Maana ya neno fadhili ni kusaidia.
Mungu yeye ni msaada kwa kila mtu anayemkimbilia ikiwa anampendeza. “Mhisani (mfadhili )wangu na boma
langu, Ngome yangu na mwokozi wangu, Ngao yangu niliyemkimbilia,....” Zab 144:2.
Kuwasaidia masikini ni jambo jema na
muhimu ambalo Yesu Kristo ameagiza, akisema, “....imewapasa
kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema
mwenyewe. Ni heri kutoa kuliko kupokea.” Mdo 20:35.
Yampasayo
anayesaidi masikini.
1. Asaidie kwa
moyo safi bila kusikitika na wala si kwa ajili ya kujionyesha. “....mwenye
kukirimu, kwa moyo mweupe....” Rum 12:8. “Kama akiwapo
masikini pamoja nawe, nduguzo mmojawapo, ndani ya malango yako.... Jitunze,
msiwe na neno lisilofaa moyoni mwako.... jicho lako likawa ovvu juu ya nduguyo
usimpe kitu; naye akamlilia Bwana juu yako, ikawa dhambi kwako.Mpe kwa kweli,
wala moyo wako usisikitike utakapompa; kwa kuwa atakubarikia Bwana, Mungu wako,
kwa neno hili katika kazi yako yote, na katika kila utakalotia mkono wako.Kwa
maana masikini hawatakoma katika nchi milele; ndipo ninakuamuru na kukuambia,
Mfumbulie kwa kweli mkono wako nduguyo, mhitaji wako, masikini wako, katika
nchi yako.” Kum
15:7,9,10.
Kinachotokeo
kwa mtu anayesaidia masikini.
1.Haki yake inadumu na wala haitapotea ikiwa anadumu katika sheria Mungu. “Amekirimu, na kuwapa masikini, Haki yake yakaa milele.” Zab 112:9.
2.Anabarikiwa. “Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; Maana huwapa masikini chakula chake.” Mit 22:9.
Maoni
Chapisha Maoni