Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MTU HUFANYA DHAMBI KWA HIARI.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu ni kweli mwanadamu hufanya dhambi kwa hiari. Nasema hivyo kwa sababu Mungu alimuumba mtu na kuweka ndani yake utashi wa kufanya maamuzi katika  mambo mbalimbali. Lakini sii kila jambo ambalo mwanadamu alifanyalo ni sawasawa na neno la Mungu. Ijapokuwa Mungu  ametuwekea hiari ndani yetu sii kwa ajili kuamua kutenda mabaya, bali ni kwa ajili ya kutenda mema sawasawa na neno lake.

Ni muhimu kufahamu ya kwamba kusudi la Mungu kumuumba mwanadamu ni ili aishi kama neno lake linavyosema. Ndio maana neno la Mungu linasema katika waefeso, “Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.” Waefeso 2:10. Pia Yesu wakati akifundisha  alidhihirisha wazi ya kwamba mtu anaweza kufanya mema au mabaya. Kwa sababu hiyo anaonesha ya kwamba  mwanadamu anayo hiari ya kuamua katika mambo ya Mungu. “Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri; au ufanyeni mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana.” Mathayo 12:33. “Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana; baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, niwaagizayo leo; na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya BWANA, Mungu wenu, mkikengeuka katika njia niwaagizayo leo, kwa kuandama miungu mingine msiyoijua.” Kumbukumbu la Torati 11:26-28.

Kwa kuwa mwanadamu anayo hiari na maamuzi shetani hana mamlaka juu yake kumlazimisha kufanya dhambi. Ninasema hivyo kwa sababu shetani kazi yake yeye ni kujaribu mtu na kumshawishi ili afanye dhambi. Kuna njia ambazo mtu anaweza kujaribiwa ni kama ifuatavyo;

1. Tunaweza kuona njia ya kwanza ambayo mtu anaweza kujaribiwa ni kupitia Shetani. Hawa alijaribiwa na Shetani naye  aliposhawishika alikula matunda aliyokatazwa na Mungu asile. Alikuwa amedanganywa na Shetani ili amkosee Mungu. “BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.” Mwanzo 2:16-17. “Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa.” Mwanzo 3:4.

2. Mtu hujaribiwa mwenyewe kwa yale anayoyatamani. Hapa nitatoa mifano ili uweze kuelewa. Ikiwa kuna mtu anatamani kuwa na gari, nyumba ya kisasa, simu ya mkononi. Lakini hana fedha za kununulia vitu hivyo. Kwa sababu ya tamaa zake akashawishika moyoni mwake na kuamua kuvipata kwa njia za wizi, dhuluma, na unyang’anyi, anakuwa amejaribiwa na tamaa zake mwenyewe. “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.” Yakobo 1:14.

3. Pia mtu apotamani kufanya  mambo yoyote ambayo ni kinyume na neno la Mungu Shetani anaweza kumwingia na  kumshawishi ili afanye haraka na kumkosea Mungu. Tuaweza kuona alivyofanya kwa Yuda Iskariote. “Shetani akamwingia Yuda, aitwaye Iskariote, naye ni mmoja wa wale Thenashara. Akaondoka, akaenda akasema na wakuu wa makuhani na majemadari, jinsi atakavyoweza kumtia mikononi mwao.” Luka 22:3-4. 

Kutokana na somo hili unaweza kuona wazi ya kwamba Shetani hahusiki kwa kila jambo. Kwa sababu hiyo kuna mambo ambayo Mwanadamu anafanya kwa Upumbavu na uzembe, hapa Shetani hahusiki. Kuendelea kujifunza zaidi bofya hapa; Kuepuka dhambi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...