Hivi sasa ni nyakati za mwisho na yule mwovu amekuwa na wivu kwa ajili ya wale ambao wamesimama imara na kumtumikia Mungu. Kwa sababu hiyo halali usingizi anafanya bidii mchana na usiku ili amwangushe mmojawapo.
“Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. 1Petro 5:8.”
Kwa hiyo kila mkristo aliyeokoka na kusimama imara yampasa kuwa makini asije akayaamini mafundisho na mahubiri ya uongo na kupotea. Nyakati hizi kuna baadhi ya watu ambao wanafundisha na kuhubiri kwa kupotosha neno la Mungu katika biblia. Wanayoyafundisha tunaweza kuyambua kwa sababu yako kinyume na maandiko. Kwa hiyo ukiyalinganisha na maandiko katika biblia hayaendani, bali yanapingana. Njia nyingine ya kuwatambua waalimu wa uongo ni kupitia maisha wanayoishi ambayo ni kinyume na neno la Mungu.
“Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua. Mathayo 7:16,18,20.”
“Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua. Mathayo 7:16,18,20.”
Kwa hiyo jinsi ya kuwapima ni kama ambavyo nimeeleza hapa juu. Kwa sababu hiyo siyo sahihi kuwaamini waalimu wa uongo kwa sababu ya miujiza wanayoifanya. Ndio maana Bwana wetu Yesu Kristo alitahadharisha kwa kusema; “Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule. Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele. Mathayo 24:24-25.”
Ni muhimu mkristo kufahamu ya kwamba kuna miujiza ya aina mbili kama ifuatavyo;
1.Miujiza itokayo kwa Mungu.
2.Miujiza itokayo kwa Shetani.
Tunaweza Kuona miujiza ya Shetani ilifanyika wakati wa Musa na Ayubu. Shetani alishusha moto na kuvumisha upepo wenye nguvu kutoka jangwani ukaangamiza wanyama, watumishi na watoto wake Ayubu. Pia wachawi waliifanya fimbo kugeuka na kuwa nyoka. “Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Moto wa Mungu umeanguka kutoka mbinguni na kuwateketeza kondoo, na wale watumishi, na kuwaangamiza; mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Ayubu 1:16,18-19.”
“Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Wanao na binti zako walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa; mara, tazama, upepo wenye nguvu ukatoka pande za jangwani, ukaipiga hiyo nyumba pembe zake nne, nayo ikawaangukia hao vijana, nao wamekufa; na mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Ayubu 1:16,18-19.”
“Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Wanao na binti zako walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa; mara, tazama, upepo wenye nguvu ukatoka pande za jangwani, ukaipiga hiyo nyumba pembe zake nne, nayo ikawaangukia hao vijana, nao wamekufa; na mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Ayubu 1:16,18-19.”
“BWANA akanena na Musa na Haruni, akawaambia, Farao atakaponena nanyi, na kuwaambia, Jifanyieni miujiza; ndipo utakapomwambia Haruni, Shika fimbo yako, uibwage chini mbele ya Farao, ili iwe nyoka. Basi Musa na Haruni wakaingia kwa Farao, wakafanya vivyo kama BWANA alivyowaambia; Haruni akaibwaga fimbo yake chini mbele ya Farao, mbele ya watumishi wake, ikawa nyoka. Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi; na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao. Wakabwaga chini kila mtu fimbo yake, nazo zikawa nyoka; lakini fimbo ya Haruni ikazimeza fimbo zao. Kutoka 7:8-12.
Maoni
Chapisha Maoni