Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TUNDA LA FURAHA.

Hili ni tunda la Roho ambalo ni muhimu kwa kila mkristo aliyeokoka kuwa nalo. Hii ni furaha inayotokana na Mungu mwenyewe. “....Kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi Ee Mungu wangu....” Zab 43:4. 

Aina za furaha
a. Furaha ya hapa duniani.  
Hii ni furaha ambayo mwanadamu  anakuwa nayo pale anapokuwa na nyumba nzuri, au gari, anafurahi. Anacho chakula cha kutosha na fedha, anafurahi.  Hiyo ni furaha ya hapa duniani ikiwa mtu anapata yale anayoyahitaji.

b. Furaha inayotokana na Mungu
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia ili mtu aweze kuwa na furaha inayotokana na Mungu.
1. Katika Roho Mtakatifu.  
Mkristo ambaye ameokoka na kujazwa Roho Mtakatifu anakuwa na furaha katika maisha yake. Ndio maana kila aliyeokoka akizingatia neno la Mungu linavyosema uso wake huonekana mkunjufu kutokana na furaha aliyonayo ndani yake. “ .... Mkiisha kulipokea neno pamoja na furaha ya Roho Mtakatifu”.  1The 1:6.

2. Kulijua neno la Mungu.
Hii ni furaha ipatikanayao kwa kujifunza,  kulipenda na kulitii neno la Mungu “Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, Ambayo nimeyapenda, ....Maagizo yako ni furaha yangu.” Zab 119:47, 143. “Upenda haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta,  Mafuta ya shangwe kupita wenzio.”Ebr 1:9.

3. Kufurahi katika dhiki.
Hapa duniani mtu anaweza kupitia katika shida mbalimbali ambazo katika hizo hujengwa na kuimarika katika Mungu, ikiwa anazingatia kumpenda  Mungu katika  neno lake. “....Tufurahi katika dhiki pia; tukijua yakuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi (uvumilivu); na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti nwa moyo ni tumaini, na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu aliyetupa sisi.”   Rum 5:4.%

Maoni