Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUWEKWA HURU KUTOKA DHAMBI YA UZINZI NA UASHARATI.

Jambo la kwanza ninamshukuru Mungu kwa neema yake aliyonipa kufundisha neno lake. Ndungu mpendwa ninajua ya kwamba Mungu alikupenda sana, hata akamtoa Mwana wake wa pekee Yesu Kristo kwa ajili yako ili akukomboe kutoka katika dhambi zote ikiwemo dhambi ya uzinzi na uasherati. Sasa ninakusihi kwa neema ya Mungu fuatana nami kwa makini kuhusu  somo hili nawe utauna utukufu wa Mungu katika maisha yako.

Tunaweza kuangalia kwa makini dhambi ya uzinzi na uasharati ambayo mtu akiitenda inaharibu ufahamu wake na hatimaye kuangamia. Mtu anapoteza uhusiano wake na Mungu, mawasiliano kati yake na Mungu yanakatika. Mungu  ni Makatifu hana ushirika na wenye dhambi. “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.” Mithali 6:26.  “Lakini maovu yenu yamewafarikisha (yamewatenganisha) ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki  kusikia.”  Isahau 59:2.

Atendaye dhambi ya zinaa au  uasherati  kamwe hawezi kupata utoshelevu (kuridhika au kutosheka) kwa sababu tendo hilo ni kinyume na sheria ya Mungu na limelaaniwa. Ndiyo maana imeandikwa;  “...wala hamtazitimiza kamwe  tamaa za mwili.”  Wagalatia 5:16.  Mtu akishanaswa katika dhambi hiyo asipotubu hawezi  kuwa huru katika maisha yake, bali atakuwa anateseka kwa kutumikishwa katika  dhambi hiyo. Bali mtu akiwekwa huru anakuwa na amani na furaha.
Ndugu mpedwa ninaamini ya kwamba kutokana na andiko hili hapa juu  linaonyesha wazi ya kwamba mtu hawezi kupata utoshelevu katika zinaa. Kwa sababu hiyo mtu anaweza  kupata utoshelevu kwa mkewe au kwa mumewe wa halali.

Kwa wale waliokoka au kuzaliwa mara ya pili.
Wakati mtu alipookoka alimaanisha kutubu dhambi zake zote na kuziacha,   ndipo Mungu alimsamehe sawasawa na ilivyoandikwa; “...Aziungamaye dhambi zake na kuziacha  atapata rehema (atasamehewa). Mithali 28:13.  Kwa yule ambaye  amekwisha okoka amewekwa huru mbali  na dhambi, hatumikii dhambi. “...Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi. Basi Mwana  akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.”  Yohanan 8:34,36. “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya.”  2Wakorintho 5:17.Hawezi kutenda dhambi ikiwa atazingatia kuishi sawasawa na neno la Mungu linavyosema.

Jambo ambalo yakupasa kufanya ni kujilinda na kuepuka  vishawishi ambavyo vinaweza kukusababishia utende dhambi.  Pia unapaswa kuwa na kiasi pamoja na kujiwekea mipaka kwa mtu ambaye siyo mkeo au mume katika mahusiano.  Mahusiano ninayosema ni yale ambayo yanaweza kuwa ya kikazi kama biashara, kilimo, kazi za ofisini, masomo na nyinginezo. Mkristo aliyeokoka na kusimama imara katika neno la Mungu hatakuwa na tamaa ya mwili kwa sababu amekwisha sulubishwa na Kristo ili asitende dhambi. “Tukijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena.” Warumi 6:6. Mstari huu unaonya au kukataza mtu aliyekwishaokoka asitende tena dhambi. Kwa hiyo ni muhimu kuzingatia maarifa ya neno la Mungu ambalo litakuongoza. Neno litakusaidi kujua jinsi ya kuishi kwa utaratibu ili usije ukavutwa na tamaa za kila namna, mojawapo ikiwemo tamaa ya mwili.   

Dhambi inavyoanza ndani ya mtu.
Dhambi yoyote huanza ndani ya moyo wa mtu anapoanza kuwaza mawazo mabaya katika moyo wake.  Ni vyema kutambua kuwa unapowaza mawazo mabaya unakuwa umetenda dhambi. Ikiwa mtu akimwona mtu asiyekuwa  mkewe au mumewe na akamtamani moyoni mwake, huyo amekwisha kuzini. Ndiyo maana Yesu alifundisha akisema; “Mmesikia kwamba  imenenwa, usizini; Lakini mimi nawaambia, mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.”  Mathayo 25:27-28.

