Karibu katika somo mbalo linakuhusu wewe kuwa na umoja na Mungu na Yesu Kristo. Umoja ninaofundisha katika somo hili ni ule unaotokana na mtu aliyemwamini Yesu na kuokolewa, na kuamua kuishi sawasawa na maneno ya Mungu yasemavyo. Mtu kama huyo anakuwa ni mtakatifu kama Mungu alivyo mtakatifu. Ndio maana Yesu akasema. "Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake." (Yoh 14:23). "Lakini yeye alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake." (1Yoh 2:5)
Wale walio watakatifu ndio ambao Mungu amewapa haki ya kuwa na umoja na yeye. Ndio maana imeandikwa, "Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia. Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu..." (Yoh 15:3-4). Tunaweza kuona Bwana wetu Yesu Kristo alivyomwomba Mungu kwa ajili yao watakaomwamini ili wawe na umoja na yeye na Baba. "Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao. Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu usadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma." (Yoh 17:20-21).
Kuna umuhimu ambao ni jambo la msingi, Mwamini kukamilishwa katika umoja na Mungu. Anakamilishwa kwa kuishi sawasawa na neno la Mungu linavyosema, na pia Baba na Mwana wanapofanya makao ndani yake. Ndio maana Yesu akasema alipokuwa akiomba, "Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi." (Yoh 17:23).
Vilevile tunapaswa kuwa na umoja sisi kwa sisi ambao Yesu alipokuwa akiomba mbele za Mungu alisema hivi; "Nami utukufu ule nimewapa wao; ili wao wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja." (Yoh 17:22 ). Huo ndio umoja wa kweli ambao Mungu alikusudia tuwe nao. Kwa sababu hiyo tunaweza kuona ni mpango wa Mungu kuweka kanuni ili wale wote wanaomtii katika neno lake waishi katika umoja, kati yao na yeye.
Kuwa na umoja na Mungu kuna faida zaidi ya tunavyoweza kufahamu, lakini Yesu ametuahidi ya kuwa aliye umoja naye akiombacho chochote atafanyiwa. "Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa" (Yoh 15:7).
Wale walio watakatifu ndio ambao Mungu amewapa haki ya kuwa na umoja na yeye. Ndio maana imeandikwa, "Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia. Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu..." (Yoh 15:3-4). Tunaweza kuona Bwana wetu Yesu Kristo alivyomwomba Mungu kwa ajili yao watakaomwamini ili wawe na umoja na yeye na Baba. "Wala si hao tu ninaowaombea; lakini na wale watakaoniamini kwa sababu ya neno lao. Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu usadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma." (Yoh 17:20-21).
Kuna umuhimu ambao ni jambo la msingi, Mwamini kukamilishwa katika umoja na Mungu. Anakamilishwa kwa kuishi sawasawa na neno la Mungu linavyosema, na pia Baba na Mwana wanapofanya makao ndani yake. Ndio maana Yesu akasema alipokuwa akiomba, "Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi." (Yoh 17:23).
Vilevile tunapaswa kuwa na umoja sisi kwa sisi ambao Yesu alipokuwa akiomba mbele za Mungu alisema hivi; "Nami utukufu ule nimewapa wao; ili wao wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja." (Yoh 17:22 ). Huo ndio umoja wa kweli ambao Mungu alikusudia tuwe nao. Kwa sababu hiyo tunaweza kuona ni mpango wa Mungu kuweka kanuni ili wale wote wanaomtii katika neno lake waishi katika umoja, kati yao na yeye.
Kuwa na umoja na Mungu kuna faida zaidi ya tunavyoweza kufahamu, lakini Yesu ametuahidi ya kuwa aliye umoja naye akiombacho chochote atafanyiwa. "Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa" (Yoh 15:7).
Barikiwa
JibuFuta