Ahadi ya Mungu.
Mungu aliahidi kwa kinywa cha nabii Yoeli wakati wa agano la kale
akasema nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili. Alikuwa anausemea wakati
wa sasa ambao ni wa angano jipya. “Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina
roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri,
wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono, tena juu ya watumishi
wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile nitamimina roho yangu” Yoeli 2:28,29.
Ni nani atampokea Roho Mtakatifu?
1) Anayetubu na kusamehewa.
“Petro akawaambia, tubuni mkabatizwe kila
mmoja kwa jina la Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea
kipawa cha Roho mtakatifu” Matendo 2:38.
2) Anayemtii Mungu.
Anayemtii Mungu ni mtu yule aliyemwamini Yesu na kuokoka na
kuweka nia ya kuishi sawa sawa na neno la Mungu, huyo hakika atampokea Roho
Mtakatifu. “Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, pamoja
na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wote wamtiio” Matendo 5:32.
3) Aliye na kiu na
kumwamini Yesu. “…Yesu akasimama; akapaza sauti yake
akasema, mtu akiona kiu (kutamani), na aje anywe. Aniaminiye, kama vile
maandiko yanavyonena, mito ya maji yalio hai itatoka ndani yake. Na neno hilo
alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminiye watampokea badaye; kwa
maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa” Yohana 7:37-39.
4.Yampasa kukubali ubatizo halisi ambao Mungu alimtuma Yohana abatize watu kwa kuwazamisha ndani ya maji mengi. Haiwezekani kwa mtu ambaye anampinga Mungu kuhusu ubatizo halisi wa kuzamishwa katika maji mengi, halafu akampokea Roho Mtakatifu. Ni jambo la muhimu kufahamu ya kwamba ubatizo sahihi ni ule ambao Mungu alimwagiza Yohana hata akambatiza Yesu ili kutimiza majawapo ya agizo la Mungu. Kwa kuwa Yesu alikuwa anayafahamu maagizo ya Mungu alifundisha na kuonyesha ya kwamba ni jambo la lazima mtu azaliwe kwa maji na roho na ndipo ataingia mbinguni. Ndio maana, “Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu. Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.” Yohana 3:5-6.
Maana ya kuzaliwa kwa maji na roho.
Kuzaliwa kwa maji ni wakati mtu anapobatizwa kwa kuzamishwa ndani ya maji mengi. Pia mtu huzaliwa kwa roho wakati ameamua kuokoka na kumwamini Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake kwa kutubu na kuziacha dhambi.
Mtu anaweza kumpokea Roho Mtakatifu akiwa na imani na utakatifu. Kama mtu hana imani na utakatifu haiwezekani akampokea Roho Mtakatifu. Siyo sahihi mwamini yeyote kufikiria ya kwamba mtu anaweza kujazwa Roho Mtakatifu kwa imani bila kuwa na utakatifu. Ni lazima mwamini awe na utakatifu kwa kuwa Roho Mtakatifu yeye ni Mtakatifu, hukaa na wale walio watakatifu.
Maana ya kuzaliwa kwa maji na roho.
Kuzaliwa kwa maji ni wakati mtu anapobatizwa kwa kuzamishwa ndani ya maji mengi. Pia mtu huzaliwa kwa roho wakati ameamua kuokoka na kumwamini Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake kwa kutubu na kuziacha dhambi.
Mtu anaweza kumpokea Roho Mtakatifu akiwa na imani na utakatifu. Kama mtu hana imani na utakatifu haiwezekani akampokea Roho Mtakatifu. Siyo sahihi mwamini yeyote kufikiria ya kwamba mtu anaweza kujazwa Roho Mtakatifu kwa imani bila kuwa na utakatifu. Ni lazima mwamini awe na utakatifu kwa kuwa Roho Mtakatifu yeye ni Mtakatifu, hukaa na wale walio watakatifu.
Ni wakati gani mtu anajazwa Roho
Mtakatifu?