Mambo ambayo unapaswa kuzingatia ili uweze  kushinda dhambi.
Sehemu hii nitafundisha jinsi ya kushinda na kuishi katika furaha ya wokovu.  Yafuatayo ni  mambo ya kuepuka ambayo yana ushawishi kwa mwanaume na mwanamke:

1. Kutokuangalia picha kwenye mtandao ambazo zinaonyesha wanaume na wanawake wakikutana kimwili. Vilevile kuepuka kusoma magazeti au vitabu vyenye mambo machafu yanayohusiana na zinaa.

2. Kutokufanya mizaha kati ya mwanaume na mwanamke. Hapa nitatoa kisa  ambacho nilikiona siku moja. Siku hiyo nilimwona mwanaume mmoja akimwambia mke wa mtu mwingine unapendeza. Kufanya hivyo ni jambo baya kwa sababu huyo si mke wake. Kisa hiki kinaonyesha kwa uhalisi ni mojawapo ya mzaha. Kila mtu ana uhalali mbele za Mungu ikiwa anavutiwa na mkewe au mumewe na kumwambia unapendeza au ninakupenda. Hata hivyo kitendo hiki kinatakiwa kifanyike pale ambapo wako peke yao na haya ndio maadili. Yakupasa ujue mambo yanayofaa kumwambia au kumfanyia mkeo au mumeo mnapokuwa mbele za watu.   

3. Kuulinda moyo wako ili usiyaruhusu mawazo mabaya kuingia. Ni muhimu kutambua ya kuwa dhambi yoyote inaanzia moyoni kwa kuwaza. Yakupasa kuamua kuutawala moyo wako na kutambua lipi linafaa kuwaza na lipi halifai na kuliacha. Haiwezekani usilolitaka kuwaza likapata nafasi na kukaa katika moyo wako. Wewe mwenyewe ndiye mwenye uwezo wa kuruhusu wazo lolote liwe jema au baya. Ndiyo maana imeandikwa; “Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri; au ufanyeni mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya... Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya.” Mathayo 12:33, 35. Utakapoulinda moyo wako usiwaze mabaya unaweza kuutawala mwili. “Kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili  (kuutawala mwili)  wake katika utakatifu na heshi huu n jihadharima. Si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu. Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.”  1Wthesalonike 4:4-5, 7.

Kama ulianguka katika dhambi.
Baada ya wewe kulisoma somo hili sasa ni wakati ambao Mungu amekujalia ili uweze kumgeukia. Yeye  ni mwaminifu atakusamehe na kukuweka huru kutoka katika dhambi. Yafuatayo ni mambo yakupasayo  kufanya:
1. Weka nia moyoni na kuamua kuacha kufanya dhambi.

2. Ungama mbele za Mungu kwa kukiri makosa uliyoyafanya na yale yaliyofichika ili akusamehe.

3. Weka  nia mbele za Mungu ya kwamba  kuanzia sasa hutaki kufanya tena dhambi, bali utadumu katika sheria zake.

4. Mshukuru Mungu kwa wema wake  amekusamehe, na pia kwa sababu alikujalia  kuwa hai kwa uvumilivu wake hadi leo hata ukatubu.  Kuna wengine wamekufa katika dhambi  bila  kuzitubia, lakini wewe haukuwa mwema kuliko wao.

5. Omba kila siku na wakati mwingine funga ili uweze kusimama imara katika neno la  Mungu. “Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; lakini roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.” Mathayo 26:41.  Andiko hili linadhihirisha wazi ya kwamba mtu akikesha (akidumu) katika kuomba hawezi kutenda dhambi. Ndiyo maana andiko hili  linaonyesha kuwa kuna kujaribiwa lakini yule mtu ambaye anaomba hataingi katika majaribu. lakini  kwa mtu yule ambaye haombi  akijaribiwa na yule mwovu ni rahisi kutenda dhambi.

