Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TUNDA LA FURAHA.

Hili ni tunda la Roho ambalo ni muhimu kwa kila mkristo aliyeokoka kuwa nalo. Hii ni furaha inayotokana na Mungu mwenyewe. “....Kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi Ee Mungu wangu....” Zab 43:4. 

Aina za furaha
a. Furaha ya hapa duniani.  
Hii ni furaha ambayo mwanadamu  anakuwa nayo pale anapokuwa na nyumba nzuri, au gari, anafurahi. Anacho chakula cha kutosha na fedha, anafurahi.  Hiyo ni furaha ya hapa duniani ikiwa mtu anapata yale anayoyahitaji.

b. Furaha inayotokana na Mungu
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia ili mtu aweze kuwa na furaha inayotokana na Mungu.
1. Katika Roho Mtakatifu.  
Mkristo ambaye ameokoka na kujazwa Roho Mtakatifu anakuwa na furaha katika maisha yake. Ndio maana kila aliyeokoka akizingatia neno la Mungu linavyosema uso wake huonekana mkunjufu kutokana na furaha aliyonayo ndani yake. “ .... Mkiisha kulipokea neno pamoja na furaha ya Roho Mtakatifu”.  1The 1:6.

2. Kulijua neno la Mungu.
Hii ni furaha ipatikanayao kwa kujifunza,  kulipenda na kulitii neno la Mungu “Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, Ambayo nimeyapenda, ....Maagizo yako ni furaha yangu.” Zab 119:47, 143. “Upenda haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta,  Mafuta ya shangwe kupita wenzio.”Ebr 1:9.

3. Kufurahi katika dhiki.
Hapa duniani mtu anaweza kupitia katika shida mbalimbali ambazo katika hizo hujengwa na kuimarika katika Mungu, ikiwa anazingatia kumpenda  Mungu katika  neno lake. “....Tufurahi katika dhiki pia; tukijua yakuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi (uvumilivu); na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti nwa moyo ni tumaini, na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu aliyetupa sisi.”   Rum 5:4.%

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...