Mkristo aliyeokoka ni muhimu kuthibitisha kama yeye ni mtakatifu. Kwa sababu Sifa ya Mungu yeye ni Mtakatifu, naye anataka tuwe watakatifu kama yeye alivyo. Ndio maana Mungu amesema; "...Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi Bwana, Mungu wenu, ni mtakatifu."(Law 19:2). Yampasa mtu kuchunguza moyoni mwake ili aweze kufahamu ya kwamba je! Yeye ni mtakatifu? Jinsi ya kuthibitisha na kuwa na uhakika ni kama ifuatavyo;
1. Anaishi sawasawa neno la Mungu linavyosema. Hatawaliwi na dhambi katika maisha yake, kwa sababu emeweka nia moyoni mwake kutenda yaliyo ya haki. kwa sababu hiyo dhambi haina nguvu wala haiwezi kumtawala katika maisha yake kwa kuwa amekufa katika mambo ya dhambi. Ndipo katika maisha yake andiko hili lifuatalo litatimia kwake; "Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi... lakini kwa kule kuishi kwake, amwishi Mungu. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu." (Rum 6:10-11). "Yeye mwenyewe alizichukua dhaambi zetu katika mwili wake juu ya mti, ili, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki..." (1Pet (2:24).
2. Moyoni anayo amani na utulivu kwa kuwa hakutenda dhambi, wala hana hila ndani yake. Kwa sababu hiyo hakuna hukumu katika moyo wake. "Wapemzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu." (1Yoh 3:20-21). Heri Bwana asiyemhesabia upotovu, ambaye rohoni mwake hamna hila. (Zab 32:2).
3. Anatunza utakatifu katika maisha yake. Ni pale mtu anapoweka nia moyoni hatatenda dhambi na kudumu kwa kutenda sawasawa na neno la Mungu linavyosema. Na ndio maana imeandikwa; "Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi." (1Yoh 5:18).
4. Anakuwa na amani moyoni na watu wote. Hili ni jambo la muhimu katika maisha ya mkristo aliyeokoka kuwa na amani na watu wote. Ikiwa mtu hana amani na watu wote hatakuwa na utakatifu. "Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu akayemwona Bwana asipokuwa nao; mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo." (Ebr 12:14, 15).
1. Anaishi sawasawa neno la Mungu linavyosema. Hatawaliwi na dhambi katika maisha yake, kwa sababu emeweka nia moyoni mwake kutenda yaliyo ya haki. kwa sababu hiyo dhambi haina nguvu wala haiwezi kumtawala katika maisha yake kwa kuwa amekufa katika mambo ya dhambi. Ndipo katika maisha yake andiko hili lifuatalo litatimia kwake; "Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi... lakini kwa kule kuishi kwake, amwishi Mungu. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu." (Rum 6:10-11). "Yeye mwenyewe alizichukua dhaambi zetu katika mwili wake juu ya mti, ili, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki..." (1Pet (2:24).
2. Moyoni anayo amani na utulivu kwa kuwa hakutenda dhambi, wala hana hila ndani yake. Kwa sababu hiyo hakuna hukumu katika moyo wake. "Wapemzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu." (1Yoh 3:20-21). Heri Bwana asiyemhesabia upotovu, ambaye rohoni mwake hamna hila. (Zab 32:2).
3. Anatunza utakatifu katika maisha yake. Ni pale mtu anapoweka nia moyoni hatatenda dhambi na kudumu kwa kutenda sawasawa na neno la Mungu linavyosema. Na ndio maana imeandikwa; "Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi." (1Yoh 5:18).
4. Anakuwa na amani moyoni na watu wote. Hili ni jambo la muhimu katika maisha ya mkristo aliyeokoka kuwa na amani na watu wote. Ikiwa mtu hana amani na watu wote hatakuwa na utakatifu. "Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu akayemwona Bwana asipokuwa nao; mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo." (Ebr 12:14, 15).
Maoni
Chapisha Maoni