6. Vunja uhusiano na yule mwanamke au mwanaume uliyeanguka naye katika dhambi ya uzinzi.

7. Vunja mazoea yaliyopitiliza ambayo si ya kawaida uliyokuwa nayo kwa mtu ambaye si mkeo au mumeo.

8. Jihadhari na kuepuka wale wote ambao unajua wanaweza kukushawishi ili ufanye nao dhambi ya uzinzi.

Kwa kuzingatia hatua hizo unageuzwa na kuwa mtu mpya katika utakatifu. Nawe utauona uzuri wa Mungu ulivyo mkuu ndani yako kuliko mambo ya mwili. Kwa neema ya Mungu na Yesu Kristo hakika utazidi kuuona utukufu wa Mungu, ukuu wake, nguvu zake na wema wake usiopimika kwa mwanadamu.

Usipozingatia kanuni ambazo nimefundisha utashindwa na kuanguka katika dhambi mara kwa mara. Udanganyifu wa shetani utaingia ndani ya moyo wako ya kwamba haiwezekani kuishi bila kufanya dhambi. Kwa wale ambao wamezingatia sheria na kanuni ya neno la Mungu dhambi haina nafasi ndani yao. Wamewekwa huru hawatawaliwi tena na dhambi.

Sasa ninamwomba Mungu Baba kwa ajili yako ikiwa umenaswa kwenye dhambi yoyote, Mungu akujalie uwezo wa kushinda na kudumu katika mapenzi yake.  Ni kwa jina la Yesu
Kristo ninaomba na
 kumshukuru Mungu, Amen.

Maoni

  1. Asante kwa Neno zuri. Mungu akubariki

    JibuFuta
  2. Ahsante sana mtumishi wa Mungu.

    JibuFuta
  3. Mungu akubariki sana nimepata vitu vya kunitoa sehemu moja nakunipeleka sehemu nyingine

    JibuFuta
  4. Neno zuri sana, ubarikiwe mtumishi wa bwana.

    JibuFuta
  5. nimesoma mwaka 2018 lakini ujumbe huu umekua baraka sana!! maana umenijenga sana. namshukuru Mungu nimepata kitu. Mungu akubariki sana.

    JibuFuta
  6. Asante Mungu akubariki

    JibuFuta
  7. Asante sana Mtu wa Mungu, tuzidi kuombeana maana hii dhambi ya uzinzi imekisiri sana upande wangu.

    JibuFuta
  8. mtumishi wa mungu ubarikiwe sana kiukweli nimekuwa nikitenda dhambi hii kwa takribani miaka yote niliyo nayo tangia kujifahamu nakingine zaidi huwa naumia sana ninapomaliza kufanya tendo kwa ninafahamu fikra kwamba nimemkosea mungu wangu daah mtumishi yani umenigusa mimi moja kwa moja .

    JibuFuta
  9. Ubarikiwe sana munishi wa MUNGU

    JibuFuta
  10. Somo zuri sana na Mungu anisaidie niwe huru kweli kweli, Amen

    JibuFuta
  11. Bwana akubariki.

    JibuFuta
  12. Asante mtumishi wa MUNGU nayapokea mafundisho yako kwa jina la yesu kristo bwana wangu AMINA

    JibuFuta
  13. Ujumbe umenigusa sana,naomba Mungu anisaidie sana.

    JibuFuta
  14. Mungu akubariki sana sana nimepata kitu hapa

    JibuFuta
  15. Bila jina20:00

    Asante Sana mtumishi wa MUNGU, nimeguswa na SOMO hili moja kwa moja, Mungu anisaidie niweze kuyashika mafundisho haya

    JibuFuta
  16. Bila jina20:39

    Amen SoMo nzuri

    JibuFuta
  17. Bila jina13:05

    Amina napata nguvu

    JibuFuta
  18. Bila jina13:10

    Ubarikiwe mtumishi wa Mungu

    JibuFuta
  19. Bila jina01:50

    Nimebarikiwa sana mtumishi

    JibuFuta
  20. Bila jina22:05

    mungu aendelee kukujaza roho mtakatifu katika kufanya kazi yake na kuokoa roho za watoto wa mungu amina.

