Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUOMBA NA KUABUDU KATIKA ROHO MTAKATIFU.


Hapa tutaangalia mtu ambaye anaweza kuwa na uwezo wa kuomba na kuabudu katika Roho Mtakatifu ni Mkristo ambaye ameokoka na kumtii Mungu kwa kuishi sawasawa na neno lake. Na ndipo  anajazwa Roho Mtakatifu, naye Roho atajidhihirisha kwake kama ifuayavyo;

1. Atasikia au kuhisi nguvu ndani yake anapokuja Roho Mtakatifu juu yake. Tunaweza kuona kwa uthibitisho wa maandiko haya yafuatayo, "Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu..." Matendo 1:8. Katika andiko tunaweza kuona mtumishi wa Mungu Daudi alipotiwa mafuta na nabii Samweli kuwa Mfalme wa Israel. Roho Mtakatifu alikuja juu yake kwa nguvu. "Ndipo Samweli akaitoa pembe yake ya mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na Roho ya Bwana ikamjia Daudi kwa nguvu tangu siku ile." 1Samweli16:13.

2. Ataongozwa na Roho Mtakatifu kunena kwa lugha mpya ambayo hajawahi kuisikia wala kufundishwa. "Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka." Matendo 2:4.

Ni jambo la muhimu na inatupasa kuomba katika uwepo wa Roho Mtakatifu. Na ndiyo maana Mitume walifundisha na kuonyesha umuhimu wa kuomba katika Roho. "Kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho..." Waefeso 6:18. "Bali ninyi, wapenzi, mkijijenga juu ya imani yenu iliyo takatifu sana, na kuomba katika Roho Mtakatifu." Yuda 1:20.

Pia ni dhahiri kutokana hili fundisho hapa juu, vilevile ni jambo la muhimu kumsifu na kumwimbia Bwana katika Roho Mtakatifu. Na si hivyo tu, pia unaweza kumshukuru Mungu katika Roho Mtakatifu. Yesu alipowatuma wale wanafunzi wake kuihubiri habari njema waliporudi wakampa taarifa ya kwamba  waliwatoa  pepo juu ya watu waliokuwa wamepagawa nao walitii. Ndipo Yesu alimshukuru Mungu katika Roho Mtskatifu. "Saa ile ile alishangilia kwa Roho Mtakatifu, akasema, nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili, umewafunulia waatoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza." Luka 10:21.

Ninayo furaha kuu ndani yangu kwa kuwa ninaye Roho Mtakatifu, naye hububujika kutoka ndani yangu kama maji yanayobubujika katika chemichemi isiyokoma. Na ashukuriwe Mungu wa utukufu wote milele na milele. Amina. Ikiwa umemwishia Mungu kwa kujitolea kwake kama sadaka iliyoteketezwa madhabahuni  pa Mungu, ndipo utauona utukufu wa Mungu ukishuka juu yako kwa nguvu na Roho Mtakatifu  akibubujika kutoka ndani yako. Haleluya! Ni jambo la kufurahisha sana. Ndio maana imeandikwa; "...Yesu akasimama akapasa sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe, aniaminiye mimi, kama maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake. Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye..." Yohana 7:37-39.

Wakati ambao mtu anaweza kububujika katika Roho ni kama ifuatavyo;  Ni pale mkirsto anapoabudu, kusifu, kuimba. Na Kuomba. Lakini kububujika kwa Roho hutokea ndani ya mtu ikiwa anazingatia kanuni aliyoiweka Mungu ambayo Yesu aliifundisha akisema; " saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo wamwabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa 
Kumwabudu katika roho na kweli" Yohana 4:23-24.

Hapa nitaelezea jinsi mtu anavyomwabudu Mungu kwa roho na kweli ni kama ifuatavyo. Ni pale mtu anapodumu kwa kuishi sawasawa na neno la Mungu lisemavyo. Maana ya neno kweli ni neno la Mungu.

Ibada yetu ili ikubalike kwa Mungu na kumpendeza yatupasa kuitoa miili yetu kuwa viungo vya haki kwa Mungu.
"...Itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msifuatishe namna ya dumia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapeni ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu." Warumi 12:1-2. " Basi dhambi isitawale ndani ya miili yenu ipatikanayo na mauti, hata mkazitii tamaa Zake; wala msiendelee kuvitoa viungo veynu kuwa silaha za dhuluma kwa dhambi; bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama walio hai baada ya kufa, na viungo vyenu kwa Mungu kuwa silaha za haki." Warumi 6:13.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...