1). Mtu anajazwa Roho Mtakatifu wakati anapofanya maombi.
“Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali
pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu …” Matendo 4:31. Pia mtu anaweza kujazwa Roho Mtakatifu akiwa ananwabudu na
kumsifu Mungu. Au wakati anapobatizwa.
Kinachotokea mtu anapojazwa Roho Mtakatifu
1). Anapokea nguvu ndani yake na
ujasiri wa kuwa shahidi wa Yesu.
Anakuwa na nguvu ya kushinda dhambi, na ujasiri wa kuhubiri habari
njema za ufalme wa Mungu.“Lakini mtapokea
nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi
katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa
nchi.…wote wakajaa Roho mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri” Matendo 1:8, 4:31.
2). Roho Mtakatifu anakaa ndani yake. “Ndiye Roho wa kweli, ambaye ulimwengu
hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala kumtambua; bali ninyi mnamtambua,
maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu” Yohana 14:17.
3). Anasema kwa lugha nyingine. Anajaliwa na Roho Mtakatifu kusema kwa
lugha nyingine. “Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza
kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka” Matendo 2:4.
Ni kwa nini Roho Mtakatifu alikuja kwetu? Majibu ya swali hili ni kama ifuatavyo:
1). Alikuja ili awe msaidizi wetu na
kukaa nasi. Yeye
anatusaidia katika maisha yetu mambo mengi. “Nami nitamwomba Baba, naye atawapa msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata
milele. Ndiye Roho wa kweli…”Yohana 14:16, 17.
2). Kutusaidia kuomba.
“Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu
wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo; lakini Roho mwenyewe hutuombea
kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho
ilivyo kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu” Warumi 8:26, 27.
3). Kutuongoza na kutuambia mambo
yajayo. “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa
kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake
mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha
habari yake. Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatoa katika yaliyo yangu na
kuwapasha habari. Na yote aliyo nayo Baba ni yangu, kwa hiyo nalisema ya kwamba
atatoa yaliyo yangu na kuwapashani habari” Yohana 16:13-15.
“Kwa kuwa wote wanaongozwa na Roho wa
Mungu, hao ndio wana wa Mungu” Warumi 8:14. Neno linaonyesha wazi wanaongozwa na
Roho mtakatifu ni wana wa Mungu, ambao wamekwishafanyika watoto wa Mungu kwa
kumpokea Yesu. “Bli wote waliompokea waliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa
Mungu, ndio wale waliaminio jina lake” Yohana1:12.
4). Kutufundisha na kutukumbusha.
“Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu,
ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha
yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia” Yohana 14:26.
5). Kutumiminia pendo la Mungu katika
mioyo yetu.
“…kwa maana pendo la Mungu limekwisha
kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu aliyetupa sisi” Warumi 5:5.
6). Kuuhakikishia ulimwengu dhambi, haki
na hukumu.
“…huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi
nikienda zangu, nitampeleka kwenu. Naye akiisha kuja, huyo atauhakikishia
ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu” Yohana 16:7,8. Roho Mtakatifu anauhakikishia
ulimwengu kwa habari ya dhambi, haki na hukumu wakati watumishi wa Mungu
wanapohubiri na kufundisha neno la Mungu.
7.Kutushuhudia kuwa watoto wa Mungu.
“Roho mwenyewe hutushuhudia pamoja na roho
zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu.” Warumi 8:16. Ukiishi sawasawa na neno la Mungu Roho
mtakatifu anakushuhudia
ndani yako ya kwamba wewe ni mtoto wa Mungu. Kama neno la Mungu linavyofundisha
waliompokea Yesu walipewa haki ya kuwa watoto wa Mungu. Lakini haki hii
hawakuipata bila kujitolea au kujikabidhi kwa Mungu. Walimgeukia Mungu na kuacha
maovu yote kwa kutubu na kusamehewa, ndio maana walifanyika watoto wa Mungu.
Barikiwa na somo
JibuFuta