Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KUOA NA KUOLEWA.

Kanuni ya Mungu kuhusu kuoa na kuolewa
1. Mungu alianzisha ndoa ya watu wawili mume na mke wakati alipowaumba. Imeandikwa, “…. Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja”. Mwanzo 1:27; 2:24.

Tunaweza kuona mfano mzuri  kwa Nuhu ambaye aliku mcha Mungu yeye na watoto wake watatu wa kiume kila mmoja alioa mke mmoja. “Siku ile ile Nuhu akaingia katika safina, yeye, Shemu na Hamu na Yafethi, wana wa Nuhu, na mkewe Nuhu, Na wake watatu wa wanawe pamoja naye”.  Mwanzo 7:13.   Kwa kuwa Nuhu na familia yake walikuwa watu wa haki, Mungu hakuwaangamiza kwa ngarika akawahifadhi salama katika safina.

2.Aliyeamini asioane au kuolewa na asiyeamini kwa sababu imeandikwa, “Msifungiwe nira na wasioamini, kwa jinsi isivyo swasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya uasi na haki? Tena pana ulinganifu gani na Kristo na Beliari? (ufisadi au uchafu) Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini…. Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, nitakaa ndani yao, na katikati yao nitatembea nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu”. 2Wakorintho 6:14-16.

Lakini  wale ambao walikwisha kuoana kabla ya kuamini (kuokoka) na mmojawapo akaamini asimwache yule ambaye hajaamini kama ilivyoandikwa  ….iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache. Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache muwewe”. 1Wakorintho  7:12; 13  

3.Mungu amezuia kuoana na jamii ya karibu kiukoo. 
Imeandikwa, “Mtu ye yote wa kwenu asimkaribiye mwenziwe aliye wa jamaa yake wa karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana”.  Walawi 18;1. Ndungu msomaji maandiko  yaliyosalia sikuyaandika hapa,  unaweza kuyasoma  katika  biblia yako nawe utajengwa Walawi 18:2-17.

Jinsi ya kumpata mke au mume mwenye busara.
1.Hupatikana kwa Bwana. “Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana. Nyumba na mali ni urithi apatao mtu kwa babaye; Bali mke mwenye busara, mtu hupewa na Bwana”.  Mithali 18:22; 19:14

2.Anayeishi sawasawa na neno la Mungu.
“Yeye aendaye kwa unyofu wake kumcha Bwana. Mithali 14:2. Hufunua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema i katika ulimi wake”. Mithali 31:26.

3. Kumwomba Mungu kwa imani naye atakupa. Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba. 1Yohana 5:14,15. Msijisumbue  kwa neno lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba pamoja na kushukuru, na haja zenu zijulikane na Mungu”. Wafilipi 4:6.

Hapa Neno  la Mungu linatufudisha kumwomba Mungu katika mambo yote, kwa sababu pasipo yeye hatuwezi neno lolote. Kwa maneno mengine hatutafanikiwa katika mambo yetu bila kuomba. Ndio maana imeandikwa,  kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga…” Yakobo 1: 17.  

Waliokwisha kuoa au kuolewa wakiwa wameamini  hawaruhusiwi kuachana.
“Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe”. 1Wakorintho 7:10,11. “Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini”. Luka 16:18. Pia kila mwanamke amwachaye mumewe akaolewa na mume mwingine azini. Maana mimi nachukia kuachana, asema Bwana Mungu wa Israeli…”  Malaki 2:16.

Onyo kuhusu tamaa mbaya
“Mmesikia kwamba imenenwa, usizini; lakini mimi nawaambia, kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake”. Mathayo 5:27;28. Andiko hili pia linawahusu wanawake. Kila mwanamke amtazamaye mwanaume kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni. “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasharati na wasinzi Mungu atawahukumia adhabu”. Waebrania 13:4.

“Lakini uasharati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wala kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu  Maana neno hili mnalijua hakika, hakuna mwasharati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalume wa Kristo na Mungu” Waefeso 5:3;5. Maandiko haya yanaonya kila mtu asifanye uasharati. afanyaye uasharati ni chukizo kwa Mungu, atahukumiwa na kutupwa  jehanum kwenye moto usiozimika na kuteseka milele. Na moshi wa maumivu yao hupanda juuhata milele na milele wala hawana raha mchana na usiku…”Ufunuo 14:11.  

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...