Ruka hadi kwenye maudhui makuu

UPONYAJI WA MAGONJWA.


Chanzo cha magonjwa.
Kuna magonjwa yanayotokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya yule mtu ambaye aliyekuwa mngonjwa akamwabia, “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi” Yn 5:14. 

Ikiwa mtu aliyeokoka akirudia kuishi maisha ya dhambi pepo mchafu anapoona nafasi anachukua pepo wengine na kuingia kwake. Yesu alisema, “Mara huenda akachukua pamoja naye  pepo  wengine walio waovu  kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya” Mt 12:45.  

Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili. Kwa upande mwingine mtu anaweza akawa ni mgonjwa au amekosa lishe. 

Uponyaji wa Mungu.                    
Mambo ya kuzingatia na kuponywa ni haya yafuatayo;
1.kutubu na kuziacha dhambi.
Imeandikwa,
“Azifichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha on atapata rehema”  Mithali 28:13. Pia andiko linasema, “Twajua ya kwamba Mungu hawasikii wenye dhambi;bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake huyo humsikia” Yhana 9:31.

2. Kuishi maisha ya utakatifu
Ndio maana Mungu amesema; “Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako. Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote…” Kumb  7:12, 15. Katika maandiko haya tunaona Mungu alisema na baba zetu. Pia katika nyakati hizi anasema nasi katika ahadi ya maandiko  hayo yakwamba tunapozishika na kuzitenda hukumu zake (Sheria zake). Naye hutuondolea ugonjwa wote. Kwa sababu Mungu aliwaapia baba zetu ni ili kuthibitisha atafanya yale aliyoahidi. Kwa hiyo katika maisha yako yote yakupasa kumtegemea Mungu kwa yale yote aliyoahidi katika neno lake.

3.Kumwamini Mungu na neno lake. 
Ndiyo maana Mungu alisema “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita roho yangu haina furaha naye.” Ebr10:38. 
Kutokana na andiko hili, linaonyesha lazima mtu awe mwenye haki ndipo aweze kuishi kwa imani. Pia lazima kwanza kuamini moyoni na kuwa na uhakika Mungu atakuponya kama neno  linavyosema,“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana (wazi) ya mambo yasiyoonekana” Ebr 11:1                                                                      
Kwa sababu hiyo katika maisha yako yote yakupasa kumtegemea Mungu kwa yale yote aliyoahidi katika neno lake.
"Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote,…Mche Bwana, ukajiepushe na uovu, Itakuwa afya mwilini pako. Na mafuta mifupani mwako. Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzishike kauli zangu. Kwa maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote”Mit 3:5,7,8.                                                                  4. Kuishi maisha ya unyenyekevu.
“Dhabihu za Mungu ni mioyo iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka Ee Mungu hutaudharau. “Huwaponya waliopondeka moyo,  Na kuwaganga jeraha zao” Zab 51:17; 147:3. Mungu anahitaji watu waliovunjika na kupondeka moyo ili awaponye. Maana ya kuvunjika na kupondeka moyo ni kunyenyekea chini ya Mungu na kujua yeye  ni mwenye uwezo na nguvu zote. Pia kunyenyekea ni kuacha kuwa na kiburi na kujiona wewe ni bora kuliko wengine, kutokuonea na kunyanyasa wengine, kutokujivunia ulivyo nayo, na kujisifia kwa yale unayoyafanya, kutokudharau wengine na kuwapuuza. Andiko linasema “Amdharauye mwenzake afanya dhambi;…” Mit 14:21. Yesu Kristo yeye ni mfano kwetu, alikuwa ni mnyenyekevu aliacha enzi na mamlaka aliyokuwa nayo mbinguni akaja duniani kwa namna ya mtumwa hakutaka makuu na fahari, alimtii Mungu.

5. Kuomba kwa imani.
“Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa , tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba”Yoh 5:14-15. Haya maandiko yanafundisha ni muhimu kujua kwamba tunapomwomba Mungu anatuskia, tunapoomba sawaswa na mapenzi yake (neno lake). Pia kujua tulichoomba tunacho tayari. Kama umemwomba Mungu uponyaji unajua umekuponya. Hiyo ndiyo imani katika Mungu. Ndiyo maana Yesu alifundisha akisema, “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote  myaoombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” Mk 11:24.  

