Kutokana na somo hili linalohusu je Shetani anaweza kuzuia maombi? Majibu swali hilo tunawe kuyapata kwa njia ya neno la Mungu ambalo ndio kweli. Ukweli wa neno la Mungu ndio njia sahihi kwa ajili ya kuthibitisha mambo yote. Kwa sababu hiyo yatupasa kuthibitisha mambo yote ambayo tunaamini kama ni sahihi na neno la Mungu. Jinsi ya kufahamu mambo yale tunayoamini kama ni sahihi ni pale yanapokuwa yanaendana au kukubaliana na neno la Mungu. Hiyo ndio imani sahihi. Lakini ikiwa mambo yoyote tunayoamini yanapingana na neno la Mungu hiyo ni imani isiyo sahihi. Kwa sababu hiyo mtu anakuwa anaishi kinyume na neno la Mungu. Ni muhimu kufahamu ya kwamba mtu ambaye anaishi katika imani isiyo sahihi hataingia katika ufalme wa Mungu.
Jibu la kichwa cha somo hapo juu ni kwamba Shetani hana nafasi wala mamlaka kuzuia maombi ya watakatifu.
Kwa sababu imeandikwa;
“BWANA yu mbali na wasio haki;
Bali huisikia sala ya mwenye haki.” Mithali 15:29. “Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.” 1 Petro 3:12. “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.” 1 Petro 3:7. Kutokana maandiko haya yanaonyesha wazi ya kwamba maombi huzuiliwa kutokana na dhambi. Kwa maneno mengine ina maana ikiwa mtu anaishi maisha ya dhambi, hicho ndio kizuizi cha maombi yake. Jambo lingine ambalo ni kizuizi cha maombi ni pale mtu anapokuwa hamsheshimu mkewe au mumewe. Na si hivyo tu; ikiwa mtu haheshimu watu wengine hicho pia ni kizuizi cha maombi. Pia kuna kizuizi kingine ambacho ni pale mtu anapoomba kwa nia mbaya au kinyume na neno la Mungu "Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu." Yakobo 4:3.
Kwa sababu hiyo sii sahihi kuamini Shetani anawez a kuzuia maombi ya watakatifu. Ijapokuwa Shatani alimzuia Malaika aliyetumwa kutoka kwa Mungu kwa ajili ya kumpelekea Danieli majibu ya maombi yake. “Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako. Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.” Danieli 10:12-13. Ni muhimu kufahamu ya kwamba maandiko ya hapa juu yanaonyesha wazi Mungu huwasikiliza na kuwaangalia wenye haki wanapomwomba yeye. Kwa sababu hiyo maombi ya watakatifu yanafika kwa Mungu bila kuzuiwa na Shetani.
“BWANA yu mbali na wasio haki;
Bali huisikia sala ya mwenye haki.” Mithali 15:29. “Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.” 1 Petro 3:12. “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.” 1 Petro 3:7. Kutokana maandiko haya yanaonyesha wazi ya kwamba maombi huzuiliwa kutokana na dhambi. Kwa maneno mengine ina maana ikiwa mtu anaishi maisha ya dhambi, hicho ndio kizuizi cha maombi yake. Jambo lingine ambalo ni kizuizi cha maombi ni pale mtu anapokuwa hamsheshimu mkewe au mumewe. Na si hivyo tu; ikiwa mtu haheshimu watu wengine hicho pia ni kizuizi cha maombi. Pia kuna kizuizi kingine ambacho ni pale mtu anapoomba kwa nia mbaya au kinyume na neno la Mungu "Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu." Yakobo 4:3.
Kwa sababu hiyo sii sahihi kuamini Shetani anawez a kuzuia maombi ya watakatifu. Ijapokuwa Shatani alimzuia Malaika aliyetumwa kutoka kwa Mungu kwa ajili ya kumpelekea Danieli majibu ya maombi yake. “Ndipo akaniambia, Usiogope, Danieli; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako. Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi.” Danieli 10:12-13. Ni muhimu kufahamu ya kwamba maandiko ya hapa juu yanaonyesha wazi Mungu huwasikiliza na kuwaangalia wenye haki wanapomwomba yeye. Kwa sababu hiyo maombi ya watakatifu yanafika kwa Mungu bila kuzuiwa na Shetani.
Ubarikiwe Sana kw somo zuri
JibuFutaManeno matamu sana
JibuFuta