Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2017

MTU ALIYEOKOKA ANAWEZAJE KUTAMBUA IMANI YA KWELI?.

Hivi sasa ni nyakati za mwisho na yule mwovu amekuwa na wivu kwa ajili ya wale ambao wamesimama imara na kumtumikia Mungu. Kwa sababu hiyo halali usingizi anafanya bidii mchana na usiku ili amwangushe mmojawapo. “ Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. 1Petro 5:8.” Kwa hiyo kila mkristo  aliyeokoka na kusimama imara yampasa kuwa makini asije akayaamini mafundisho na mahubiri ya uongo na kupotea. Nyakati hizi kuna baadhi ya watu ambao wanafundisha na kuhubiri kwa kupotosha neno la Mungu katika biblia. Wanayoyafundisha tunaweza kuyambua kwa sababu yako kinyume na maandiko. Kwa hiyo ukiyalinganisha na maandiko katika biblia hayaendani, bali yanapingana. Njia nyingine ya kuwatambua waalimu wa uongo ni kupitia maisha wanayoishi ambayo ni kinyume na neno la Mungu. “ Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala m...

MTU ANAVYOWEZA KUPOTEZA IMAINI.

Ninafundisha mambo ambayo ni sababu kwa  mkristo aliyeokoka kupoteza imani yake. Tutaangalia matokeo yatokanayo kwa mkristo ambaye amepoteza imani. Ni kama ifuatavyo; 1. Anakuwa amepoteza ujasiri wa Mungu ndani yake. Kwa sababu hiyo anakuwa na hofu na mashaka. Hali ya kutoamini inachukua nafasi moyoni mwake. Tunaweza kuona  na kujifunza kwa Yesu Kristo alivyowafundisha wale mitume wake. “ Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu. Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Marko 11:22-23.” 2. Jambo lingine mkristo anapokuwa amepoteza imani anakuwa hana matumaini kwa Mungu. Mambo ambayo ni sababu ya mtu kupoteza imani yake;  Ni haya yafuatayo. 1.Kuishi katika dhambi. 2. Kuwa na mashaka. ” Ila na aombe kwa imani, pasipo shaka yo yote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku. Maana mtu k...

UTUKUFU WA MUNGU HUSHUKA.

Ninaposema utukufu wa Mungu hushuka ni kweli. Tunaweza kuona na kudhibitisha katika maandiko ya kwamba Mungu wakati wa Agano la kale alidhihirisha uwepo wake aliposhuka katika wingu hekaluni.   "Hata makuhani hawakuweza kusimama ili kufanya huduma yao, kwa sababu ya lile wingu; kwa kuwa nyumba ya Mungu imejaa utukufu wa BWANA".   2 Mambo ya Nyakati 5:14.  Pia nyakati hizi za Agano jipya Mungu anadhihirisha uwepo wake katika Roho Mtakatifu wakati anaposhuka juu ya kanisa.  Kwa hiyo ni muhimu watumishi wa Mungu kuwa makini na kutambua uwepo wa Mungu unaposhuka. Ili kuacha nafasi ya ya kanisa kububujika katika Roho Mtakatifu bila kuwanyamazisha. Huo ni muda wa peke kwa kila mtu kujimimina kwa maomba, sifa na shukrani mbele za Mungu.  Kwa hiyo si vyema mtumishi wa Mungu  kuwanyamazisha waamini wakati Roho Mtakatifu anaposhuka juu yao. Kwa hiyo kufanya hivyo ni kumzimisha na kumzuia nafasi ya kutenda kazi katika wakatifu. " Msimzimishe Roho; msitweze unab...