Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUOMBA NA KUFUNDISHA KWA NAMNA INAYOFAA.

Ni muhimu kwa kila mtu aliyeokoka kufahamu ya kwamba  kanuni  na utaratibu unaotakiwa kufuatwa wakati  wa kuomba.  Ndio maana Yesu alifundisha namna inayofaa  kufuatwa na kufahamu wakati  wa  kuomba. Akasema “Tena msalipo, msiwe wanafiki, kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagagi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe usalipo ingia katika chumba cha ndani na ukiisha kufunga mlango wako, usalipo mbele ya Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi. Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke- payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi. Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua unayohitaji kabla ninyi hamjamwomba”. (Mathayo 6:5-7).Katika maandiko haya unaweza kuona namna Yesu alivyofundisha kwa kuwaonya wanafunzi wake.

Vilevile katika mafundisho hayo yanawahusu  pia wale ambao wamekwisha kuokoka na  kufanyika kuwa wanafunzi wa Yesu. Wakati wa kuomba inapasa mwamini  kuepuka unafiki au kujionyesha ili  kujulikana na watu  wakati wa kuomba .  Mafundisho haya yanahusu pia  mambo ya maisha yetu mbalimbali.  Kwa mfano, ikiwa mtu  anataka  kununua gari  na moyoni mwake anataka kujionyesha mbele za watu  ili ajulikane ya kwamba amenunua gari. Kwa kufanya hivyo atakuwa amejivuna na kujitukuza. Afanyaye hayo ni sawa na kutenda dhambi na  ni machukizo mbele za Mungu. Kwa sababu hiyo Mungu hatayasikiliza maombi yake. 

Neno  kupayuka- payuka maana yake ni:
Kusema maneno yasiyofaa   ambayo ni ya upumbavu na kupaza sauti kwa namna isiyofaa.  Mfano ikiwa mtu yuko mbali na mwenzake na anamwita kwa kupaza sauti,  kufanya hivyo ni njia mojawapo ya kupayuka.

Kutokana na mfano huo,  kuna umuhimu wa kila mtu kuwa na busara wakati anapomwomba Mungu. Iwapo mtu yupo nyumbani kwake yampasa aombe bila  kupayuka-payuka ili asiwasumbue wenzake (majirani).

Mtu binafsi anapofanya maombi ni muhimu kufanya maombi ya siri yeye  na Mungu wake, si vyema kujulikana na kila mtu ya kwamba anamwomba Mungu.

Mfano mwingine ikiwa mtu wa Mungu ameenda hospitalini   kuwaona wagonjwa na kufanya huduma  ya kuwambea,  aombe  bila kupayuka. Kwa kufanya hivyo  atakuwa amefanya maombi kwa busara bila kuwasumbua wagonjwa.

Kuhusu  kuhubiri na kufundisha. Wakati wa kufanya mambo haya inapasa kufanya kwa umakini kwa ajili ya faida ya kanisa.  Yapo mambo muhimu ya kuzingatia ambayo ni:

1.Anayehubiri au kufundisha ni muhimu kuhakikisha  anafanya  huduma kwa  kuongea kwa sauti ya wastani  ambayo itasikika vizuri kwa wanaomsikiliza yaani  kanisa. Ikiwa sauti ni kubwa kupita kiasi inakuwa kelele na usumbufu kwa washirika. Na si hivyo tu hawawezi kusikia vizuri anachosema.

2. Jambo lingine la muhimu siyo vema kuweka kipasa sauti karibu sana na mdomo, kwa kufanya hivyo  sauti itakuwa ya kukoroma na kutokusikika vizuri.

3. Kuhubiri na kufundisha kwa kusema haraka haraka,  husababisha baadhi ya washirika kukosa  kusikia vizuri na kuelewa. Kwa kufanya hivyo inakuwa ni sawa na kupayuka.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...