Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TUNDA LA AMANI.

Hili ni tunda la Roho ambalo limethibitishwa katika maandiko ya kwamba Mungu ni wa amani na amani ya kweli inatoka kwake. “Sasa Bwana wa amani mwenyewe na awape amani daima kwa njia zote.” 2The 3:16. “....Na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo Bwan wetu.” 1Tim 1:2.

Kudumu katika amani.
Ili  kudumu katika amani yakupasa kuzingatia yafuatayo:
1. Kulipenda neno la Mungu na kulitii. “Wana amani nyingi waipendao sheria yako, Wala hawana la kuwakwaza.” Zab 119:165. “Mwanangu usiisahau sheria yangu, Bali moyo wako uzishike amri zangu. Maana zitakuongezea wingi wa siku, Na mika ya uzima na amani.” Mit 3:1-2.

2. Kuwapenda na kuishi kwa amani na watu na utakatifu. “Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote. Kama yamkini kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.” Rum 12:17-18. “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu , ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.”  Ebr 12:14-15.

3. Kuwasamehe wale waliokukosea na kuachilia makosa yao. Haupaswi kuyahifadhi na kuyakumbuka, bali uyasahau, huo ndio msamaha ulio mkamilifu. “Mimi, naam, mimi ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe; wala sitazikumbuka dhambi zako” Isa 43:25. Anayesamehe anajitendea wema. “Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake, Aliye mkali hujisumbua mwili wake.” Mit 11:17.

Maoni