Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUOMBA KWA NIDHAMU.





Kuomba kwa nidhamu ni jambo jema. Ikiwa mtu haombi kwa busara anakuwa anakera na kuwaudhi watu  wengine. Nimekuwa nikiona baadhi yao waliookoka wanapokuwa katika ibada wanafanya mambo ambayo si kwa kutumia busara. Ni haya yafuatayo:

1. Kuomba kwa kupaza sauti na kulia. Kufanya hivyo ni jambo jema ikiwa kanisa lina jambo zito ambalo wamepatana kuliombea. Lakini ukiwa na jambo lako lolote hata kama ni zito omba kwa  sauti ya kawaida na kulia kmya kimya. Wala usikunje uso wako. Tuaweza kujifunza kwa Hana alivyoomba kwa busara katika hekalu. Ijapokuwa alikuwa na jambo gumu hakupaza sauti na kulia. “Ikawa, hapo alipodumu kuomba mbele za BWANA, Eli akamwangalia kinywa chake. Basi Hana alikuwa akinena moyoni mwake; midomo yake tu ilionekana kama anena, sauti yake isisikiwe; kwa hiyo huyo Eli alimdhania kuwa amelewa.” 1 Samweli 1:12-13

2. Kuomba kwa kukunja uso. Kwa kufanya hivyo unakuwa umeharibu muonekano wa uso wako. “Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao, ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao.”  Mathayo 6:16

3. Kuomba kwa kutumia nguvu kwa njia ya kurusha rusha mikono. Kwa kufanya hivyo si sahihi kwa sababu kumwomba Mungu ni katika Roho mtakatifu, wala si kwa kutumia nguvu za mwili. “kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;.”  Waefeso 6:18

Ndugu wapendwa katika Bwana  tunaweza kuona mambo hayo kama ni ya kawaida, lakini yanaharibu heshima na hadhi ya kanisa la Mungu. Nasema hivyo kwa sababu wale ambao bado hajafahamu habari njema ya wokovu wataona tunafanya vitendo vya hovyo. Kwa sababu hiyo hawataelewa wokovu ni njia nzuri ya ufalme wa Mungu.

Hivi sasa kanisa ambalo ni mimi na wewe yatupasa kuwa makini  katika hekima ya Mungu na kufahamu ni jambo lipi linafaa kwa wakati gani. Pia kutambua ni jambo lipi lisilofaa na kuliacha. Ninawatakia neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi Amina.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...