Ili tuweze kufahamu maana ya rafiki wa kweli kati ya mtu na mwenzake, ni vizuri tukaangalia neno la Mungu linavyosema. Mungu wetu ndiye rafiki wa kweli kwa sababu yeye ndiye aliyetupenda kwanza. Tulipokuwa ni wenye dhambi, kwanza yeye alitupenda sisi watu ambao tulikuwa hatustahili mbele zake, kwa sababu yeye ni mtakatifu. Kwa upendo wake alimtoa na kumtuma mwanawe. Kupitia yeye sisi tulio na dhambi tuokolewe na kuishi katika upendo wa kweli wa Mungu. Kwa hiyo, inatupasa sisi kuishi katika urafiki wa kweli kati ya mtu na mwenzake. “Kwa maana jinsi Mungu alipenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee... hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye”. ( Yohana 3:16,17 ).
Jambo la muhimu.
Ni vizuri kufahamu ya kwamba marafiki wa aina mbili:
1.Rafiki wa kweli wakati wote.
Huyu ni rafiki anayependa kuwa na uhusiano wa karibu kati yako na wewe wakati wote. Wakati wa shida hakuachi wala kukuepuka. Huyu haangalii hali yako ya maisha kwamba wewe ni masikini au ni tajiri. Rafiki wa namna hii, huyo ndiye rafiki mwenye upendo wa kweli.
2.Rafiki ambaye siyo wa kweli.
Rafiki wa namna hii anapenda kuwa na uhusiano na wewe kwa sababu ya vitu kama fedha, mali au cheo. Huonyesha kuwa na urafiki na wewe wakati ambao anahitaji kupata msaada au kitu chochote kutoka kwako. Lakini atakapofahumu ya kuwa huna anachokihitaji kama vile fedha, mali na cheo, bali ni mtu mwenye shida hawezi kuendelea kuwa na urafiki na wewe. Kwa sababu hiyo anakuacha na kukuepuka kabisa. Rafiki wa namna hii a maonyesho wazi ya kwamba hakuwa na upendo wa kweli kwa ajili yako. Bali alikuwa anapenda vitu alivyokuwa anatarajia kupata kwako
Fuatilia somo lingine kwa kubofya hapa upate kufahamu; RAFIKI WA KWELI WA MUNGU
Maoni
Chapisha Maoni