6.  Kuomba kwa bidii.
Kuomba kwa bidii bila kukata tamaa naye Bwana atakuponye kabisa. Iwapo umeomba lakini bado Bwana hajakuponya endelea kunyenyeke na kumlilia tena na tena mpaka Bwana akuponye. Kuna mifano ya watumishi wa Mungu maandiko waliomwomba Mungu kwa bidii tena na tena wakajibiwa. Mmojapo ni Eliya;
“Naye Eliya akapanda juu  mpaka  kilele cha  Karmeli; akasujudu kifudifudi; akainama uso mpaka magotini. Akamwambia mtumishi wake, kwea sasa ukatazame upande wa bahari. Akakwea na kutazama, akasema, hakuna kitu. Naye  akanena, enenda tena mara saba. Ikawa mara ya saba akasema, tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. … Ikawa muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikawa mvua nyingi…” 1Fal 18:42-45. Hapa maandiko yanaonyesha jinsi Eliya alimwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili, wingu la mvua halikutokea lakini hakukata tamaa aliendelea kuomba mpaka mara ya saba wingu likaonekana na mvua ikanyesha. 

Na mwingine aliyeomba kwa bidii na kujibiwa ni Elisha baada ya kumtuma Gehazi mtumishi wake kumfufua mtoto.
“Na Gehazi akawatagulia, akaiweka ile fimbo juu ya mtoto; lakini hapakuwa na sauti wala majibu. Basi Elisha alipofika nyumbani, tazama, mtoto amekwisha kufa, amelazwa kitandani pake. Basi akaingia ndani akajifungia mlango, yeye na Yule mtoto wote wawili, akamwomba Bwana... Kisha akarudi, akatembea nyumbani, huko Na huko mara moja; akapanda akajinyoosha juu yake; Na Yule mtoto akapiga chafya mara Saba, Na mtoto akafumbua macho yake.” 2 Fal 4:31-35. Elisha naye alimtuma mtumishi wake Gehazi akaiweke fimbo juu mtoto abaye alikuwa amekufa ili afufuke, wala hakufufuka, lakini Elisha hakukata tamaa alikwenda mwenyewe akamwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili na mtoto akafufuka.

7. Kumshukuru Mungu. 
“Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” 1The 5:18. Katika maisha yetu ni muhimu tumshukuru Mungu kwa ajili ya mema yote anayotutende kila siku. Kwa Kufanya hivyo ni kutimiza agizo la Mungu kuhusu kushukuru.

Mungu ni mwaminifu kwako.
Usiogope kwa sababu yale yote aliyoyaahidi katika neno lake hakika atayafanya kama alivyosema; “Mimi sitalihalifu agano langu, sitalibadili Neno lililotoka midomoni mwangu.” Zab 89:34. “Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu” Kut 20:6.  “Maana Kama vile mvua ishukavyo, Na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; Bali huinywesha ardhi, Na kuizalisha Na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, Na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure Bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma” Isa 55:10-11.

USHUHUDA. 
Hapa ninatoa ushuhuda wa mtu ambaye Bwana amemponya mara nyingi kwa magonjwa tofauti. Siri ya uponyaji wake ni kwamba yeye ni mtakatifu amejilinda na kuepuka dhambi. 
Amekuwa ni mwenye imani na unyenyekevu, amevunjika na kupondeka moyo. Wakati mwingine anapomwomba Mungu huanguka kifulifuli akimsihi Mungu. Hakika mtu kama huyu atasikilizwa kwa sababu anao ujasiri mbele za Mungu, na ndani  ya moyo wake hakuna dhambi inayomhukumu.
Ndio maana imeandikwa Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.” Ebr 4:16. Mtu anapodumu katika maisha ya kumpendeza Mungu  anapata neema au upendeleo kujibiwa maombi. Wakati mwingine hata kabla ya kuomba hujibiwa. Andiko  linasema “Na itakuwa kwamba, kabla ya kuomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.” Isa 65:24. “….maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.” Mt 6:8.

