mtu anaweza kuishi maisha ya haki kwa kuyatenda mambo yote sawasawa na neno la Mungu. Kwa sababu hiyo humpendeza Mungu kama ilivyoandikwa; ”Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye. Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho zetu. Waebrania 10:38-39.” Kuna jambo la kujifunza kutokana na huu msitari hapa juu. Unaonesha ikiwa mtu anashindwa kumtumaini Mungu na kumtegemea na kusta sita atapotea. Ina maana atahukumiwa na kutupwa Jehanum ya moto na kuteseka milele. Hata hivyo katika kitabu cha Waebrania Jambo hilo limeandikiwa. ”Tena ni akina nani aliowaapia ya kwamba hawataingia katika raha yake, ila wale walioasi? Basi twaona ya kuwa hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutokuamini kwao. Waebrania 3:18-19.”
Mambo ya kuzingatia ili kujengwa,kuimarishwa na kudumu katika imani ni haya yafuatayo;
1.Kujifunza neno la Mungu kwa bidii na kujengwa katika imani.
“Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo. Warumi 10:17.”
“Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo. Warumi 10:17.”
2 .Kuyaweka maneno ya Mungu moyoni mwako. Ukifanya hivyo ni rahisi kutambua mambo yoyote ambayo ni kinyume na neno la Mungu na kuyaepuka. “Moyoni mwangu nimeliweka neno lako,
Nisije nikakutenda dhambi. Zaburi 119:11.”
Nisije nikakutenda dhambi. Zaburi 119:11.”
3. Kuishi maisha ya kumpendeza Mungu. “Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako. Zaburi 119:9.
4. Kuishi kwa kumtumaini na kumtegemea Mungu katika mambo yote. “Wamtumainio BWANA ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele. Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu,
Ndivyo BWANA anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele. Zaburi 125:1-2.” Kutokana na andiko hilo linaonesha ya kwamba mtu anayemtumaini Bwana atakuwa imara na kulindwa na yeye.
Ndivyo BWANA anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele. Zaburi 125:1-2.” Kutokana na andiko hilo linaonesha ya kwamba mtu anayemtumaini Bwana atakuwa imara na kulindwa na yeye.
5. Kuomba na kufunga. Ni jambo la muhimu sana na kuzingatia kwa sababu kuna mambo ambayo hayawezekani ila kwa kuomba na kufunga.
Ndio maana Bwana wetu Yesu Kristo kabla ya kufanya huduma ya kuhubiri habari njema na kufanya matendo makuu kuna mambo ya kwanza ambayo yangefanyika kwake ni kama ifuatavyo;
•Alibatizwa.
•Alijazwa Roho Mtakatifu.
•Aliongozwa na Roho kufunga.
Baada ya hayo ndipo alianza kuhubiri na kutenda matendo makuu ya Mungu.
Maoni
Chapisha Maoni