Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TUNDA LA UPOLE.

Neno upole linaitwa kwa lugha ya kiyunani praytes. Kwa mkristo ambaye amemjua Mungu inampasa kufahamu ni jambo la msingi kuwa mpole. Upole hujengwa na Mkristo mwenyewe anapoudhiwa akivumilia na kusamehe. Katika maisha ya mkristo aliyesimama imara katika Mungu anakutana na maudhi mengi, lakini anayashinda kwa maombi. Hatimaye anakuwa na furaha na amani kama ilivyoandikwa; “Bali wenye upole....watajifurahisha kwa wingi wa imani.” Zab 37:11.
 Kutokana na mafundisho haya mkristo hatafadhaishwa na maudhi bali atakuwa na utulivu ndani ya moyo wako. Hatimaye atakuwa amesimama imara katika Kristo Yesu. Ndipo andiko lisemalo furahi na kushangilia litatimia kwake, nalo linasema; “Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo kwa ajili yangu. Furahini na kushangilia kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni....” Mt 5:11-12. 

Ili  uweze kudumu katika upole.
Yakupasa usiwe na hasira na ghadhabu uyasikiapo maneno ya kukuumiza , usiyaweke moyoni mwako bali uyapuuze na kuyaachilia wakati huo huo, ndipo utakuwa salama moyoni mwako, kwa sababu neno linasema, “Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.” Mit 15:1.

Unaposikia maneno yaumizayo, njia ni  kuyapuuza na kuyaachilia. Hapo  unakuwa umeepuka kukasirika na kuhamaki, ndio maana imeandikwa, “Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya kuhamaki hutukuza upumbavu.” Mit 14:29. “Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusem;, wala kukasirika; kwa maana hasira ya mwanadamu haitendi haki ya M ungu.” Yak 1:19-20. “Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa ; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu autekaye mji.” Mit 16:32.
  
Upole unavyojengwe.
Upole hujengwa na kupatikana kwa  njia ya kujifunza na kulishika neno la Mungu.  “Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu.” Mt 11:29.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...