Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2013

KUISHI KATIKA AMANI.

Kuishi kwa amani ni jambo la muhimu sana katika maisha yako, ikiwa umekwisha kumpokea Yesu Kristo na Roho mtakatifu .  Utaweza kuamua mambo mbalimbali kwa kumwomba Mungu akupe    ufumbuzi. Neno la Mungu linasema;   “Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu...”  Kol 3:15.  Hapa ninatoa ushuhuda   wangu, katika maisha yangu nimekutana na mambo magumu yanayohitaji maamuzi. Lakini kwa kuwa nilimwomba Bwana hakukawia, alinijalia kuwa na wazo    la uamuzi wa kutoa, na ndani ya moyo wangu nilikuwa na amani. Na yote niliyoyatolea maamuzi yalikuwa ni sahihi sawasawa na mwongozo wa Mungu. Kufanya kazi kwa haki.   Kama wewe ni mwalimu, daktari, kiongozi, mfanyabiashara, askari au unafanya kazi yoyote inakupasa kuifanya    kwa haki. Kwa kufanya hivyo ndipo utakuwa na amani na utulivu moyoni mwako; na pia utakuwa na haki ya kumtumaini Mungu kama ilivyoandikwa,  “Na kazi ya haki itakuwa amani; na mazao ya haki yatakuwa utulivu ...

UPONYAJI WA MAGONJWA.

Chanzo cha magonjwa. Kuna magonjwa yanayotokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya yule mtu ambaye aliyekuwa mngonjwa akamwabia,   “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi”   Yn 5:14.   Ikiwa mtu aliyeokoka akirudia kuishi maisha ya dhambi pepo mchafu anapoona nafasi anachukua pepo wengine na kuingia kwake. Yesu alisema,  “Mara huenda akachukua pamoja naye    pepo    wengine walio waovu    kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”   Mt 12:45.    Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili. Kwa upande mwingine mtu anaweza akawa ni mgonjwa au amekosa lishe.  Uponyaji wa Mungu.                     Mambo ya kuzingatia na kuponywa ni ha...

IMANI.

Chanzo cha imani “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”   Rum 10:17.  Imani inatokana na neno la Kristo au neno la Mungu, mtu akilisikia neno na kulifahamu na kuliamini anakuwa na imani katika neno la Mungu. Ni jambo la msingi na muhimu kuliamini neno, ndio maana Mungu amesema;   "Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita; roho yangu haina furaha naye”   Ebr 10:38. Kuamini neno la Mungu. Asiyeamini neno la Mungu hampendezi Mungu bali amemwasi, hataingia mbinguni. Wana wa Israel walikufa jangwani kwa sababu hawakuamini maneno ambayo Mungu aliowaambia.   “Tena ni akina nani aliochukizwa nao miaka arobaini? Si wale waliokosa, ambao mizoga yao ilianguka jangwani? Tena ni akina nani aliowaapia ya kwamba hawataingia katika raha yake   (mbinguni),   ila wale walioasi? Basi twaona ya kuwa hawakuweza kuingia kwa sababu ya kutoamini kwao. Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vil...