Ruka hadi kwenye maudhui makuu

TUNDA LA UPENDO.

Tunda hili linadhihirisha upendo wa Mungu kwa wanadamu  ijapokuwa ni wenye dhambi ambao hawastahili mbele zake. Mungu ni wa kwanza kutupenda kwa sababu andiko linasema, “....Yeye alitupenda sisi kwanza. 1Yoh 4:19".  Ndio maana alimtoa mwanawe Yesu Kristo aje hapa duniani ili kupitia yeye  kila mtu aokolewe na kuwa na uzima wa milele. Ndio maana imeandikwa, “....Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili  kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye Yn 3:16-17."

Kwa upendo wake Mungu alitupenda bure,  na kwa neema yake akamtuma Mwanawe Yesu Kristo aje  kutupatanisha na Mungu. Ndio maana andiko linathibitisha kwa kusema, “Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu 1Yoh 4:10." Kwa sababu Mungu alitupenda yatupasa sisi kumpenda kama andiko linavyosema, “Wapenzi, ikiwa Mungu alitupenda hivi, imetupasa na sisi kupendana. Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati  wowote. Tukipendana Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilishwa ndani yetu....Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake. 1Yoh 4:11-12, 16."

Mambo ya kuzingatia na kuishi katika pendo Mungu. Ni haya ifuatavyo:
1. Kuzitii sheria za Mungu.
“Katika hili twajua kwamba twawapenda watoto wa Mungu , tumpendapo Mungu, na kuzishika amri zake.” 1Yoh 5:2. Anayeishi katika pendo siku ile ya mwisho hatahukumiwa. “Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo na sisi tulivyo ulimwenguni humu, Katika pendo hamna hofu ; lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa maana hofu ina adhabu, na mwenye hofu hakukamilishwa katika pendo.” 1Yoh 4:17-18.

2. Kupendana kila mtu na mwenzake. Haiwezekani kumpenda Mungu bila sisi kupendana. Ndio maana imeandikwa, “Mtu akisema, nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake,ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.” 1Yoh 4:20-21.  

3. Kuwapenda adui zetu na wale wanaotuudhi. Kwa kuwa Yesu alinasema, “....Wapendeni adui zenu waombeeni wanaowaudhi; ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni....Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu. Mt 5:44-45,48."

4. Kuepuka  kuipenda dunia na mambo yake.
Kuipenda dunia na mambo yake ni pale mtu anapokuwa na tamaa mbaya. Kwa hiyo mtu aliye na tamaa mbaya kila kitu anacho kiona anataka awe nacho. Kwa mfano ameona toleo jipya la simu, viatu, nguo, au kitu kingine chochote anakitamani. Jambo la msingi hapa yampasa mtu kupanga na kuzingatia yale mahitaji ya muhimu katika maisha. Imeandikwa “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. Maana kila kilichopo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia. Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.” 1Yoh 2:15-17."

"1 Timotheo 6
6 Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa.

7 Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu;

8 ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.

9 Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu.

10 Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi."

Kutokana na  maandiko hayo yanatufundisha jinsi ya kuepuka tamaa mbaya, ni pale   tunaporidhika kwa yale mahitaji yote ya muhimu katika maisha yetu. Kwa sababu hiyo tunakuwa na kiasi katika maisha yatu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

KUMTUMIKIA MUNGU KWA BIDII.

Kutokana na kichwa cha somo hapa juu katika matukio wazi ili mtu amtumikie Mungu ni lazima awe na bidii. Kwa sababu hiyo kwa mtu yule ambaye ameweka nia moyoni mwake ya kwamba atatumikia Mungu kwa bidii. Tukiangalia kuhusu mwanadamu kuna mambo mengi katika maisha yake ameyafanya kutokana na bidii aliyo nayo. Lakini ikiwa mtu hana bidii kwa ajili ya mambo ya Mungu kamwe hawezi kuingia ufalme wa Mungu. Ndio maana imeandikwa;  "Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatimkana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka,   Mathayo 11:12 ."    " Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu."   Luka 16:16. Hapa ninatoa ushuhuda wangu binafsi, kuhusu kumtumikia Mungu kwa bidii. Wakati nilipookoka nilikuwa na kiu au shauku kwa ajili ya kutaka kujazwa Roho Mtakatifu. Kwa sababu nilikuwa ninamhitaji sana nilimwomba mtumishi mmoja wa Mungu aniombee ili niweze kujazwa...

KUISHI MAISHA YA UTAKATIFU.

Utakatifu  - Ni maisha ya Mkristo anayoyaishi kwa kuzingatia kanuni ya neno la Mungu baada ya kumkiri na kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yake. Kuishi maisha ya utakatifu ni jambo linalowezekana, kwa sababu Mungu alipomuumba mwanadamu alimwekea hiari ndani yake kwa kutokea kwa tukio. Ndio maana Yesu alipokuwa akifundisha alitumia mfano wa mti kuonyesha mtu anavyoweza kuishi maisha haya ya kumpendeza Mungu au ya maisha ya dhambi. "   "Ufanye mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri, au ufanye mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana" Mathayo 12:33. Kuishi maisha ya utakatifu ni agizo la Mungu kwa wale wote aliowachagua. Ndio maana Mungu alimwambia Musa,   "Nena na makutano wote na wana wa Israel, uwaambie, mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi Bwana Mungu wenu ni mtakatifu"  Walawi    19:2. Kuwa mtakatifu ni kumpendeza Mungu, kwa sababu amesema;  “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora...

TUNDA LA UAMINIFU.

Uaminifu ni mojawapo ya tunda la Roho katika maandiko matakatifu. Tutajifunza uaminifu wa Mungu unaopatikana katika neno lake. Yeye amesema atatimiza yale aliyoahidi katika neno lake, si tu kwa wana wa Israel bali kwa watu    wote wanaoishi sawasawa na neno lake. Kwa hiyo, kwa upande wetu inatupasa sisi nasi kuwa waaminifu kwa kuliishi na kulitenda neno la Mungu.   “Basi jueni ya kuwa Bwana, Mungu wenu, ndiye Mungu; Mungu mwaminifu, ashikaye agano lake na rehema zake kwao wampendao, na kushika amri zake, hata vizazi elfu.   Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako.”   Kum 7:9, 12.   “Ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu    halitanirudia bure bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma.   Isa 55:11" Tabia ya mtu mwaminifu. 1. Mtu aliye mwaminifu ni yule ambaye anatenda sawa...