    JibuFuta
  21. Bila jina18:51

    I blessed with article. God bless you and keep going

    JibuFuta
  22. Bila jina07:06

    Amina mtumishi wa Mungu. Ubarikiwe kbs uzidishiwe tumefundishika kbs

    JibuFuta
  23. Bila jina18:47

    Asante sanaa

    JibuFuta
  24. Bila jina12:38

    Nimeguswa sana na somo hili. Ninakiri nimekuwa natenda dhambi hii baada ya kusalitiwa na mwenzangu wa ndoa. Tukio lile lilinivunja moyo na kuona sina thamani ndipo nikaanguka na sikuweza kujinasua. Namshukuru Mungu kwa somo kwani baada ya kutenda nilipoteza tumaini la kusamehewa na Mungu lakn kwa somo hili limenipa tumaini mpya. Nimetambua kuwa sikuwa imara na hasira ya kusalitiwa ilinipeleka kwenye dhambi ileile niliyoichukia ilipotendwa na mwenzangu... Mungu namwomba anisamehe na ninataka kusimama tena bila kujali matendo au moni ya wengine. Uendelee kutupa maarifa haya ya rohoni.

    JibuFuta
  25. Bila jina01:00

    Asante sana mtumishi

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...

UPONYAJI WA MAGONJWA.

Chanzo cha magonjwa. Kuna magonjwa yanayotokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya yule mtu ambaye aliyekuwa mngonjwa akamwabia,   “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi”   Yn 5:14.   Ikiwa mtu aliyeokoka akirudia kuishi maisha ya dhambi pepo mchafu anapoona nafasi anachukua pepo wengine na kuingia kwake. Yesu alisema,  “Mara huenda akachukua pamoja naye    pepo    wengine walio waovu    kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”   Mt 12:45.    Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili. Kwa upande mwingine mtu anaweza akawa ni mgonjwa au amekosa lishe.  Uponyaji wa Mungu.                     Mambo ya kuzingatia na kuponywa ni ha...

KUDUMU KATIKA UPENDO WA MUNGU.

Neno la Mungu katika Biblia linatufudisha kuhusu upendo wa Mungu  kwetu. Yeye Mungu ndiye  mwanzo wa upendo kwa sababu alitupenda kwanza. “...alitupenda sisi kwanza”.   1 Yohana 4:19. Jinsi mtu anavyoweza kuwa na upendo wa Mungu. Ni pale mtu anapokuwa amezingatia kudumu katika upendo wa Mungu kama ifuatavyo; 1.Kuishi sawasawa na maagizo yote ya neno la Mungu na kumpenda. “Na sasa, Israeli, BWANA, Mungu wako, anataka nini kwako, ila umche BWANA, Mungu wako, na kwenda katika njia zake zote, na kumpenda, na kumtumikia BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote;”   Kumbukumbu la Torati 10:12.   “Lakini mjibidiishe sana kuzifanya amri na sheria, ambazo Musa, mtumishi wa BWANA, aliwaamuru, kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kwenenda katika njia zake zote, na kuzishika amri zake, na kushikamana na yeye, na kumtumikia kwa moyo wenu wote na nafsi yenu yote”.   Yoshua 22:5. 2. Jambo lingine la kuzingatia ni kwamba yampasa mtu kuyashika maagiz...

MADHARA YA DHAMBI.

Huu ni wakati mwingine ambao Bwana amenijalia kuwepo kwa kusudi lake jema. Nitaelezea katika somo hili kuhusu dhambi ilivyo na madhara kwa mtu aitendaye. Kwanza tuangalie dhambi  ilivyoanza kwa Adamu na Hawa ni wakati walipokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambayo Mungu aliwakataza wasile. Kwa sababu hiyo dhambi ilisababisha madhara mengi kwa uzao wake na vizazi vyote duniani. Kwa hiyo shida zote zilizopo duniani zimetokana na dhambi. Kutokana na wazazi wetu wa kwanza Adamu na Hawa kwa kuwa walitenda dhambi na vizazi vingine vyote vimehesabiwa ni wenye dhambi. Mtu  anazaliwa akiwa na asili ya dhambi kutoka kwa wazazi wa kwanza Adamu na Hawa. Warumi 3:23 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;” Kutokana na sababu hiyo ndio maana kila mwanadamu anakufa sawasawa na Mungu  alivyosema katika kitabu cha Mwanzo 2:16-17 “BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa u...