Ruka hadi kwenye maudhui makuu

VIPIMO VYA HAKI.








Maana ya vipimo vya haki ni vipimo vyenye uwiano ulio sawa. Kwa mfano mizani ni kipimo chenye uwiano ulio sawa. Vipimo ambavyo siyo rasmi ambavyo jamii inavitumia kupimia bidhaa kama ndoo, magunia, nakadhalika. Vipimo hivyo ikiwa mtu anavitumia kwa namna isiyo sawa humpunja mnunuzi au muuzaji. Baadhi ya wanunuzi wanapokwenda kununua mazao kama viazi au vituguu wanataka gunia lijazwe kupita ujazo unaotakiwa hivyo hushonea ziada wanayoiita LUMBESA.

Kwa mfanya biashara  yampasa kuuza bidhaa zake sawasawa na bei ya sako. Ikiwa mtu anauza kitu chochote pia yampasa kuuza bei ya soko. Kwa sababu hiyo anakuwa ameuza kwa bei ya haki.
Lakini kwa mtu yule auzaye kitu au bidhaa yoyote kinyume na bei ya soko anakuwa amelangua au kwa neno lingine ni mlanguzi. Hapa nitatoa mfano ili uweze kuelewa zaidi. Ikiwa kitu kinauzwa kwa  bei ya soko ambayo ni Sh. 20,  lakini ukakiuza kwa shilingi 25 au kwa shilingi 30 unakuwa umeuza kwa bei isiyo ya haki. Kufanya hivyo siyo haki mbele ya Mungu, kwa kuwa Mungu amesema:
"Uwe na jiwe timilifu la haki, uwe na kipimo kitimilifu cha haki; zipate kuwa nyingi siku zako, katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako. Kwa kuwa wote wayatendayo mambo kama haya, wote watendao yasiyo haki, ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako. Msifanye yasiyo haki katika hukumu, wala katika kupima, wala katika mizani, wala katika cheo.” Kumbukumbu 25:15-16.
“Mwanangu, usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu. Maana;zitakuongezea wingi wa siku. Na miaka ya uzima, na amani.” Mithali 3:1-2

Kutokana na neno la Mungu hapa juu linaonyesha wazi ya kwamba mtu akitenda haki na kuishi sawasawa na sheria na amri za Mungu ataongezewa miaka nyingi ya kuishi hapa duniani. Ina maana ya kwamba hatakufa mapema kwa sababu amemtii Mungu kwa kutenda Sheria na amri zake. Pia atamjalia kuishi kwa amani.

Hapa nitaelezea maana ya neno Mlanguzi. Ni kama ifuatavyo;
1.Ni mtu anayenunua bidhaa,  kutoka kwa wakulima, kwa bei rahisi na kuwauzia wengine kwa bei ghali ili kupata faida kubwa.
 
2.Mfanyabiashara wa mnadani.
3.Mtu anayefanya biashara isiyo halali.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...