Maoni

  1. Bila jina18:30

    Mimi naitwa benedicta napatikana mkoani arusha na shida na magonjwa naombeni imani na maombi yenu

    JibuFuta
  2. Bila jina19:26

    Ubarikiwe sana mtumishi Wa Mungu

    JibuFuta
  3. Bila jina22:51

    Barikiwa mtumishi

    JibuFuta

Chapisha Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...

KUWEKWA HURU KUTOKA DHAMBI YA UZINZI NA UASHARATI.

Jambo la kwanza ninamshukuru Mungu kwa neema yake aliyonipa kufundisha neno lake. Ndungu mpendwa ninajua ya kwamba Mungu alikupenda sana, hata akamtoa Mwana wake wa pekee Yesu Kristo kwa ajili yako ili akukomboe kutoka katika dhambi zote ikiwemo dhambi ya uzinzi na uasherati. Sasa ninakusihi kwa neema ya Mungu fuatana nami kwa makini kuhusu  somo hili nawe utauna utukufu wa Mungu katika maisha yako. Tunaweza kuangalia kwa makini dhambi ya uzinzi na uasharati ambayo mtu akiitenda inaharibu ufahamu wake na hatimaye kuangamia. Mtu anapoteza uhusiano wake na Mungu, mawasiliano kati yake na Mungu yanakatika. Mungu  ni Makatifu hana ushirika na wenye dhambi. “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.” Mithali 6:26.   “Lakini maovu yenu yamewafarikisha (yamewatenganisha) ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki  kusikia.”   Isahau 59:2. Atendaye dhambi ya zinaa au  uasherati ...

KUDUMU KATIKA UPENDO WA MUNGU.

Neno la Mungu katika Biblia linatufudisha kuhusu upendo wa Mungu  kwetu. Yeye Mungu ndiye  mwanzo wa upendo kwa sababu alitupenda kwanza. “...alitupenda sisi kwanza”.   1 Yohana 4:19. Jinsi mtu anavyoweza kuwa na upendo wa Mungu. Ni pale mtu anapokuwa amezingatia kudumu katika upendo wa Mungu kama ifuatavyo; 1.Kuishi sawasawa na maagizo yote ya neno la Mungu na kumpenda. “Na sasa, Israeli, BWANA, Mungu wako, anataka nini kwako, ila umche BWANA, Mungu wako, na kwenda katika njia zake zote, na kumpenda, na kumtumikia BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote;”   Kumbukumbu la Torati 10:12.   “Lakini mjibidiishe sana kuzifanya amri na sheria, ambazo Musa, mtumishi wa BWANA, aliwaamuru, kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kwenenda katika njia zake zote, na kuzishika amri zake, na kushikamana na yeye, na kumtumikia kwa moyo wenu wote na nafsi yenu yote”.   Yoshua 22:5. 2. Jambo lingine la kuzingatia ni kwamba yampasa mtu kuyashika maagiz...

MADHARA YA DHAMBI.

Huu ni wakati mwingine ambao Bwana amenijalia kuwepo kwa kusudi lake jema. Nitaelezea katika somo hili kuhusu dhambi ilivyo na madhara kwa mtu aitendaye. Kwanza tuangalie dhambi  ilivyoanza kwa Adamu na Hawa ni wakati walipokula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambayo Mungu aliwakataza wasile. Kwa sababu hiyo dhambi ilisababisha madhara mengi kwa uzao wake na vizazi vyote duniani. Kwa hiyo shida zote zilizopo duniani zimetokana na dhambi. Kutokana na wazazi wetu wa kwanza Adamu na Hawa kwa kuwa walitenda dhambi na vizazi vingine vyote vimehesabiwa ni wenye dhambi. Mtu  anazaliwa akiwa na asili ya dhambi kutoka kwa wazazi wa kwanza Adamu na Hawa. Warumi 3:23 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;” Kutokana na sababu hiyo ndio maana kila mwanadamu anakufa sawasawa na Mungu  alivyosema katika kitabu cha Mwanzo 2:16-17 “BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa u...